Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya TOP 15 YA WAFUNGAJI BORA WA MUDA WOTE WA MICHUANO YA EURO

TOP 15 YA WAFUNGAJI BORA WA MUDA WOTE WA MICHUANO YA EURO

Picha
Michuano ya 15 ya Euro inaanza leo nchini Ufaransa huku kwa mara ya kwanza timu 24 zikitaraji kuchuana vikali kuwania taji hilo. Ufaransa, Uhispania, Ujerumani, Ubelgiji na England ndizo timu zinazopewa nafasi kubwa na kubeba ndoo hiyo mwaka huu. Leo kutakuwa na mchezo mmoja tu wa ufunguzi ambapo wenyeji Ufaransa watakuwa wakipambana na Romania, mchezo wa kundi A utakaopigwa kunako dimba la Stade de France saa nne usiku (kwa saa za Afrika Mashariki). Timu nyingine katika kundi hilo ni Albania na Uswizi. Tangu kuanzishwa kwa michuano hiyo mwaka 1927, wachezaji mbalimbali waliowahi kuwa na majina makubwa kutoka nchi mbalimbali wameacha alama zao katika historia ya michuano hiyo. Lakini hapa tunawaangazia wachezaji 15 tu wenye magoli mengi zaidi katika michuano hiyo. 15.  ZINEDINE ZIDANE Huyu ni mfaransa ambaye alicheza kwa mafanikio makubwa katika ngazi ya klabu na timu ya taifa. Zidane amecheza Euro katika miaka ya 1996, 2000 na 2004. Alifanikiwa kucheza michezo 14 na k...