Habari sanaa na michezo

Jumatatu, 9 Machi 2026

T media news

Rais wa Urusi, Vladimir Putin amesaini na kurasimisha sheria inayokataza kuwarejesha (Extradition) raia wa kigeni waliotumikia na wanaotumikia Jeshi la Urusi.

Kwa maana hii, wageni au watu wasio na uraia (stateless) hawatarejeshwa nchini mwao au nchi yoyote kwa ajili ya kufunguliwa mashtaka ya jinai kwa kushiriki vita vya Urusi na Ukraine, badala yake watasalia nchini Urusi na kupewa uraia. 

 Sheria hii inawalenga wale wanaotumikia sasa na waliowahi kutumikia huko nyum kwa mkataba katika jeshi la Urusi au katika “vikosi vingine vya kijeshi” vya Urusi.



Bunge la Urusi, State Duma, liliidhinisha sheria hiyo mnamo tarehe 26 Februari 2026 na baadaye Baraza la Shirikisho la Urusi (Federation Council of Russia) likaipitisha tarehe 4 Machi 2026. 


Kabla ya sheria hii wageni walipewa haki ya kusaini mikataba ya kujiunga na jeshi la Urusi kuanzia Novemba 2022, na baadaye Julai 2024 watu wasio na uraia rasmi nao walirubusiwa. 


Kwa mujibu wa Alexander Bastrykin, mkuu wa Kamati ya Uchunguzi katika jeshi la Urusi alisema kufikia Januari 2024 takribani wahamiaji 10,000 waliokuwa na uraia wa Urusi tayari walikuwa wameshiriki katika operesheni ya kijeshi nchini Ukraine. 

Na kuanzia hapo, wageni wengine waliotia saini mikataba ya kuhudumu katika jeshi la Urusi kabla ya kumalizika kwa operesheni ya kijeshi nchini Ukraine, pamoja na wanafamilia wao, wanaweza kupata uraia wa Urusi kupitia mchakato rahisi zaidi baada ya Rais Putin kusaini sheria hii. 


Hakutakuwa na ulazima wa kutimiza sharti la kuishi nchini Urusi kwa miaka mitano ili kupata kibali cha makazi ya kudumu.

Wale watakaoachishwa kazi jeshini na hata waombaji ambao watathibitika kuwa hawana vigezo vya kuhudumu jeshini, nao pia wanaweza kuomba uraia wa Urusi kupitia mchakato uliorahisishwa na sheria hii. 


Read More
T media news

Wakati unaendelea kuimarisha misuri ya uume na tendo la ndoa kwa ujumla nakusihi ACHANA NA KUANGALIA VIDEO ZA CHAFU


 

Usiangalie video za 'x’ zenye kuchochea kufika kileleni haraka. Ungaliaji wa movie za namna hii huchochea zaidi mbegu na kupandisha ashki na munkari wa kufanya mapenzi ambapo unapokutana na mwenza, uume kugusa tu mashavu ya uk* shahawa huwa zimeshamwagika tayari 


Hali hii inatukuta haswa vijana ambao tulizoea kujichua na kuendekeza sana kuangalia picha za ngono..


Kabla sijaondoka nikuachie mbinu nyingine wakati unaendelea na tiba kuwa.. Ile nusu saa kabla hujaenda kushiriki tendo la ndoa hakikisha umeandaa kinywaji cha tangawizi iwe kali kidogo, kunywa walau kikombe kidogo kimoja. Hii inakusaidia damu kuchangamka na kusambaa kwenye misuri na uume kudindaa vizuri pale unapohitaji kushiriki faragha... Unaweza usipate matokeo mazuri kwa siku moja ila kadri unavyojiwekea utaratibu huu kila mara utapata matokeo yaliyo mazuri zaidi.


Read More
T media news

FAIDA ZA MCHAICHAI

  


Huu Mmea ni Mmea Mkubwa sana ktk sekta ya Afya.

Watu wengi wenye hekima wamelima mashamba makubwa ya mchaichai kwa ajili ya  tiba.


 Huu Mmea kuna Magonjwa unatibu ambayo hayatibiki kirahisi kwa dawa za kisasa.. ila yanakuja kutibiwa na mmea huu , ambao ni maarufu kwa matumizi ya chai


Mmea huu una virutubisho, madini na vitamn kama ifuatavyo 


Energy (Nishati)

1Wanga (Carbohydrates )

2 Protein (protini)

3  Fat  (Mafuta)

4 Folates 

5 Niacin (Vitamn B3)

6 Pyridoxine (Vitamn B6)

7 Riboflavin (Vitamn B2)

8 Thiamin (Vitamin B1)

9 Vitamin A 6 

10Vitamin C 

11 Madini ya Sodium 6 

12 Madini ya Potassium 

13 Madini ya Calcium 

14 Una madini ya Copper  (shaba)

15 Madini ya  Iron (chuma)

16 Madini ya Magnesium 

17 Pia madini ya Manganese 

17 Madini ya Selenium 

Na madini ya Zinc


Hivyo huu fanya mmea huu kuwa na faida kubwa mnoo mwilini


Ukianza kuchambua kila kimojawapo hapo , utajikuta mwili umejaa kila hitaji linalohitajika


FAIDA ZA KUTUMIA MCHAICHI


🌹 Ina sifa ya  Antidepressant


Matumizi ya Mafuta ya mchaichai huongeza kujistahi, kujiamini, matumaini, nguvu ya kiakili,.. Hii inaweza kusaidia sana kuondoa unyogovu kutokana na kushindwa katika kazi, maisha ya kibinafsi, wasiwasi , upweke, vilio, kifo katika familia, na sababu nyingine nyingi... Mafuta ya asili ya mchaichai ukijipaka tu hata kama ulikuwa na hofu , mshituko kama wa msiba , hali hiyo ikikutokea paka haya mafuta utakaa sawa


 🌹Kupunguza Uzito


Mchaichai una citral, ambayo ni bora dhidi ya fetma.. Inapunguza mkusanyiko wa mafuta ya tumbo na kukuza utumiaji wa nishati iliyohifadhiwa, ambayo husaidia kuzuia kupata uzito unaosababishwa na ulaji mbaya wa chakula bila mpangilio ,Mtu anakula mara tano , badala ya mara moja au mbili kwa siku  ,pia  huongeza oxidation ya asidi ya mafuta katika mwili. 


Ina sifa ya kupambana na Saratani


Citral ni  kemikali iliyo ktk Mchaichai, inaweza kuwa na ufanisi katika kuzuia ukuaji wa seli za saratani bila kuathiri seli za afya za mwili. Citral n nzur  katika kuzuia ukuaji wa seli za saratani ya ini  na kuzuia ukuaji zaidi wa seli za saratani..


🌹Huondoa Matatizo ya Kupumua


Mchaichai hutumiwa sana katika dawa ya Ayurvedic ... Huondoa madhara ya vidonge vinavyohusika na  katika kutibu kikohozi na baridi yabis . Lakin pia  vitamini C iliyoko ktk mchaichai , inasaidia katika kutoa unafuu kutokana na kuziba kwa pua, mafua, na matatizo mengine ya kupumua kama vile pumu ..


Hudhibiti Kisukari

Mchaichai ni Utafiti unaonyesha ni  kwa ajili ya kutibu kisukari aina ya 2. Citral iliyopo ktk mchaichai inasaidia  kudumisha viwango bora vya insulini na kuboresha uvumilivu wa glukosi mwilini na kuifanya kuwa bora kwa watu wenye kisukali aina ya 2


Mambo Mengine ambayo yanatibiwa na huu Mmea 


🌹Inasaidia kwenye mmeng’enyo wa chakula kama vile kuvimbiwa na gesi.

🌹Kusafisha mwili na kutoa sumu

🌹Kuboresha afya ya ngozi

🌹Kupunguza mafua na kikohozi 

🌹Inapunguza maumivu na kuvimba

🌹Huongeza Kinga za mwili 

🌹Huzuia Kuvu 

🌹Inatatua tatizo la kugombana Kwa mke na Mme

🌹Ni nzuri kwa magonjwa ya tumbo

🌹Ukiuchanganya na Mmea wa Mziwaziwa unatibu UTI sugu iliyoshindikaña 

🌹Mafuta ya mchai Chai ni mazuri kwa 


Mapunye, fangasi nk. Mafuta ya mchaichai ni dawa. kuna wakati watoto wanakuja na mapunye toka shule uko, wakati mwingine minyoo tu inakuletea fangasi au ndio mambo ya kujaribisha mitumba… unatoka na ugonjwa wa ngozi hapo au utangotango….


🌹Mchaichai una kiwango kikubwa cha Catechins  ambacho husaidia mishipa ya damu kuzalisha  Nitric Oxide  (NO), ambayo husaidia kutanua mishipa ya damu ikiwepo mishipa ya damu ktk uume.


🌹Pia mchaichai husaidia uzalishaji wa antioxidants ambazo husaidia kuondoa sumu mwilini..


🌹Mwanamke ukimchanganyia mme wako Chai ya Kijiko 1 karafuu + tangawizi + Mchaichai + Mdalasini+ Iliki


Mpe Kikombe 1 Asubuhi na Jioni baada ya wiki Mbili , Njoo Utoe Ushuhuda

Read More
T media news

Usiku wa kuamkia leo Iran imeshusha mashambulizi makali kwa Israel kwa kupiga uwanja wa ndege wa kimataifa


 Usiku wa kuamkia leo Iran imeshusha mashambulizi makali kwa Israel kwa kupiga uwanja wa ndege wa kimataifa wa Ben Gurion uliopo pembeni ya mji wa Tel Aviv makombora yalionekana yakishuka kwa wingi kama mvua bila mifumo ya ulinzi wa anga wa Israel ku Intercept makombora hayo.

Ben Gurion Airport ni uwanja mkuu wa ndege wa Israel, zaidi ya Asilimia 90% ya wasafiri wa kimataifa wa Israel hupitia hapo, lakini pia ni moja kati ya Airport zenye ulinzi mkali duniani kwani uwanja huo unatumika pia kwa operation za kijeshi na usalama.

Mashambulizi na wingi wa makombora yaliyorushwa usiku wa kuamkia leo Israel umesababisha kutiliwa shaka kwa kauli ya Trump kwa kutangaza ushindi kuwa kaivunja nguvu Iran kwa kuharibu Missile Launchers (mifumo ya kurusha makombora)  ya Iran.


Maana ndani ya masaa 24 tangu atoe kauli hiyo Iran wameshambulia maeneo mengi ya mshariki ya kati yenye uhusiano na Marekani, ndani ya masaa 24 Iran wameshambulia Base za marekani kwa kupiga Al-Udair base na Command bulding zilizopo kuwait , baada ya hapo wakapiga US naval infrastructure (miundombinu ya jeshi la wanamaji wa marekani) huko Bahrain, lakini pia wakapiga oil facilities ikiwepo Bapco ,Oild depots ya Kuwait na Oil refinery ya Haifa huko Israel.

Na baada ya hapo ndipo usiku wa kuamkia leo Iran wakatangaza Supreme Leader mpya ambae ni Ayatollah Mujtaba Khamenei na wakamkaribisha  kwa kuishambulia Israel kwa makombora mengi maeneo mbalimbali ikiwepo uwanja huu wa Ben Gurion.

 

Je kwa idadi ile ya makombora waliyorusha jana Iran ni kweli Trump aliharibu mifumo ya kurusha makombora (Missile Launchers) za Iran au hana taarifa za uhakika kuhusu nguvu ya Iran?

Read More
T media news

Israel Yaiomba Dunia Msaada Kufuatia Vitisho vya Makombora,

 

Katika kipindi hiki cha mvutano unaoendelea katika eneo la Mashariki ya Kati, maafisa wa Israel wamezitaka nchi mbalimbali duniani pamoja na United Nations (UN) kuchukua hatua kuhusu mashambulizi ya makombora yanayolenga taifa hilo.


Kwa mujibu wa taarifa za awali, viongozi wa Israel wanasema mashambulizi hayo yanaongeza hatari ya usalama katika eneo hilo na wanasisitiza umuhimu wa jumuiya ya kimataifa kuingilia kati ili kuzuia kuongezeka kwa mzozo.

Maelezo zaidi kuhusu tukio hilo bado yanaendelea kutolewa huku hali ikiendelea kufuatiliwa kwa karibu.


Read More
T media news

LABDA SASA TUNAWEZA KUSIMAMISHA USAMBAZAJI WA GESI KWA ULAYA PUTIN KATIKA VITA VYA IRAN



Rais wa Urusi Vladimir Putin amedokeza kwamba Urusi inaweza kuacha kusambaza gesi barani Ulaya, akisema inaweza kuwa na faida zaidi kuelekeza mauzo ya nje kwenye masoko mengine

Maoni hayo yanakuja huku bei za nishati zikipanda huku migogoro ikizidi kuongezeka Mashariki ya Kati


Huku kukiwa na mvutano karibu na Iran na usumbufu karibu na Mlango-Bahari wa Hormuz, njia muhimu inayobeba takriban 20-30% ya mafuta duniani, hofu ya usambazaji wa kimataifa imeongeza bei ya gesi barani Ulaya juu zaidi. Urusi hapo awali iliwahi kutoa takriban 40% ya gesi ya bomba la Ulaya, lakini sehemu hiyo tayari imeshuka sana baada ya vikwazo na Ukraine kuiwekea vikwazo.

Sasa, Moscow inaashiria kwamba ikiwa wanunuzi wanaolipa vizuri watatokea kwingineko, inaweza kuhamisha mauzo yake ya nishati kutoka Ulaya kabisa. Ikiwa hilo litatokea, soko la nishati duniani linaweza kukabiliwa na mshtuko mwingine mkubwa.

Read More
T media news

WAKURDI WA IRAQ WAKATAA KUSHIRIKI MASHAMBULIZI YA MAREKANI DHIDI YA IRAN


 

Viongozi wa Wakurdi nchini Iraq wamesema wazi kuwa hawatakuwa sehemu ya mpango wowote wa kijeshi wa Marekani dhidi ya Iran. Wamesisitiza kuwa watabaki upande wa kati katika mvutano unaoendelea katika eneo la Mashariki ya Kati.


Kwa mujibu wa kauli zao, Wakurdi wanasema bado wana shaka kubwa juu ya nia ya Washington, wakijiuliza kama Marekani inalenga kubadilisha utawala wa Iran au kufanya mabadiliko ya ndani tu.


Pia wameonya kuwa hawataki kutumika kama “ncha ya mkuki” katika vita vya wengine, wakikumbusha historia ya matukio ambapo Wakurdi walidai kutumiwa kisiasa na baadaye kuachwa bila msaada.


Wakurdi wameeleza kuwa bila uvamizi wa ardhini wa Marekani, madai ya mabadiliko ya utawala nchini Iran yanaonekana kuwa magumu kutekelezeka. Hivyo, wamechagua kusalia nje ya mpango wowote wa mashambulizi dhidi ya Tehran.

Read More