RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 19 & 20
Mtunzi:EDDAZARIA G.MSULWA ILIPOISHIA... “Sheila nakuomba unipe nafasi nijielezeee” “SITAKI NASEMA EDDY TOKA NDANI KWANGU” Sheila alizungumza huku akinisukuma kitandani na sikuwa na kipingamizi nikashuka huku machozi yakinilenga lenga na kuichukua surualia yangu na kuivaa taratibu.Nikachukua shati langu na kuliweka begani na huku begi langu nikiwa nimelishika mgongoni. “Sheila ninaondoka huu usiku na umenifukuza mimi kama mwizi…Ila ninakuombea maisha mema.Mimi ngoja nikalale pembeni mwa geti lako ili huu usiku upite nakuomba kwa hilo” Nilizungumza huku machozi yakinimwagika na nikafungua mlango na kutoka taratibu huku nikiwa siamini kiu kilicho nitokea ENDELEA.... .....Nikaendelea kupiga hatua za taratibu hadi nikafika getini na kusimama baada ya kuisikia sauti ya Sheila ikiniita “Eddy unataka kwenda wapi?” “Kwani wewe unataka kujua hivyo kama nani?” “Hapana Eddy mpenzi wangu ninakuomba unisamehe ni hasi...