SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Jumamosi, 5 Machi 2016

T media news

Wenger amempa lawama huyu kwa kutoka suluhu na Spurs


 Kocha Wenger amempa lawama mchezaji wake Francis Conquelin kwa kupata kadi nyekundu ambapo anasema alii-cost club yake. Kabla ya kadi nyekundu hiyo Arsenal walikua wanatawala mchezo na kuongoza kwa goli moja bila.

Arsene Wenger anasema kwamba wakati wa mapumziko walimpa onyo mchezaji huyo kwa uchezaji wake ikiwa tayari ana kadi ya njano. Kipindi cha pili alicheza rafu nyingine na kupewa kadi ya nyekundu. Wenger anasema amekua dissapointed na kadi aliyopewa mchezaji wake ambapo imepunguza nguvu ya team nzima.

Sio Wenger peke yake lakini hadi mashabiki kwenye mitandao wameonyeshwa kuchukuia kwa kadi nyekundu ile ambayo amepewa mchezaji huyo.

Baada ya kadi hiyo dakika ya 55, Spurs waliongoza mchezo huo na kufunga magoli mawili ndani ya dakika 2 kabla ya Sanchez kuja kusawazisha dakika ya 76. Hadi sasa Arsenal wana points 52 na mechi 29 wakati Leicester City wapo nafasi ya kwanza wanaongoza kwa points 57 na michezo 28.