Waziri mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, amesema kuwa Uislamu iwe wa Sunni au Shia ni tishio kwa dunia nzima, kauli ambayo imezua mjadala na ukosoaji katika duru za kimataifa.
Netanyahu alidai kuwa changamoto kubwa kwa usalama wa kimataifa inahusishwa na makundi yenye msimamo mkali yanayojihusisha na itikadi za Kiislamu, akisisitiza kuwa jamii ya kimataifa inapaswa kuchukua hatua kukabiliana na kile alichokiita hatari hiyo.
Kauli hiyo imeibua hisia tofauti, huku baadhi ya
wachambuzi wakisema inaweza kuongeza mvutano wa kidini na kisiasa katika maeneo mbalimbali duniani.
