YANGA VS TOTO,PLUIJM ANENA HAYA...!!!
KOCHA wa mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga, Hans Pluijm ametamba timu yake leo kuibuka na ushindi dhidi ya Toto Africans ili kuzidi kukaribia kutetea taji hilo. Akizungumza wakati wa mazoezi ya timu hiyo jijini hapa, Pluijm alisema kuwa licha ya uzuri wa Toto Africans, lakini wataibuka na ushindi katika mchezo huo wa leo CCM Kirumba. Alisema wachezaji wake mwanzo mwisho watacheza kwa kujituma huku wakilishambulia kwa nguvu lango la Toto African wakisaka pointi tatu muhimu. “Toto African ni timu iliyojaa wachezaji wadogo wanaojituma na wanacheza mpira mzuri sana. Jambo muhimu kwetu ni kuhakikisha tunashinda kila mechi ili tuweze kubaki kileleni mwa Ligi Kuu na kutwaa taji,“ alisema Pluijm. Hata hivyo, Pluijm alithibitisha kikosi chake kuwa na majeruhi, lakini amesema wameziba mapengo hayo. “Golikipa wetu Barthez na Godfrey Mwashiuya ni majeruhi ila nina imani mapengo yao yatazibwa na wachezaji waliopo,” alisema Pluijm. Kwa upande wake kocha mkuu wa...