Mapigano ya kugombea ardhi kati ya Wasonjo na Wamasai yaibuka na kusababisha vifo vya watu 3 Ngorongoro
Mapigano kati ya makabila ya Masai na Wasonjo yameibuka tena katika vijiji vya naan na Kisangiro wilaya ya Ngorongoro na kusababisha vifo vya watu watatu na mmoja kujeruhiwa huku sababu ikidaiwa ni kugombea ardhi kati makabila hayo ya jamii za wakulima na wafugaji. Tarafa za Loliondo na Sare kutaka kupata undani wa tukio ilo na kuzungumza na wawakilishi wa wananchi wakiwemo madiwani kutoka tarafa za Loliondo na Sare baada ya uongozi wa wilaya kuwazuia waandishi wa habari wasifike katika eneo la tukio ambapo wamesema hali ni mbaya kwanikatika matukio hayo kumeoneka matumizi ya silaha za moto na wananchi bado wana hasira na wanaviziana huku kila upande ukitoa maoni tofauti ya kumaliza mgogoro huo. Mwenyekiti wa halmshauri ya Ngorongoro Mathew Siloma amesema mauaji hayo yameleta changamoto kubwa katika halmashauri na haoni sababu ya kuificha huku akidai hakuna ufumbuzi zaidi ya kupima vijiji na kuweka mipaka na kumbwomba waziri wa ardhi aingilie kati. Kwa upande wake mkuu wa wilaya Ng...