Rais Magufuli Awaapisha Makatibu Tawala Wapya Wa Mikoa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewaapisha Makatibu Tawala wapya kumi aliowateua tarehe 25 Aprili, 2016 na kuwapangia vituo vyao vya kazi.

Makatibu Tawala hao wameapishwa leo tarehe 27 Aprili, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam na kisha wametia saini hati ya ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma, zoezi lililoendeshwa na Kamishna wa maadili Sekreatieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Mheshimiwa Jaji Salome Kaganda na kushuhudiwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi.

Makatibu Tawala walioapishwa ni;

    Arusha -         Richard Kwitega    Geita -             Selestine Muhochi Gesimba    Kagera -          Armatus C. Msole    Kilimanjaro - Eng. Aisha Amour    Pwani -           Zuberi Mhina Samataba    Shinyanga -    Albert Gabriel Msovela    Singida -         Dr. Angelina Mageni Lutambi    Simiyu -          Jumanne Abdallah Sagini    Tabora -         Dkt. Thea Medard Ntara    Tanga -           Eng. Zena Said

Makatibu Tawala wengine wa Mikoa ambao hawakuapishwa leo, ni wale waliohamishwa vituo vya kazi na wale waliobaki katika vituo vya kazi walivyokuwep,o ambao tayari walishakula kiapo cha kuwa Katibu Tawala wa Mkoa.

Gerson Msigwa

Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU

Dar es salaa

27 Aprili, 2016

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akimuapisha ndugu Albert Gabriel Msovela kuwa katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Ikulu jijini Dar es salaam April 27,2016

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akimuapisha ndugu Amantius Casmiri Msole kuwa katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera Ikulu jijini Dar es salaam April 27,2016

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akimuapisha ndugu Angelina Mgeni Lutambi kuwa katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Ikulu jijini Dar es salaam April 27,2016




Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

CHOMBEZO: UTAMU WA MADAM JESCA

Simulizi; MTOTO WA BOSS WANGU

SIMULIZI FUPI: UCHI WANGU UMENIPONZA