Diamond ni Msanii Pekee wa Afrika Mashariki Aliyetakwa Kuwania Tuzo za African Culture Image 2016

Msimu wa tuzo umeanza na mwaka huu kuna tuzo mpya imeanzishwa na taasisi ijulikanayo kama African Culture Initiatives. 

Imeanzisha tuzo ziitwazo African Culture Image (ACI) Awards ambazo ni kwaajili ya kuwatuza waafrika popote walipo duniani. 

Diamond ni msanii pekee kutoka Afrika Mashariki aliyetajwa kuwania tuzo hizo zilizotawaliwa na Wanaijeria. Ametajwa kuwania kipengele cha Male Artist of the Year akichuana na wasanii kama Wizkid, Davido, KCEE, Patoranking, Olamide na wengine. 

Tuzo hizo zitatolewa katikati ya mwaka huu huko Atlanta Georgia, Marekani. Bofya hapa kuanzia kumpigia kura Diamond.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

CHOMBEZO: UTAMU WA MADAM JESCA

Simulizi; MTOTO WA BOSS WANGU

SIMULIZI FUPI: UCHI WANGU UMENIPONZA