SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Ijumaa, 29 Aprili 2016

T media news

Hawa wa Nitarejea ya Diamond Ataka Menejimenti

Akiongea kwenye kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na east Africa Radio, Hawa amesema anaogopa kutangaza kuwa anahitaji mtu wa kumsimamia (manager) kutokana na aliyoyapitia siku za nyuma, na kuhofia kudharauliwa iwapo atatangaza kuhitaji meneja.

“Naogopa sasa hivi naogopa watu, nahitaji mtu wa kunisimamia, nahitaji kabisaa mtu wa kunisimamia niweze kufanya vitu vyangu, lakini siwezi kujieleza yaani , nikijieleza kwa kila mtu siwezi kumaliza, mtu mwenye imani yake anaweza akanisaidia, lakini siwezi kusema kwa kila mtu naonekana mi mwendawazimu, naonekana kama nimepagawa saa nyingine”, alisema Hawa.

Hawa ambaye siku za nyuma alikumbwa na mikasa tofauti tofauti ikiwemo ule wa kutelekezwa na mwanaume aliyemzalisha, baada ya kutangaza atamsadia na kuishia kumpachika ujauzito.

Kwa sasa mwanadada huyo anaendelea na shughuli za muziki na anaimba muziki wa injili, ingawa bado anaendelea na bongo fleva pia.

Tazama hapa moja ya kazi zake alizofanya hivi karibuni.

eatv.tv