Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Bandari yajitetea matishari mabovu Tanga

Bandari yajitetea matishari mabovu Tanga

Picha
Ufisadi ulioibuliwa hivi karibuni na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwenye bandari ya Tanga, bado unaitesa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), ambayo imetoa taarifa ndefu ya kujitetea huku ikikiri kwamba matishari hayo hayajafanya kazi tangu yanunuliwe. Matishari hayo yaliyonunuliwa kwa Dola za Marekani 10,113,000 sawa na zaidi ya Sh. bilioni 21, hayajafanya kazi kwa miaka mitano licha ya kwamba muuzaji ameshalipwa asilimia 87 ya malipo yake. Mamlaka hiyo imetoa taarifa kuelezea mchakato mzima wa ununuzi ulivyoanza mwaka 2011 hadi matishari hayo kufika katika bandari ya Tanga. Kwa mujibu wa tarifa ya TPA, matishari hayo kwa mujibu wa mkataba wao na muuzaji yalipaswa kusafirishwa kwa njia ya kubebwa na meli lakini haikuwa hivyo. Ilisema matishari hayo yalivutwa kutumia boti badala ya kubebwa na meli kama walivyokubaliana kwa madai kuwa matishari hayo yalikuwa makubwa mno kupakiwa kwenye meli. Ilisema wakati yakiwa njiani kuja nchini, yalikumbana na dhoruba ya kimbunga kikali baharini...