BREAKING NEWS: RAIS MAGUFULI AMFUTA KAZI MKURUGENZI WA JIJI LA DAR
Rais wa Jmhuri ya Muungano wa Tanzania ametangaza kumfuta kazi Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam Wilson Kabwe. Hatua ya kumfuta kazi Mkurugenzi huyo imefuata baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda kumwambia Rais Magufuli wakati wa Uzinduzi wa Daraja la Kigamboni, kuwa Mkurugenzi huyo wa Jiji alisaini mikataba kadhaa ambapo mmoja kati ya hiyo imelisababishia taifa hasara ya shilingitakribani bilioni 3 tangu 2009- 2015.