Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Hawara wa Mfanyakazi wa ndani Atiwa Mbaroni Akihusishwa na Mauaji ya Aneth Msuya ( Dada wa Bilionea Msuya )

Hawara wa Mfanyakazi wa ndani Atiwa Mbaroni Akihusishwa na Mauaji ya Aneth Msuya ( Dada wa Bilionea Msuya )

Picha
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limewakamata watu wengine wawili, akiwamo mpenzi wa mfanyakazi wa ndani wa Aneth Msuya, aliyeuawa kwa kuchinjwa nyumbani kwake. Aneth, ambaye ni dada wa Bilionea Erasto Msuya, aliuawa kwa kuchinjwa na watu wasiojulikana Mei 26 nyumbani kwake Kibada, Kigamboni jijini Dar es Salaam. Wauaji hao hawakuchukua chochote kwenye nyumba hiyo. Bilionea Msuya aliuawa Agosti mwaka jana kwa kupigwa risasi na tayari watu 12 wamekatwa, wakituhumiwa kuhusika na mauaji hayo. Kamanda wa Kanda hiyo, Simon Sirro alisema hadi sasa wamekamata watuhumiwa wanne wakihusishwa na mauaji ya dada wa bilionea huyo. Kati ya watuhumiwa waliokamatwa, yumo mume wa Aneth, msaidizi wa ndani wa Aneth na mtuhumiwa mwingine ambaye Kamanda Sirro hakumtaja jina. “Mwanzo tulimkamata mume wa marehemu na msaidizi wa ndani wa marehemu, lakini sasa wameongezeka wengine wawili, akiwamo hawara wa msaidizi wa ndani. Tunaendelea kuwahoji na upelelezi ukikamilika tutawafikisha m...