SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Ijumaa, 4 Machi 2016

T media news

MESSI APIGA HAT-TRICK, BARCA YAVUNJA REKODI YA MIAKA 27



Barcelona imevunja rekodi iliyodumu miaka 27 nchini Hispania baada ya kucheza mechi 35 mfululizo bila kupoteza mchezo kwenye mashindano yote msimu huu hiyo ni baada ya kuichapa Rayo Vallecano kwenye mchezo wa usiku wa March 3 kuamkia March 4.

Leo Messi alipiga hat-trick kwenye mchezo huo baada ya wenyeji ya kukubali kipigo cha magoli 5-1 huku goli la kwanza likifungwa na Ivan Rakitic kutokana na makosa ya mlinda mlango wa Rayo.