SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Jumanne, 1 Machi 2016

T media news

MAKALA YA SHERIA: JE UNAHITAJI KUPIMIWA ARDHI MJINI, FUATA UTARATIBU HUU

Na  Bashir  Yakub.

Tunapoongelea  upimaji   ifahamike  kuwa  upimaji  upo  wa  aina  nyingi.Kutokana na hilo upimaji  unaoongelewa  hapa  ni  upimaji  miliki. Lakini  pia  tunaongelea   upimaji miliki wa  ardhi  mijini na  sio vijijini. Upimaji wa  ardhi miliki ni  upimaji  ambao  lengo  lake  ni  kummilikisha  mtu  ardhi. 

Kummilikisha  mtu  ardhi  sio  kumuuzia  ardhi.  Kummilikisha  mtu  ardhi  ni  kutambua  ardhi  yake  kimipaka  na  kumpatia  nyaraka  mahsusi(specific)  inayohusiana  na  umiliki( hati).  

Kwa  maana  hii  wanaomiliki  ardhi  ambazo  hazijapimwa   hatuwezi  kusema  wamemilikishwa  ardhi . Haijalishi  ardhi  hizo  ni  za  kwao na  wamezinunua  kwa  pesa zao. Kwa  kusema  hivyo  haimaniishi  kuwa  ambao  hawana  hati  au  hawajapima  ardhi  zao  basi  sio  wamiliki,  hapana  isipokuwa  ni  kuwa  tu kwamba hawajamilikishwa  kisheria  na  mamlaka    za  serikali. 

Kutokana  na  hilo   ardhi  iliyopimwa  na  ile  ambayo  haikupimwa  hutofautiana  hadhi na thamani kwa  kiasi  kikubwa.

1.NYARAKA  ZINAZOHITAJIKA   ILI  UPIMIWE  ARDHI.

( a )  Barua  kwenda  kwa  mkurugenzi.  Anayetaka  kupimiwa  ardhi   anatakiwa  kuandika  barua  kwenda  kwa mkurugenzi  wa  halmashauri  husika. Barua  ni  nyaraka  ya  kwanza  kabisa  ambayo unatakiwa  kuwa  nayo.  Ni katika  barua  hiyo  ambamo  utaeleza   nia  yako  ya  kutaka   kupimiwa  ardhi na  matumizi  ya  ardhi  yako kama  ni  makazi,kiwanda n.k.

( b ) Kuambatanisha  mkataba  wa  mauziano.  Katika  hatua  hii  mkataba  wa  mauziano utatambuliwa kama nyaraka  ya  umiliki. Mkataba  huu  ndio  utakaokutambulisha  kama  mmiliki  wa  ardhi  husika. Huu  unaambatanishwa  kwasababu  mmiliki  wa  ardhi  ndiye  mwenye  jukumu  la  kuomba  kupimiwa.  

Hivyo  kuambatanishwa  kwa  mkataba  kunathibitisha  kuwa  mmiliki  ndiye  anayeomba  kupimiwa  kwa  mujibu  wa  sheria. Ni  vema  mkataba  wa  umiliki  ukawa  ni  ule   mkataba  wa  kisheria   ulioandaliwa  na  kushuhudiwa  na  mwanasheria.

( c ) Barua  iliyotajwa  hapo  juu  katika  “A”  hakikisha  ina  muhuri  wa  mwen yekiti  wa  serikali  za  mtaa,  sahihi  pamoja  na mhuri  wa  mtendaji. Mwenyekiti  na  mtendaji  atakayetumika  sio  wa  pale  unapoishi    bali  pale  lilipo  eneo  unalotaka  kupima.  Kama  eneo  lipo  unapoishi  basi  utamtumia  huyohuyo  wa  eneo  unaloishi.