RASHFORD AIPELEKA MAN U NUSU FAINALI FA
Hewala si Utumwa, msemo huu unatua Old Trafford katika Jiji la Manchester United kwa kijana Rashford aliyeiumiza Arsenal na kutengeneza Rekodi yake mwenyewe katika Derby la Manchester kufunga goli akiwa na miaka 18 hakuna aliewahi kufanya hivyo lakini yeye anazidi kufanya mengi ndani ya Manchester. Ushindi wa magoli 2-1 walio upata Manchester United unaipeleka moja kwa moja katika Nusu Fainali ya kombe Kongwe Duniani FA, Goli la Marcus Rashford lilikuwa goli bora katika maisha ya Kinda huyu alipiga kwa ufundi wa aina yake na nyota inaonesha huenda akaisaidia England hapo Baadae. MICHEZO INAYOFUATA Sasa hatua hii itachezwa pale katika uwanja mkubwa nchini England ambao unaingiza watu elfu tisini 900,000 na atakutana na Everton siku ya jumamosi wakati Crystal Palace atakutana na mbabe wa Arsenal kwenye michuano hii ambaye Watford siku ya Jumapili. JUMAMOSI 23/04/2016 Manchester United VS Everton JUMAPILI 24/04/2016 Cystal Palace VS Watford