Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya VODACOM GLOBAL WAWASOGEZA WASANII KWA MASHABIKI WAO

VODACOM GLOBAL WAWASOGEZA WASANII KWA MASHABIKI WAO

Picha
Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu akiongea na wanahabari wakati wa uzinduzi huo leo. KAMPUNI ya Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na Global Publishers & General Enterprises Ltd, leo wamezindua huduma itakayowawezesha wateja wake kupata habari juu ya maisha ya kila siku ya wasaniii mbalimbali hapa nchini.Akizungumza na wanahabari katika makao makuu ya Vodacom yaliyopo Mlimani City jijini Dar es Salaam, Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu, alisema huduma hiyo itagharimu kiasi cha shilingi mia moja tu (100/=) kwa siku, ambapo mteja atakuwa akipokea taarifa za msanii aliyemchagua kila siku kwa bei hiyo. “Ili kujiunga na huduma hii, mteja anatakiwa kutuma jina la msanii mfano, Shilole au Kajala kwenda namba 15542, na hapo moja kwa moja atakuwa amejiunga na kuanza kupata habari za msanii husika. “Kila siku mteja atakuwa anakatwa Sh 100 kwa ajili ya huduma hiyo, pia kwa kiwango hicho cha fedha kwa siku moja anaweza kupata taarifa za msanii h...