Shirika La Umeme Tanzania Tanesco Lazindua ”Tanesco Huduma";
Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (Tanesco), limezindua huduma mpya inayotoa nafasi kwa wateja kutoa na kupata taarifa kupitia mfumo wa mawasiliano uliounganishwa kwenye simu za kiganjani unaoanza kwa majaribio katika mkoa wa kihuduma wa Kinondoni Kaskazini. Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Mhandisi Felchesmi Mramba alisema jana jijini Dar es salaam kuwa, mfumo huo ambao uko kwenye programu maalumu, utasaidia kuboresha utendaji kazi wa shirika. “Mfumo huu utaongeza kasi ya uwajibikaji wa watendaji kuwahudumia wananchi, lakini kwa sasa tumeuanza kwa majaribio katika mkoa wetu wa Kinondoni Kaskazini, wateja wetu watatoa taarifa za matukio yanayowakabili hata wale wanaoomba rushwa, watujulishe tupate ushahidi tuchukue hatua,” alisema Mramba. Alisema mfumo huo umeundwa kutokana na ushirikiano kati ya Tanesco na Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania (Costech) na alisema itawapunguzia usumbufu wateja wa kupiga simu kwenye vituo vya huduma wanapokuwa na malalamiko binafsi a...