Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya MADIMBA-MTWARA

MH. MAJALIWA ATEMBELEA KIWANDA CHA KUCHAKATA GESI, MADIMBA-MTWARA

Picha
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa (MB) mwishoni mwa juma alifanya ziara katika mitambo ya kuchakata gesi asilia iliyopo Madimba, Mtwara. Katika ziara hiyo, Mh. Majaliwa aliweza kujionea uwekezaji wa kimataifa uliofanywa na Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanznaia (TPDC). Akiongea wakati wa ziara hiyo, Mh. Majaliwa alisema “nawapongeza sana kwa kazi nzuri mnayoifanya, ni jambo la fahari kuona Watanzania wakiendesha mitambo hii tena kwa umakini mkubwa”. Akiwa kiwandani hapo, Mh. Majaliwa aliweza kuzungumza na watumishi wa TPDC na kuwataka kuendelea kuchapa kazi kwa kutumia utaalam wao na kutambua kwamba Taifa linawategemea katika utendaji wao. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC, Dkt. James Mataragio alieleza juhudi za TPDC kuuelimisha umma kuhusu sekta ndogo ya gesi na mafuta ili kuwaandaa wananchi na fursa zilizopo na zinazokuja na miradi mikubwa ya gesi.  Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano w...