ILI UCHEZE SIMBA INATEGEMEA NANI KAKUSAJILI-MGEVEKE
Beki wa kati wa Mwadui FC ya Shinyanga Joram Mgeveke anasema kupata nafasi ya kucheza kwenye klabu ya Simba inategemea na nani amekusajili kwenye timu. Mgeveke ambaye anamalizia muda wake wa mkopo akiwa na Mwadui anasema, mkataba wake na Simba unamalizika baada ya kumalizika kwa msimu huu. “Unajua saizi mimi nipo huru sina mkataba na Simba saizi so hata nikirudi kule tunaanza mkataba mpya”, anasema beki huyo ambaye amekuwa nguzo ya kutumainiwa kwenye kikosi cha Julio katika msimu huu. “Mkuu saizi mimi nimemaliza mkataba na Simba yaani nipo huru kwenda timu yoyote hata kama watataka nirejee kule tutakuwa na maongezi mapya”. Mgeveke anaendelea kusema kwamba, kucheza na kutokucheza ndani ya klabu ya Simba kunategemea na uongozi wa juu kwasababu wao ndiyo wanafanya usajili, na ili upate nafasi ya kucheza inategemea na kiongozi aliyekusajili ananguvu kiasi gani. “Dah!!! Unajua timu zile zinakuwa na makundi mengi mkuu kuanzia kwenye uongozi so chanzo kinaa...