April 23 2016 uongozi wa klabu ya Liverpool ulitangaza kumsimamisha beki wa kati wa kimataifa wa Ufaransa anayeichezea klabu hiyo Mamadou Sakho kutokana na kugundulika kutumia dawa za kusisimua misuli michezo, dawa ambazo ni kinyume na taratibu. Shirikisho la soka barani Ulaya (UEFA) leo limetangaza uamuzi au adhabu ya kumsimamisha Mamodou Sakho kwa siku 30.