Ndoto za ubingwa bye bye kama Arsenal wasipofanya hivi


Arsene Wenger mwenyewe amekubali kwamba wakali wake wamepata ukame wa kucheka na nyavu kwa muda kidogo. “Kuna vitu vingi sana navichambua na tunatakiwa kutafuta jibu la haraka.
Hili swala lipo kichwani mwangu na ninakubali kwamba kuna ukame mkubwa wa ufungaji kwa washambuliaji wetu”, alisema Wenger.
Fikiria kuanzia kwa Sanchez amecheza mechi 10 hajafunga hata mara moja, Giroud amecheza mechi 6 hajafunga hata mara moja, Walcott amecheza mechi 10 kafunga mara moja tu. Hawa ni baadhi ya wachezaji muhimu ambao wanategemewa kuwa wanatupia nyavuni mara nyingi kusaidia club. Ukame huu wa wafungaji una athari kubwa kwenye harakati za kutafuta ubingwa.
Arsenal ipo kwenye nafasi nzuri ya kushinda ubingwa msimu huu ambapo hivi sasa wapo nafasi ya 3 wakiwa na points 51. Leo watacheza mechi ya ya 28 dhidi ya Swansea City. Kila timu inataka ushindi na huu utakua ni ushindi muhimu sana kwa Arsenal.
Baada ya Welbeck kurudi vizuri ameogeza tumaini la Arsenal kuendelea kwenye harakati za kuutafuta ubingwa.Mechi ya Arsenal VS Swansea itakua live mida ya saa 5:45.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

CHOMBEZO: UTAMU WA MADAM JESCA

Simulizi; MTOTO WA BOSS WANGU

SIMULIZI FUPI: UCHI WANGU UMENIPONZA