SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Jumapili, 6 Machi 2016

T media news

SHUHUDIA HAPA ATHARI ZA KUJIBADILISHA MUONEKANO KWA MADAWA


Rajee Narinesingh ambaye ni mwathiriwa wa upasuaji huo
Mwanamke mwenye jinsia yenye utata ambaye uso wake umeharibiwa baada ya kuchomwa sindano zenye simenti na malighafi za tairi alitoka nje Jumapili kuonyesha muonekana wake mpya.
Rajee Narinesingh alikuwa mmoja wa waathiriwa wa “sumu” ya daktari Onela Ron Morris, ambaye
alimfanyia upasuaji kinyume cha sheria kwa kutumua vitu kama fix-a-flat, gundi na mafuta ya madini.
Mama huyo alimruhusu Morris amchome sindano kwenye mashavu yake, midomo, kidevu, mapaja na kwenye makalio yake mwaka 2005, na kuishia kuwa na umbo la ajabu baada ya kukosa fedha za kwenda kwa mpasuaji mzuri wa urembo.
Rajee alisema alifanya upasuaji huo ili awe mwanamke mrembo.

Rajee alichomwa sindano za upasuaji kwenye mashavu, kidevu,midomo, makalio na mapajani
Rajee Narinesingh alizaliwa New York na kukulia Philadelphia
Ole wenu wakina dada msiokubali namna mlivyoumbwa