Kakonko. Kijana mwenye umri wa miaka 30, amefanya tukio la kushangaza kwa kujipasua tumbo kwa wembe na kuukatakata vipande utumbo wake. Tukio hilo lilitokea Februari 28, katika Wilaya ya Kakonko, Kigoma. Mkazi huyo wa Kijiji cha Kinonko, Furaha John alifikia uamuzi huo baada ya jaribio la kujinyonga kwa kutumia kamba kushindikana. John ambaye anaelezwa kuwa ni mfanyabiashara wa pombe za kienyeji, aliamua kujiua kutokana na hasira za kudhulumiwa Sh35,000 na pia kunyimwa chakula na mkewe. Akisimulia mkasa huo, John ambaye amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kibondo, alisema alirejea nyumbani akiwa na hasira za ‘kurushwa’ fedha zake na mfanyabiashara mwenzake. Alisema nyumbani nako alikutana na tukio la kunyimwa chakula na mkewe, jambo lililomuongezea hasira na kuona bora afe. “Yaani nilitoka kazini nimekasirika baada ya mwenzangu kunidhulumu fedha zote za mauzo ya siku hiyo, nafika nyumbani mke wangu naye akaninyima chakula. Nikaona ni bora kufa kwa sababu sina haja ya...