Sababu 10 za Maumivu ya Tumbo Wakati wa Mimba
Maumivu ya tumbo wakati wa miezi mitatu ya kwanza ya mimba ni mojawapo ya matatizo yanayolalamikiwa na kina mama wengi.Kuna matatizo mengi ambayo yanahusiana tu na mimba, hata hivyo, ni muhimu kukumbuka kwamba hali yoyote ambayo husababisha maumivu katika mgonjwa asiyekuwa na ujauzito inaweza pia kutokea kwa mama mjamzito, ingawaje historia na uchunguzi vinaweza kuwa tofauti. Kwa asili kutathmini maumivu ya tumbo kwa mama mjamzito ina changamoto kwa sababu kichefuchefu, kutapika, na maumivu ya tumbo hujitokeza mara nyingi kwa wajawazito wengi . Mfuko wa uzazi unapotanuka unaweza kusukuma viungo vingine kando ndani ya tumbo, upungufu wa damu na leukocytosis ni kawaida katika mimba ya kawaida na si viashiriwa vya upungufu wa damu au maradhi. Mgonjwa ambaye mimba imetunga nje ya mfuko kipimo cha ultrasound kinaonyesha majimaji na uchafu ndani ya mfuko wa uzazi bila ushahidi wa mimba. Kiinitete kinapojipandikiza katika ...