Kurasa

T Media News

habari michezo na burudani

Jumatano, 11 Machi 2026

T media news

Agosti 1978, hali ya Kenyatta ilikuwa mbaya

 


Agosti 1978, hali ya Kenyatta ilikuwa mbaya zaidi. Kumbukumbu yake iliharibika, hotuba yake iliyumba, na mwendo wake wa kutisha uliyumba. Alipoondoka Nakuru kwenda Mombasa mnamo Agosti 2, 1978, waliomzunguka walihisi kama ndiyo mwisho wa maisha yake. Siku iliyofuata hakutoka nje ya viwanja vya Ikulu; maneno yake yalibadilika, na hata kutembea na kukaa alitumia muda wa kutosha ili kuwasumbua hata wafuasi wake.

.

Siku ya Ijumaa, Agosti 4, Mzee alifungua Maonyesho ya Jumuiya ya Kilimo ya Mombasa Kenya na kubadilisha safu ya mwisho ya “asante” na kusema “Amina” asiyokusudiwa. Ilikuwa hotuba rasmi ya mwisho ya maisha yake ya baraka.


Siku kumi baadaye, mnamo Agosti 14, alikusanya familia yake katika Ikulu ya Mombasa. Kwa hakika, ilikuwa ni alama ya kuachiliwa kwake 1961 kutoka kizuizini. Lakini minong'ono ilisafiri haraka kuliko itifaki kila mtu alihisi kuagwa. Na kwa kweli, mzee alikuwa akifanya raundi zake za mwisho.


Kupanda ngazi na kurudi kwenye vyumba vyake ilikuwa shida, miguno na ukimya vkawa ndiyo vitu vyake. Yeyote aliye na huruma angeghairi hata kumuona kwenye burudani za Msambweni zilizopangwa kufanyika siku inayofuata. Lakini wale walio karibu naye kama, PC Mahihu anayekuwa mwanamahesabu wake na Mdhibiti mwaminifu pamoja na Gitau walijituma wakishikilia ratiba kwa kutumia akili.

.

Msafara uliendelea hadi Shule ya Msingi ya Msambweni, ambako wacheza densi na kwaya za shule walikuwa wamekusanyika kwa ajili ya onyesho la mwisho. Wakati huo, Mzee alikuwa amejishikilia kwa shida sana.

.

Baada ya kuhudhulia Nusu ya maonyesho, alikwenda bafuni kwa muda nyuma ya jukwaa. Dakika zilipita sana. Mbiyu na Mahihu waliingia kwa kasi na kumkuta akiwa amejilaza kwenye kiti chooni akiwa hana uhai ameshakufa. Walimnyanyua kwa ustadi, wakapanga upya mavazi yake, na kumrudisha kwenye jukwaa nyuma ya korido na ulinzi ukawa ni wakati wa kupunguza watu  ili kufichwa ju ya tukio la kifo cha kenyata.


Walifanya hivyo Ili kudumisha dhana kwamba kila kitu kiko sawa, Mahihu alimtaka Mzee amalize sherehe hiyo kwa kutia saini wito wake.. “Harambee”. Ilikuwa ni jambo gumu sana. Haikuwa ya lazima. Lakini Kenyatta alitimiza jambo hilo, huku akipiga kishindo zaidi kuliko kitu chochote amb

Read More
T media news

Siri ya Iran Iko Chini ya Milima



​Kwa miongo kadhaa, wakati ulimwengu ukitazama nguvu ya ndege za kivita angani, Iran imekuwa ikijenga mtandao mkubwa na wa kisasa wa kijeshi uliopenya ndani ya ardhi na kuta za milima, maarufu kama "Missile Cities." 

Vituo hivi vya siri vimechimbwa umbali wa mita 30 hadi 80 kwenda chini na kusambaa kwa makumi ya kilomita, vikiwa vimeundwa kuhimili mashambulizi makali ya mabomu mazito ya anga (bunker-busters). 

Ndani ya mahandaki hayo yaliyoimarishwa kwa zege na chuma, kuna maelfu ya makombora ya masafa marefu kama Ghadr na Emad yanayoweza kupiga malengo hadi umbali wa kilomita 2,000, pamoja na mamia ya ndege zisizo na rubani (drones) za Shahed na Arash, zote zikiwa tayari kurushwa wakati wowote kupitia mifumo ya siri ya kurushia iliyounganishwa na barabara za chini kwa chini.

​Mkakati huu wa Iran wa "asymmetric warfare" haujaishia kwenye makombora pekee, bali umehama hadi angani na baharini kupitia vituo kama Oghab 44, ambapo ndege za kivita kama F-14 Tomcat hufanyiwa matengenezo na kurushwa kutokea ndani ya milima karibu na Mlango-Bahari wa Hormuz.

Baharini, Iran hutumia mbinu ya "mosquito fleet" yenye boti ndogo za kasi zinazoweza kushambulia meli kubwa na kujificha kwenye kuta za pwani. 

Wakati mifumo ya ulinzi ya mataifa ya Magharibi ikitumia mamilioni ya dola kuzuia droni za gharama nafuu, Iran imeendelea kuimarisha ghala lake la makombora yanayokadiriwa kufikia 80,000, huku ikiweka vituo feki (decoys) ili kupoteza ramani za satelaiti za adui. 

Mfumo huu mzima unadhihirisha mpango wa muda mrefu wa Iran wa kuhakikisha uwezo wake wa kulipiza kisasi unabaki salama hata kama nchi hiyo itashambuliwa kwa kiwango kikubwa kiasi gani.



 

Read More
T media news

Charles Burton amebakiwa na siku moja tu ya kuishi.


 Hadi sasa Charles Burton amebakiwa na siku moja tu ya kuishi. Ingawa ametumia zaidi ya miongo mitatu kwenye gereza la hukumu ya kifo (death row).


Burton, anayejulikana kama “Sonny” kwa familia na marafiki zake, amepangwa kunyongwa siku ya Alhamisi.


Taarifa kutoka CNN inasema Mzee huyo mwenye umri wa miaka 75, ambaye sasa anatumia kiti cha magurudumu, yuko kwenye hukumu ya kifo kwa kosa la mauaji ya Douglas Battle, licha ya ukweli kwamba yeye mwenyewe hakufanya tukio la kumpiga risasi lililosababisha kifo hicho.


“Sikumua mtu yeyote, hilo ni kweli, lakini nilifanya kosa kwa kuwa sehemu ya uhalifu huo,” Burton aliiambia CNN katika mahojiano.


 “Nilifanya kosa, na inaonekana marafiki zangu wengi wamenisamehe. Natumaini hata nikinyongwa Alhamisi marafiki zangu watakumbuka kuwa nilikuwa rafiki wa kweli, rafiki mzuri.”

Alisema Burton.


Sasa hali ilikuwaje hadi kuhukumiwa kifo Ilihali anakiri kuto kuhusika katika mauaji?


Twende tuitazame hadithi yenyewe .


Mnamo Agosti 1991, Burton pamoja na Derrick DeBruce waliiba katika duka la AutoZone mjini Talladega. 

Wakati walipovamia duka kwa lengo la kuiba, wateja kadhaa walikuwa wakipata huduma katika duka hilo. Na ndipo Derrick ambaye alikuwa rafiki wa Burton alimfyatulia risasi na kumuua mteja mmoja katika Duka Hilo.


Wote walifikishwa mahakamani na kusomewa hukumu ya kifo ambapo hakukuwekwa tarehe Kamili ya wao kuuwawa.

Ingawa Burton hakuwa mtu aliyepiga risasi na hata hakuwa ndani ya duka wakati mauaji yalipotokea, alihukumiwa kwa kosa la mauaji ya jinai ya kiwango cha juu (capital felony murder) na kuhukumiwa kifo na jopo la majaji mwaka 1992.


Tangu hapo walikaa katika gereza la kesi la mauaji wakisubiri tarehe kamili ya kutekelezwa kwa hukumu hiyo. Hata hivyo Mwaka 2014 rafiki yake DerrickDebruce alifariki Kwa ugonjwa akiwa gerezani. 


Tangu hapo Burton alibaki gerezani kusubiri hukumu juu ya mauaji ambayo si yeye alihusika kupiga risasi hukumu ambayo inatarajia kutekelezwa Alhamisi hii.


Maoni yako ni yapi katika hili? Je adhabu hii inapaswa kutekelezwa ama Selikali inapaswa Kutazama Kwa jicho jingine juu ya hukumu hii?.

Read More
T media news

Jeshi la Israel linatarajiwa kuongeza mashambulizi yake dhidi ya Iran


 Jeshi la Israel linatarajiwa kuongeza mashambulizi yake dhidi ya Iran huku kukiwa na wasiwasi kwamba Rais wa Marekani, Donald Trump, anaweza kuhitimisha vita hivyo ghafla kupitia makubaliano ya kisiasa.


Kwa mujibu wa ripoti ya kituo cha televisheni cha Israel, Channel 12, viongozi wa kijeshi wa Israel wanaamini kuwa kuna uwezekano wa Washington kusukuma suluhisho la haraka la kidiplomasia, hali inayoweza kusimamisha operesheni za kijeshi mapema kuliko ilivyotarajiwa.


Kutokana na hali hiyo, jeshi la Israel linaripotiwa kuharakisha na kuongeza kasi ya mashambulizi dhidi ya malengo ya Iran, likitaka kufikia malengo yake ya kijeshi kabla ya uamuzi wowote wa kisiasa kuchukuliwa.


Ripoti hiyo pia inaeleza kuwa Israel inajiandaa kwa uwezekano wa mshangao, ambapo Marekani inaweza kutangaza kusitisha vita bila onyo la muda mrefu, jambo ambalo linaweza kubadilisha mwenendo wa operesheni za kijeshi katika mgogoro huo.


Mapigano kati ya Israel na Iran yameongezeka tangu mashambulizi ya pamoja ya Marekani na Israel dhidi ya Iran mapema mwaka 2026, ambayo yalisababisha mashambulizi ya kulipiza kisasi ya makombora na ndege zisizo na rubani kutoka Iran.

Read More
T media news

UAE Yafadhili Ndege Kuwahamisha Mamia ya Raia wa Israel Baada ya Ombi la Netanyahu


Gazeti la Israel Haaretz limeripoti kuwa serikali ya United Arab Emirates imefadhili ndege kwa gharama zake ili kuwahamisha takribani Waisraeli 700 waliokuwa wamekwama katika maeneo mbalimbali kutokana na hali ya vita inayoendelea katika eneo la Mashariki ya Kati.


Hatua hiyo inadaiwa kufanyika baada ya ombi lililotolewa na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kwa Rais wa UAE Mohamed bin Zayed Al Nahyan ili kusaidia kutafuta suluhisho kwa maelfu ya raia wa Israel waliokuwa wamekwama nje ya nchi yao.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, ndege hizo maalum zilipangwa kuwachukua Waisraeli kutoka Ben Gurion Airport pamoja na mji wa Athens, ambako baadhi ya raia wa Israel walikuwa wamekwama baada ya safari nyingi za ndege kusimamishwa au kuvurugika kutokana na hali ya usalama inayozidi kuwa tete.

Ripoti hiyo inaeleza kuwa serikali ya UAE iliamua kugharamia operesheni hiyo ya usafiri kama sehemu ya juhudi za kibinadamu na ushirikiano wa kidiplomasia kati ya mataifa hayo mawili.

Tangu kusainiwa kwa makubaliano ya kidiplomasia kati ya Israel na UAE miaka michache iliyopita, uhusiano wa kisiasa na kiuchumi kati ya nchi hizo umeongezeka kwa kasi, jambo ambalo limewezesha ushirikiano katika nyanja mbalimbali ikiwemo usalama, biashara na usafiri wa anga.

Kwa mujibu wa makadirio yaliyotolewa katika ripoti hiyo, inaaminika kuwa takribani Waisraeli 14,000 walikuwa ndani ya UAE mwanzoni mwa vita vilivyozuka katika eneo hilo. Idadi hiyo kubwa ya watu ilizua changamoto za kiusalama na usafiri wakati hali ya mzozo ilipoanza kuathiri safari za anga katika baadhi ya maeneo ya Mashariki ya Kati.

Maafisa wa serikali pamoja na mashirika ya usafiri wa anga wamekuwa wakifanya juhudi mbalimbali kuhakikisha kuwa raia waliokwama wanaweza kurejea nyumbani kwa usalama.

Hatua ya UAE ya kugharamia ndege maalum imeonekana na wachambuzi wa siasa za kimataifa kama ishara ya uhusiano wa karibu unaoendelea kujengwa kati ya Abu Dhabi na Tel Aviv katika miaka ya hivi karibuni.

Ingawa operesheni hiyo imehusisha takribani watu 700 pekee kwa awamu ya kwanza, ripoti zinaeleza kuwa juhudi zaidi zinaweza kuendelea kufanywa ikiwa kutakuwa na raia wengine wanaohitaji msaada wa kusafirishwa kutoka maeneo yaliyoathiriwa na hali ya vita.

Wataalamu wa masuala ya usalama wanasema kuwa migogoro mikubwa ya kijeshi mara nyingi husababisha changamoto kwa raia walioko nje ya nchi zao, hivyo operesheni za kuwahamisha watu huwa sehemu muhimu ya majibu ya dharura ya serikali.

Hadi sasa mamlaka za UAE na Israel zinaendelea kuratibu hatua zaidi za kuhakikisha usalama wa raia wao pamoja na kudhibiti athari za mgogoro unaoendelea katika eneo la Mashariki ya Kati.

Vyanzo vya kidiplomasia vinaeleza kuwa ushirikiano wa aina hii unaweza kuendelea kadri hali ya usalama inavyoendelea kubadilika katika siku zijazo.
Read More

Jumanne, 10 Machi 2026

T media news

HUKUMU YA MTU ASIE SWALI NA ANAE FUNGA LAKINI HASWALI


 

🔸سئل العلامة العثيمين رحمه الله تعالى - كما في مجموع الفتاوى ( ج ١٢ / ١٠١ - ١٠٣ )

ﻋﻦ ﺭﺟﻞ ﻻ ﻳﺼﻠﻲ الصلاﺓ ﺇطلاﻗﺎ ﻣﻊ ﺇﻗﺮاﺭﻩ ﺑﻮﺟﻮﺑﻬﺎ ﻭﻳﺼﻮﻡ ﺭﻣﻀﺎﻥ ﻟﻜﻨﻪ ﻻ ﻳﺼﻠﻲ ﻫﻞ ﻳﺤﻜﻢ ﺑﺈسلاﻣﻪ؟

Aliulizwa Mwanachuoni Uthaymiin Allah amrehemu, kama katika kitabu "Majumu'ul fataawa" (juzuu ya: 12 / 101 - 103)

Kuhusiana na mtu ambae haswali kabisa, ingawa anakiri uwajibu wa swala, na anafunga Ramadhani, lakini haswali. Je, anahukumiwa kuwa ni Muislamu?


🔹ﻓﺄﺟﺎﺏ ﺑﻘﻮﻟﻪ: 

"اﻟﺼﻼﺓ ﺃﻣﺮﻫﺎ ﻋﻈﻴﻢ ﻭﺷﺄﻧﻬﺎ ﻛﺒﻴﺮ، ﻭﻫﻲ ﺁﻛﺪ ﺃﺭﻛﺎﻥ اﻹسلاﻣ ﺑﻌﺪ اﻟﺸﻬﺎﺩﺗﻴﻦ ﺑﺈﺟﻤﺎﻉ ﺃﻫﻞ اﻟﻌﻠﻢ، ﻭﻭﺭﺩ اﻟﻮﻋﻴﺪ اﻟﺸﺪﻳﺪ ﻓﻲ ﺇﺿﺎﻋﺘﻬﺎ ﻓﻲ اﻟﻜﺘﺎﺏ ﻭاﻟﺴﻨﺔ، ﻭﻻ ﺃﻇﻦ ﺃﻥ ﺃﺣﺪا ﻳﺆﻣﻦ ﺑﻔﺮﺿﻴﺘﻬﺎ ﻭﺗﺄﻛﺪﻫﺎ ﻭاﻟﻮﻋﻴﺪ ﻋﻠﻰ ﺇﺿﺎﻋﺘﻬﺎ ﺛﻢ ﻳﺘﺮﻛﻬﺎ ﻣﻊ ﺃﻧﻬﺎ ﻋﻤﻞ ﻳﺴﻴﺮ ﺳﻬﻞ ﻣﻮﺯﻉ ﻓﻲ اﻟﻴﻮﻡ ﻭاﻟﻠﻴﻠﺔ ﻭﻻ ﻳﺘﺮﻛﻬﺎ ﺇﻻ ﺃﺣﺪ ﺭﺟﻠﻴﻦ: ﺇﻣﺎ ﺷﺎﻙ ﻓﻲ ﻓﺮﺿﻴﺘﻬﺎ، ﺃﻭ ﻣﻌﺎﻧﺪ ﺃﻋﻈﻢ ﻋﻨﺎﺩ ﻟﻠﻪ ﻭﺭﺳﻮﻟﻪ.

Akajibu kwa kusema:

Swala nafasi yake ni kubwa na jambo lake ni kubwa, na ndio nguzo ya muhimu zaidi ya Uislamu baada ya shahada mbili kwa makubaliano ya wanazuoni wote, na yamekuja makemeo makali juu ya kuipoteza, katika Qur-an na Sunnah, na sidhani kama kuna yeyote anaeamini ufaradhi wake, na mahimizo yake na makemeo yake juu ya kuipoteza, kisha anaiacha pamoja nakuwa ni amali ndogo nyepesi aliyogawanywa katika usiku na mchana, na hakuna anaeiacha ispokuwa ni mmoja kati ya watu wawili: Ima ni mtu mwenye shaka juu ya ufaradhi wake, au ni mpingaji upingaji mkubwa wa Allah na Mtume wake ﷺ.


🔸ﻭﻣﻦ ﺯﻋﻢ ﺃﻧﻪ ﻣﻘﺮ ﺑﻮﺟﻮﺑﻬﺎ، ﺃﻭ ﻗﺎﻝ ﺇﻧﻪ ﻣﻘﺮ ﺑﻮﺟﻮﺑﻬﺎ ﻭﻟﻜﻨﻪ ﻟﻢ ﻳﺼﻞ ﻓﻬﻮ ﻛﺎﻓﺮ ﻭﺇﻥ ﻛﺎﻥ ﻳﺼﻮﻡ ﻭﻳﺤﺞ ﻭﻳﺰﻛﻲ

Na atakaedai kuwa anakiri uwajibu wake, au akasema kuwa anakiri uwajibu wake, lakini haswali, basi huyo ni kafiri, hata kama atakuwa anafunga, anahiji, na anatoa zaka.


❶ ﻟﻘﻮﻝ اﻟﻨﺒﻲ ﺻﻠﻰ اﻟﻠﻪ ﻋﻠﻴﻪ ﻭﺳﻠﻢ: "ﺑﻴﻦ اﻟﺮﺟﻞ ﻭﺑﻴﻦ اﻟﺸﺮﻙ ﻭاﻟﻜﻔﺮ ﺗﺮﻙ اﻟﺼﻼﺓ"

ﺭﻭاﻩ ﻣﺴﻠﻢ.

Kwa mujibu wa kauli ya Mtume ﷺ: 

[Kitenganishi baina ya mtu na shirki na ukafiri ni kuacha Swalah]

Ameipokea Muslim.


❷ ﻭﻗﺎﻝ: "اﻟﻌﻬﺪ اﻟﺬﻱ ﺑﻴﻨﻨﺎ ﻭﺑﻴﻨﻬﻢ اﻟﺼﻼﺓ ﻓﻤﻦ ﺗﺮﻛﻬﺎ ﻓﻘﺪ ﻛﻔﺮ"

ﺭﻭاﻩ اﻟﺨﻤﺴﺔ.

#Tutekeleze_Swala_nduguzangu.✅️

Read More
T media news

Jozi ya viatu vya sandali vilivyohusishwa kijadi na Mtume Muhammad ﷺ,


  vinavyojulikana kama Na’l-i Şerif (Nalain Shareef), vimehifadhiwa kwa heshima katika Chumba cha Mabaki Matakatifu cha Jumba la Makumbusho la Jumba la Topkapi huko Istanbul, Türkiye.


Mabaki haya ya heshima yalihifadhiwa na Milki ya Ottoman katika karne ya 16 kufuatia ushindi wa Ottoman dhidi ya Misri. Pamoja na vitu vingine vitakatifu vinavyohusishwa na Mtume ﷺ — ikiwa ni pamoja na joho lake lililobarikiwa na upanga — vinasalia kuwa miongoni mwa vitu vya kale vinavyoheshimika zaidi katika historia ya Kiislamu.


Kwa Waislamu kote ulimwenguni, mabaki kama hayo hutumika kama ukumbusho wenye nguvu wa maisha, urithi, na upendo wa kudumu kwa Mtume mpendwa ﷺ, na kuimarisha uhusiano wa kina wa kiroho ambao wengi wanahisi na imani na urithi wao. SubhanAllah 🤍


Kanusho: Chapisho hili limeshirikiwa kwa madhumuni ya ufahamu, elimu, taarifa, na uandishi wa habari pekee.

Read More

Kurasa