Habari zilizotufikia hivi punde, zinaeleza kuwa Rais John Pombe Magufuli, amemteua Mhandisi John William Kijazi kuwa Katibu Mkuu Kiongozi, kuchukua nafasi ya Ombeni Sefue ambaye atapangiwa kazi nyingine. Kabla ya uteuzi huo, Mhandisi Kijazi alikuwa Balozi wa Tanzania nchini India.