Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Wahalifu Wawekewa Mkakati Mzito Mkoani Dodoma

Wahalifu Wawekewa Mkakati Mzito Mkoani Dodoma

Picha
Katika kuhakikisha wahalifu hawapati nafasi ya kutamba nchini,  makamanda wa Polisi wa mikoa, wakuu wa upelelezi na waendesha mashtaka wameazimia kuboresha ushirikiano wao katika kufanikisha kesi za wahalifu pindi zinapofikishwa mahakamani ili waweze kupewa  adhabu kali kwa mujibu wa sheria. Hayo yamo katika maazimio ya watendaji hao wa haki jinai nchini katika kikao kazi cha siku mbili kilichofanyika  mkoani Dodoma na kuwashirikisha makamanda wa polisi wa mikoa,  mawakili wafawidhi wa mikoa  na wakuu wa upelelezi wa mikoa. Kikao hicho kilikuwa chini ya uenyekiti wake Mkuu wa Jeshi la Polisi,  IGP Ernest Mangu pia kilihudhuliwa na mkurugenzi wa Mashtaka nchini, DPP  Biswalo Mganga, Makamishina wa Polisi, pamoja na taasisi mbalimbali zinazohusika na upelelezi na uendeshaji wa mashtaka. Wapelelezi hao na waendesha mashtka walisema wataendeleza  program za mafunzo ya pamoja katika ngazi ya mkoa, kufanya vikao vya mara kwa mara ili kujadili chang...