Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Wakurugenzi Katavi Kikaangoni ......Mkuu wa Mkoa Awataka Warejeshe Milioni 200 Walizolipa Watumishi Hewa

Wakurugenzi Katavi Kikaangoni ......Mkuu wa Mkoa Awataka Warejeshe Milioni 200 Walizolipa Watumishi Hewa

Picha
Wakurugenzi wa Halmashauri zote mkoani Katavi, wameagizwa kurejesha Sh200 milioni wanazodaiwa kuwalipa watumishi hewa ndani ya siku 21. Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Meja Jenerali mstaafu, Raphael Muhuga alitoa agizo hilo jana katika kikao baina yake na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa pamoja na waandishi wa habari. Alikuwa akitoa taarifa ya kubainika kwa watumishi hewa wapya mkoani humo. Muhuga alisema kuendelea kubainika kwa watumishi hao hewa, itawabidi wakurugenzi kuhakikisha fedha zote zilizolipwa kwa watu hao zinarejeshwa serikalini kwa muda aliowataka wazirejeshe na wampatie taarifa itakayothibitisha fedha hizo kurejeshwa. Pia, mkuu huyo wa mkoa aliagiza maofisi wa ofisi ya utumishi wachukuliwe hatua ya kinidhamu kwa kusababisha watumishi hao hewa kulipwa fedha. “Hili siyo suala la bahati mbaya, bali hawa watu walidhamiria kulipa mishahara hiyo hewa naimani wapo wenye maslahi juu ya jambo hili,”  alisema Muhuga. Aliagiza wakurugenzi wote wa halmashauri, waha...