Kolo Toure pamoja na Simon Mignolet walizungumza na waandishi wa habari baada ya mchezo wao dhidi ya Villarreal ambao ulimalizika kwa Liverpool kuchezea kichapo mbele ya Villarreal.
Majogoo wa jiji waliruhusu goli dakika za lala salama lililofungwa na Adrian Lopez ambalo limaanisha Liverpool wanahitaji kushinda kwa magoli 2-0 kwenye mchezo wa marejeano wiki ijayo kama wanahitaji kufika fainali ya Europa League
Kolo Toure ambaye alianza kwenye safu ya ulinzi ya kikosi cha kwanza cha Liverpool kutokana na kufungiwa kwa Mamadou Sakho, alishindwa kuizuia pasi ya mwisho ya Denis Suarez iliyomfikia Adrian Lopez na kuifungia Villarreal goli.
Badala ya kujilamu, Mu-ivory Coasta huyo alimsifia Denis Suarez kwa pasi aliyopiga kwenda kwa mfungaji.
Kolo Toure na Simon Mignolet wakizungumza baada ya mchezo dhidi ya Villarreal