Kikwete Ataka Vijana Duniani Wathaminiwe na Kuwezeshwa
Rais Mstaafu wa awamu ya Nne, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete amesema, ingawa idadi kubwa ya vijana wasiokuwa na uhakika wa maisha yao wala kazi zenye tija na staha wapo katika nchi zinazoendelea, dunia katika ujumla wake inapashwa kuonyesha utashi wa kisiasa na udhubutu wa kuwekeza kupitia vijana. Amesema, mazingira ya mamilioni ya vijana kukaa bila shughuli ya aina yote kunatoa mwanya kwa vijana hao kurubuniwa na kutumiwa na watu wasiokuwa na nia njema na hivyo kutishia hali ya Amani, usalama na ustawi wa mwanadamu na hatimaye kushindwa kufikia au kupata faida za kidemografia na maendeleo endelevu. Mhe. Kikwete ameyasema hayo ( jumanne) hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, wakati alipotoa mhadhara wa 13 wa kumbukumbu ya Rafael M. Salas. Mhadhara huu ambao mada yake ilikuwa ni ...