Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Hukumu ya Kesi Kafulila Kupinga Matokeo ya Uchaguzi Itatolewa Mei 17

Hukumu ya Kesi Kafulila Kupinga Matokeo ya Uchaguzi Itatolewa Mei 17

Picha
Mahakama  Kuu ya Tanzania Kanda ya Tabora inayosikiliza kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi ya Jimbo la Kigoma Kusini iliyofunguliwa na aliyekuwa mgombea wa jimbo hilo, David Kafulila inatarajia kutoa hukumu Mei 17, mwaka huu. Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Tabora anayesikiliza kesi hiyo mjini Kigoma, Ferdinand Wambali alisema baada ya pande zote kuwasilisha ushahidi na maelezo yao mahakamani hapo amepanga kutoa hukumu tarehe hiyo. Kutolewa kwa tarehe hiyo ya hukumu kunatokana na kufungwa kwa utoaji ushahidi wa maelezo ya kesi hiyo ambayo aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza, Ruben Mfune ambaye alikuwa msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo, aliwa mshitakiwa wa tatu katika kesi hiyo. Baada ya kukamilika kwa ushahidi wa pande zote, Jaji Wambali ameomba kupatiwa muda wa kutosha kupitia ushahidi na vielelezo vilivyowasilishwa mahakamani hapo ili atoe hukumu ya haki. Katika kesi hiyo Namba Mbili ya mwaka 2015, David Kafulila aliyekuwa mgombea ubunge wa jim...