Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Waziri Ataka Wakurugenzi NHC Washindanishwe

Waziri Ataka Wakurugenzi NHC Washindanishwe

Picha
NAIBU  Waziri  wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo  ya Makazi, Angeline Mabula, ametaka wakurugenzi  wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika mikoa yote washindanishwe   kujua utendaji kazi wao. Waziri Mabula, alitoa kauli hiyo Dar es Salaam mwishoni mwa wiki  wakati akifungua  kikao cha Baraza Kuu la Wafanyakazi  wa shirika hilo kilichokuwa kikijadili mipango na makisio  ya mapato na matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka 2016/17 kabla ya kuwasilishwa bungeni. Alisema  hatua hiyo itasaidia kutambua wakurugenzi ambao wanasubiri kubebwa na wenzao kwa kushindwa kufanya kazi kwa weledi. Alisema ujenzi na ununuzi wa nyumba unahitaji fedha nyingi, wananchi hununua nyumba kupitia mikopo kutoka benki. "Serikali inatambua umuhimu wa taasisi za fedha  katika kusaidia ukuaji  wa sekta ya nyumba jambo ambalo hufanywa duniani kote, " alisema. Alisema Serikali inatambua bado kuna changamoto  ya riba kubwa ya mikopo  ya nyumba...