Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2017

STORY : MKE MWEMA. SEHUMU YA 4

Picha
MTUNZI :  SEIF JABU NAMBA :  + 258 845018401  wasap. Sehemu ya nne. Like yako ndiyo inafanya hadithi hii ipostiwe hivyo basi like ili iendelee... Hakika niliumia sana kuona yanayo mkuta mama yangu ili hali najua hana kosa lolote. "Halima mama kafanya nini mpaka atukanwe kiasi hicho?" " Alikuwa hayupo aliporudi akaitwa akaambiwa kuwa anatakiwa kuhamia nyumba ya nyuma ile ya chumba kimoja akahoji ataishi vipi na watoto katika chumba kimoja basi ndio wakaanza kumshambulia kwa maneno mpaka sasa." " Bibi yupo?" " Yupo na amenyamanza kimya." Nilijuliza tunateswaje ndani ya nyumba ya bibi yetu ili anajua sisi hatuna ndugu zaidi yake hapa mwanza. Nilitoka nikamuangalia mama yangu anavyo sukumwa huku akitukanwa nikaumia sana nikamfuta nikamshika mkono kisha nikatoa sauti kama kiume nikawauliza. " Mnahitaji nini kwa mama yangu mpaka mumshambulie?" "Ahame humu ahamie chumba cha nyuma." " Kafanya ko...

Asante Umoja wa Ulaya. Serikali yetu imwajibishe kila anayejihusisha na rushwa.

Picha
Waraka toka Mlimani Rais Dkt Magufuli ambaye mapema juma hili juhudi zake za kupambana na rushwa ambazo zimeanza kuzaa matunda zimepongezwa na Umoja wa Ulaya (EU) Mapema juma hili, Umoja wa Ulaya (EU) umempongeza Rais Magufuli na mikakati yake katika kupambana na rushwa na kumuahidi kumuunga mkono zaidi. Pamoja na pongezi hizo imetoa msaada wa shilingi bilioni 40 bilioni za Kitanzania katika kupambana na rushwa. Balozi wa EU nchini Tanzania na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) amesema kuwa fedha hizo zitatumika katika mpango wa “Ongeza uwajibikaji kwa kupambana na rushwa na kuchukua hatua za kisheria.” Hakika, ni matumaini ya walio wengi kuwa serikali itahakikisha mkakati huo unatekelezwa kikamilifu. Siku za hivi karibuni kumekuwa na idadi kubwa ya watu wakishtakiwa kwa makosa ya rushwa na uhujumu uchumi nchini. Mfano wa watuhumiwa wa kesi hizi za rushwa ni mfanyabishara Yusuf Manji na wengine ambao wana orodha ya makosa madogo na mashatka mengine makubwa yakihusishwa n...

Waziri Mbarawa Atoa Maagizo Mazito Bodi na Menejimenti ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA)

Picha
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, amesema anasikitishwa na utendaji wa Bodi na Menejimenti ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), kutofanya maamuzi kwa wakati hali ambayo inachangia malalamiko kuongezeka Bandarini hapo. Aidha, Mbarawa amesema Serikali inapeleka Naibu Mtendaji Mkuu mpya wa shughuli za Uendeshaji Bandarini hapo kutokana na aliyekuwepo kushindwa kusimamia majukumu yake ipasavyo. Profesa Mbarawa amesema hayo leo wakati wa ziara ya kushtukiza aliyoifanya bandarini ikiwa ni siku chache baada ya Rais John Magufuli, na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, kufanya ziara ya kustukiza na kubaini madudu bandarini hapo. Ziara ya Waziri Mbarawa ni mwendelezo wa ziara mbalimbali bandarini hapo  kubaini uendeshaji na utendaji wa shughuli zinazotolewa na Mamlaka hiyo. “Nimelazimika leo kuwaita Watendaji na Bodi ya TPA ili kuwaeleza kasoro zenu  ambapo inaonesha wazi kuwa  asilimia kubwa ya mambo yanayotokea humu  ni  kuwa mnakuw...

Rais Magufuli afanya uteuzi wa Bi. Stella Chagi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Bi. Stella Tullo Chagi kuwa Msajili wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba wa Wilaya. Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi huu umeanza tarehe 25 Novemba, 2017. Kabla ya uteuzi huu Bi. Stella Tullo Chagi alikuwa Msajili Msaidizi wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Gerson Msigwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU Dar es Salaam 30 Novemba, 2017

Mfanyabiashara Akamatwa na Kilo Nane za Dhahabu Uwanja wa Ndege

Picha
Mfanyabiashara, Naushad Mohamed Suleiman amekamatwa katika Uwanja wa Ndege Zanzibar alikokuwa asafirishe kilo nane za dhahabu. Pia amekutwa na fedha taslimu za mataifa 15. Kaimu Kamishna wa Polisi Zanzibar, Juma Yussuf Ali amesema leo Alhamisi Novemba 30,2017 kuwa, mtuhumiwa alikamatwa jana Jumatano Novemba 29,2017 saa tatu usiku akitaka kusafiri na ndege ya Fly Dubai. Amesema miongoni mwa fedha alizokutwa nazo ni dola 235,000 za Marekani na euro 57,000. Juma amesema mfanyabiashara huyo alikamatwa baada ya upekuzi kufanyika kwenye mizigo yake. Amesema ili kusafirisha madini na fedha ni lazima kuwa na vibali kutoka mamlaka husika ndiyo maana wanamshikilia na itakapobainika hakuna utaratibu uliokiukwa ataachiwa. Juma amesema kazi ya polisi ni kufanya mahojiano na mtuhumiwa. Chanzo: Mwananchi

Malinzi, Aveva Wakwama Mahakamani Warudishwa Rumande

Picha
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeziahirisha kesi za utakatishaji fedha inayowakabili Rais wa klabu ya Simba, Evans Aveva na ile inayomkabili aliyekuwa Rais (TFF), Jamal Malinzi hadi December 14,2017 kwa sababu upelelezi haujakamilika. Mwendesha Mashtaka wa Takukuru, Vitalis Peter amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri kuwa kesi ya Aveva na Malinzi zimeitishwa kwa ajili ya kutajwa na upelelezi wa kesi hizo bado haujakamilika. Baada ya kueleza hayo, Hakimu Mashauri ameahirisha kesi hizo hadi December 14/2017. Kwa pamoja washtakiwa hao wanadaiwa kuwa walikula njama ya kughushi fomu ya maombi ya kuhamisha fedha ya March 15,2016 wakionesha Klabu ya Simba inalipa mkopo wa  USD 300,000 kwa Evans Aveva wakati si kweli.

Wanasiasa Muda Mwingine Tunawasha Moto Tunashindwa Kuuzima- Nape Nnauye

Picha
Ilikua ni wakati wa kuufungua Msikiti mpya uliojengwa katika jimbo la Mtama linaloongozwa na Mbunge Nape Nnauye ambapo waliohudhuria ni pamoja na Mufti wa Tanzania mwenyewe, Waziri wa zamani Benard Membe na wengine. Kwenye ufunguzi huo Nape Nnauye alinukuliwa akisema “Sisi Wanasiasa wakati mwingine tunawasha moto mwingi mno tunashindwa kuuzima lakini kupitia Dini zetu hizi kama mambo yakiwekwa vizuri mioto mingi inazimika na mambo yanakwenda vizuri“ “Tumeanza kuona wakati mwingine tunafanya chaguzi zetu, watu wanakatana mapanga, watu wanapigana…. wanashutumiana, hili jambo sisi Wanasiasa tunaweza tukashindwa kulihimili lakini nyinyi viongozi wa dini mkisimama mkatusaidia inawezekana sababu watu hawa wanatoka miongoni mwetu humuhumu“

Ahmed Albaity Aliyelala Kitandani Miaka 10 Asaidiwa na Makonda Kutibiwa kwa Milion 85 Nchini China

Picha
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amejitolea kumsaidia kijana Ahmed  Albaity  anayesumbuliwa na tatizo la uti wa mgongo lililompelekea kulala kitandani kwa takribani miaka 10. Kijana huyo anatakiwa kwenda kutibiwa nchini China kwa muda wa wiki tatu akiambatana na wasaidizi wawili ambapo gharama za matibabu zinazohitajika ni zaidi ya dola 40,000 za marekani ambapo sindano moja aliyoandikiwa inagharimu kiasi cha dolla 27,000. RC Makonda amesema atafanya jitihada zote kuhakikisha Ahmed anapatiwa Matibiwa ili aweze kupona na kutimiza ndoto zake akiwa na Afya Njema. Mapema leo RC Makonda ametembelewa ofisini kwake na Balozi mpya wa China Nchini Tanzania Bi. Wang Ke ambae amekuja kujitambulisha kwa Mkuu wa Mkoa ambapo katika mazungumzo RC Makonda amemgusia balozi huyo suala la matibabu ya AHMED ALBAITY ambapo Balozi WANG KE alieambatana pia na Daktari Bingwa wa China aliebaki Nchini kwaajili ya Shughuli ya Serikali ya China ambapo wamemtazama na kupitia Ripoti ambapo wa...

Rais wa Nigeria atoa neno kuhusu soko la watumwa Libya

Picha
Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ameingilia kati suala ambalo sasa limeigusa dunia nzima kwa kitendo cha raia wa Libya kuwauza kama watumwa wahamiaji wanaoingia nchini humo. Kwenye ukurasa wake wa twitter Rais Buhari amesema vitendo hivyo havikubaliki, na kwamba wako tayari kufanya lolote kuwalinda raia wake ambao pia ni miongoni mwa wahanga wa biashara hiyo, yenye ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu. “Hali ya Libya ya watu kuuzwa ni ya kutisha na haikubaliki, tutafanya kila kitu kuwalinda raia wetu popote walipo, na pia tumeshaanza kuwarudisha nyumbani wanigeria wote waliopo Libya na sehemu nyingine, tutahakikisha wote wanarejea nyumbani salama na kuhudumiwa”, ameandika Rais Buhari. Kitendo cha raia wa Libya kuwauza wahamiaji wanaoingia nchini humo ambao wengi wao ni raia wa mataifa ya Afrika Magharibi, kimeishtua dunia nzima ambapo mpaka watu maarufu mbali mbali duniani, wamekuwa wakipost kwenye mitandao ya kijamii kukemea vitendo hivyo.

Mbunge wa CUF Ashinda Pingamizi la Serikali Mahakamani

Picha
Mbunge wa Malindi (CUF), Ally Saleh ameruka kihunzi cha Serikali mahakamani, baada ya kushinda pingamizi la awali lililowekwa na Serikali katika kesi ya kuhoji uhalali wa wajumbe wapya wa bodi ya wadhamini wa chama hicho. Saleh ambaye pia ni mwanasheria amefungua kesi Mahakama Kuu akihoji uhalali wa wajumbe wapya wa bodi waliosajiliwa na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (Rita). CUF imegawanyika pande mbili; inayomuunga mkono Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad na inayomuunga  Mwenyekiti, Profesa Ibrahim Lipumba anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, ambaye ndiye aliunda bodi inayopingwa. Wadaiwa katika kesi hiyo ni Ofisa Mtendaji wa Rita, anayewakilishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) kupitia jopo la mawakili wa Serikali linaloongozwa na Gabriel Malata. Wengine ni bodi ya wadhamini (mpya) ya CUF, mwenyekiti wa bodi hiyo, Peter Malebo, wanaowakilishwa na wakili Majura Magafu na wajumbe wapya wa  bodi hiyo wanaowakilishwa na wakili Mashaka Ngol...

Tundu Lissu Afunguka Mazito Hali Ilivyokuwa Siku ya Tukio la Kushambuliwa

Picha
 Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu amesimulia hali ilivyokuwa siku ya tukio na pia kueleza ujumbe aliompa Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan alipomtembelea hospitalini jijini hapa juzi. Mbunge huyo, ambaye alishambuliwa kwa risasi akiwa ndani ya gari lililoegeshwa nje ya makazi yake mjini Dodoma Septemba 7, pia amesema amepitia majaribu mengi, lakini “hili ndilo kubwa”. Amesema hali yake inaendelea vizuri na madaktari wanamuelezea kuwa ni “muujiza unaoishi” baada ya kufanikiwa kuunganisha vipande vya mwili ulioharibiwa kwa risasi. Lissu alisema hayo alipofanya mahojiano na Mwananchi, ikiwa ni mara ya kwanza kwa chombo cha habari cha Tanzania tangu ashambuliwe. Lissu amelazwa Hospitali ya Nairobi jijini hapa tangu Septemba 7 na huenda akahamishiwa nje ya bara la Afrika kwa matibabu zaidi, ambayo yatahusu mazoezi, kabla ya kurejea nchini. Akizungumza na Mwananchi hospitalini hapo, Lissu alisema sasa anaamini kuwa Rais John Magufuli anajua kuna mgonjwa Nairobi...

LHRS Yazungumzia Uchaguzi Mdogo wa Madiwani " Kulikuwa na Ukiukwaji Mkubwa wa Haki za Binadamu"

Picha
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimesema kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu katika uchaguzi mdogo wa madiwani. >Ukiukwaji huo ni kama watu kupigwa na kutekwa na vyombo vya dola na wafuasi wa vyama vya siasa Wametoa mfano kata ya Kitui Iringa vijana wa CCM waliwavamia na kuwateka wanachama wa CHADEMA waliofahamika kwa majina ya Eliza Nyenza na Martha Francis na kuwapora na kuwanyanganya simu zao na kuwatupa katika msitu wa Kilolo Kushambuliwa kwa Naibu Meya wa Manispaa ya Iringa, Daudi Igogo na jeshi kumkamata na kumshikilia Alex Kimbe Pia mfuasi wa CCM jimbo la Kawe alivamiwa na kupigwa na watu wanaodaiwa kuwa wafuasi wa CHADEMA Katika kata ya Makiba wakala wa CHADEMA, Rashid Jumanne na Mwenyekiti wake wa tawi la Valeska, ndugu Nickson Mbise walijeruhiwa vibaya kwa kushambuliwa na mapanga asubuhi wakielekea vituo vya kupigia kura Pia katibu wa ccm wilaya ya Itilima mkoani Simiyu alilazwa hospitalini baadaya kushambuliwa na watuwanaodaiwa kuwa wafuasi...

Waziri Mkuu aruhusu kozi za 'Foundation' Chuo Kikuu Huria

Picha
Chuo Kikuu Huria pekee kimepewa ruhusa ya kuendelea kutoa kozi ya Foundation iliyokuwa imesitishwa na serikali kwa wanafunzi ambao wamekosa vigezo vya kujiunga na elimu ya Chuo Kikuu baada ya mtaala wake kuboreshwa na kupitishwa na Wizara ya Elimu. Ruhusa hiyo imetolewa na Waziri Mkuu, Mh. Kassim Majaliwa leo akiwa mkoani Singida yanapofanyika Mahafali ya chuo hicho. Ikumbukwe kuwa Mwaka 2016 Naibu Waziri wa Elimu, Mhandisi Stella Manyanya alitoa katazo hilo na kusema utaratibu wa kozi ya Foundation umefanywa na  vyuo  vyenyewe hivyo serikali haiwezi kuukubali mfumo wa  elimu hiyo na kwamba kama mtu anasoma kozi ya Foundation apewe cheti na kama atahitaji  kujiendeleza asafishe cheti au asome mfumo ambao utamfikisha katika shahada. Mbali na hayo katika Mahafali hayo ambayo Waziri Mkuu ndiye Mgeni rasmi atamtunuuku mkewe Bi Mery Shahada ya Uzamiri ya Elimu. "Wakati najiandaa kuja kwenye sherehe mwenzangu naye kumbe anajiandaa,  nashukuru amemaliza sasa mambo...

Ili Kuonyesha Hatukubaliani na Biashara ya Utumwa Libya Kilimanjaro Stars Isiingie Dimbani Jumapili- Zitto Kabwe

Picha
Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo na Mbunge wa Kigoma Mjini Mh. Zitto Kabwe ameitaka timu ya taifa ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) kutoshuka dimbani kuikabili Libya siku ya Jumapili katika michuano ya CECAFA ikiwa ni hatua ya kuonyesha kuchukizwa na vitendo vya biashara ya utumwa vinavyoendelea katika nchi hiyo. Zitto ameyasema hayo kupitia ukurasa wake wa kijamii wa Twitter ikiwa zimesalia siku chache  kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania Bara kucheza mchezo wake wa kwanza siku ya Jumapili ya Desemba 3 dhidi ya Libya katika michuano ya Afrika Mashariki na Kati inayofanyika huko nchini Kenya. Leo @masoudkipanya ameshauri Tanzania isusie mechi yake dhidi ya Libya siku ya Jumapili kuonyesha kuchukizwa na Biashara ya Utumwa. Ninaunga mkono. Tanzania isiingie Uwanjani kucheza na Libya. @SADC_News iagize nchi zake zote zirudishe mabalozi wake kutoka Libya. Kilimanjaro Stars itacheza mchezo huo wa kundi A, katika kuwania kombe la michuano ya Afrika Mashariki na Kati CECAFA amb...

Bunge Lawatosa Wabunge 8 wa CUF Ambao Waliovuliwa Uanachama

Picha
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limetoa ufafanuzi juu ya maamuzi ya mahakama kuhusu wabunge 8 wa CUF ambao walivuliwa uanachama na kupoteza sifa kuwa wabunge na kusema katika maamuzi ya mahakama hakuna sehemu imesema watu hao wapewe Ubunge. Katibu wa Bunge amesema kuwa amekuwa wakiona kwenye mitandao ya kijamii na katika vyombo vya habari taarifa mbalimbali zikisema kuwa wabunge hao ambao walivuliwa uanachama na CUF kuwa wanatakiwa kurudishiwa ubunge wao na kudai hakuna jambo la namna hiyo kwa kuwa nafasi zao tayari zilijazwa na Tume ya Uchaguzi. 

I SAY NO TO SLAVERY IN LIBYA BLACK IS NOT FOR SALE.

Picha
Dunia inashangaa walibya leo kuuzwa kama( Bidha) watumwa ,Naona watu wanavyo jitokeza kulaani , Hawa wanao jitokeza leo , hawakujitokeza wakati  kiongozi wa Libya anaondolewa madarakani kijeshi ( wanafiki) na huenda ndio hao hao walio kuwa wakichochea vijana hawa hawa wanao uzwa leo wafanya vurugu na kuwapa siraha Tripoli  . Tunauliza wako wapi  walio iita ile ni Demokrasia kwa kiwango kikubwa?( kimya) wako wapi walio uita ni mbadilishano wa Utawala ( Kimya) . Mimi nauita ni UZWAZWA . Lakini katika hili la Libya nasema Obama alaumiwe na kila Mwana Africa anayeguswa na hili , alikubali kutuuza ndugu zake ,Obama alisaliti  asili yake na asili ya wazazi wake na hayo ndo matokeo yake . Obama have something to pay for  this Africa and Libya! Alikuwa na Nafasi kubwa ya kuyaona haya ,alikuwa na nafasi kubwa ya kuyazuia haya . Wako wapi WANA UMAJUI wa Africa ( PAN AFRICAN) buriani Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere ,  Burian Nkwame Nkuruma tunawezaje kuruhusu h...

PONGEZI

Picha

Mhalifu wa Kivita Afariki Baada ya Kunywa Sumu Mahakamani

Picha
Kikao cha kusikiliza rufaa iliyowasilishwa na washtakiwa wa uhalifu wa kivita mjini The Hague, Uholanzi kimesitishwa ghafla baada ya mmoja wa washtakiwa kusema amekunywa sumu baada ya kusikiliza hukumu. Slobodan Praljak, 72, alikuwa mmoja wa viongozi sita wa zamani wa kisiasa na wa kijeshi wa Bosnia wa asili ya Croatia ambao walikuwa wamefika mahakamani. Amefariki akitibiwa hospitalini na Umoja wa Mataifa umesema sasa mahakama hiyo ni "eneo la uhalifu". Alikuwa amehukumiwa kufungwa jela miaka 20 mnamo 2013 kwa makosa ya uhalifu wa kivita yaliyotekelezwa katika mji wa Mostar. Baada ya kusikiliza hukumu kwamba majaji walikuwa wamedumisha kifungo hicho, alimwambia jaji, "Nimekunywa sumu". Sita hao walikuwa wanasikiliza uamuzi wa mwisho wa rufaa uliokuwa unatolewa na mahakama maalum ya kimataifa ya UN iliyokuwa inashughulikiwa makosa yaliyotekelezwa Yugoslavia (ICTY). Ingawa walikuwa washirika dhidi ya Waserbia wa Bosnia wakati wa vita hivyo vya 1992-95, Wacroati...

Mwanamke Kukaa Bila Kuolewa Aileti Picha Nzuri Nami Naolewa Ili Kutoa Nuksi- Sasha

Picha
MWANADADA mwenye mvuto wa aina yake Bongo, Sasha Kassim ambaye anatarajia kufunga ndoa mwanzoni mwa mwaka kesho amesema kuwa, ameamua kuolewa ili kutoa nuksi. Sasha ambaye hujulikana sana mitandaoni kwa picha zake za kihasara, alisema hadi sasa bado hajaenda kutambulishwa ukweni na wala hakuna mpango huo, ila amekuwa akiwasiliana na wakwe zake kwa njia ya simu, baada ya ndoa ndipo ataenda kupata baraka zao lakini makazi yake yataendelea kuwa Bongo. “Naolewa kutoa nuksi si unajua mwanamke kukaa bila ndoa haileti picha nzuri, wakwe zangu wamenikubali japo hawajawahi kuniona laivu zaidi ya kwenye simu, nimeshaongea na mume wangu mtarajiwa kwamba akinioa nitaendelea kuishi Bongo, sababu napapenda sana huko Italy nitakuwa naenda kwa muda mfupi na kurudi na amekubali,” alisema Sasha ambaye anatarajia kuolewa na Bonphace, raia wa Italy.

Hii Hapa Tiba Mbadala ya Ganzi Mikononi, Miguuni

Picha
GANZI mikononi na miguuni, ni tatizo linaloashiria kukosekana kwa fahamu katika sehemu hizo. Hisia ndiyo inakosekana kwa sababu hakuna damu na neva zinakosa mawasiliano ya moja kwa moja na ubongo. Ni jambo la kawaida linalowapata watu wengi sana katika miaka ya hivi karibuni, lakini pasipo kujua nini chanzo chake wala tiba. Vyanzo vya ganzi mwilini Vifuatavyo vinatajwa kuwa vyanzo vya ganzi mwilini mwa binadamu: 1. Shinikizo la muda mrefu kwenye miguu na mikono.2. Kuwa karibu na vitu vyenye baridi sana kwa kipindi kirefu.3. Mabadiliko ya muda mfupi kwenye neva/mishipa.4. Ajali kwenye neva.5. Kunywa pombe kupita kiasi.6. Uvutaji sigara na bangi.7. Uchovu usioisha. 8. Kutokujishughulisha na mazoezi ya viungo kila mara.9. Ukosefu wa vitamini B12 na Magnesiamu mwilini,10. Ugonjwa wa kisukari n.k Kwa kawaida, ganzi inayotokea kwa dakika kadhaa na kupotea huwa haina shida yoyote. Inaelezwa, ni vyema kuonana na daktari mapema, iwapo ina kawaida ya kutokea kila mara na inadumu muda mre...

Watalii Wakamatwa kwa Kuonyesha Makalio Hekaluni

Picha
Raia wawili wa Marekani wamekamatwa nchini Thailand baada ya kuchapisha picha yao mtandaoni wakionyesha makalio yao katika hekalu. Watalii hao walipiga picha hiyo katika hekalu maarufu nchini Bangkok Wat Arun na kuichapisha katika mitandao ya Twitter na instagram. Mamlaka ya uhamiaji iliambia BBC kwamba wawili hao Joseph na Travis Dasilva wote wakiwa na umnri wa miaka 38 watapigwa faini na kurudishwa kwao. Thailand ina sheria kali kuhusu tabia zinazoonekana kutokuwa na heshima na zinazoingilia dini yake ya Buddha. Watalii hao walikamatwa jioni Jumane wakati walipokuwa wakiondoka nchini humo katika uwanja wa ndege wa Bankok Don Mueang. Naibu msemaji wa idara ya uhamiaji nchini Thailand, kanali Choengron Rimpadee aliambia BBC kwamba wawili hao walikuwa katika orodha ya watu waliokuwa wakichunguzwa baada ya mamlaka kuona picha hizo zenye utata katika mitandao ya kijamii. ''Wakati watakaposhtakiwa maafisa wa polisi wa uhamiaji wa Thailand watafutilia mbali visa zao na kutaka...

Waombolezaji Watimua Mbio na Kulitelekeza Jeneza Lenye Mwili wa Marehemu

Picha
HALI ya taharuki na hofu imezuka katika Kijiji cha Katani Kata ya Nkandasi wilayani Nkasi mkoani Rukwa na kusababisha waombolezaji kutimua mbio na kuacha jeneza lenye mwili wa marehemu baada ya mvua kubwa kuanza kunyesha na kubomoa nyumba za wakazi wa kijiji hicho. Tukio hilo lilitokea jana saa 6 mchana baada ya kuanza kunyesha mvua kubwa iliyoambatana na radi na upepo mkali ulioezua baadhi ya nyumba za wananchi hao ambao walikuwa wakiomboleza msiba wa mwananchi mwenzao aliyefariki baada ya kuugua siku chache zilizopita.  Mwenyekiti wa serikali ya kitongoji cha Kaungo, Robert Kanoni, alisema wakiwa wanaelekea kufanya maziko ya marehemu Dismas Kanoni aliyefariki jana, ghafla ilianza kunyesha mvua kubwa ikiambatana na radi na upepo mkali hali iliyosababisha baadhi ya waombolezaji kutimua mbio na kurejea majumbani kutokana na hofu iliyoibuka kufuatia tukio hilo. Baadhi ya wananchi walivumilia nakurejea na jeneza lililokuwa na mwili wa marehemu nyumbani na kuahilisha maziko kwa...

Baraka Da Prince Awaduwaza Mashabiki wa Alikiba

Picha
Kwa muda mrefu sasa wadau wengi wa muziki wa Bongo Fleva wamekuwa wakiamini kuwa Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Barakah The Prince na mfalme wa Bongo Fleva, Alikiba wana bifu au tofauti miongoni mwao baada ya Baraka The Prince kujitoa kwenye lebo ya RockStar4000 ambayo ipo chini ya Alikiba na Meneja wake Seven Mosha. Ukweli ni kwamba Barakah The Prince hana tofauti/bifu  yoyote na Alikiba kama ambavyo mashabiki wengi wa Alikiba na wadau wa muziki walivyokuwa wakidhania kwani  Hitmaker huyo wa Sometimes kupitia ukurasa wake wa Instagram amethibitisha hilo kwa kumtakia Kheri ya siku yake ya kuzaliwa Alikiba . Alikiba leo Novemba 29, 2017 anasherehekea siku yake ya kuzaliwa na mastaa kibao wamemposti kwenye kurasa zao za mitandao ya kijamii kumtakia maisha kheri akiwemo Ommy Dimpoz, Mwana FA, na wengineo.

Trump Ajibu Mapigo 'Tutaiangamiza Korea Kaskazini Iwapo Vita Itatokea

Picha
Marekani imeyataka mataifa yote kukatiza uhusiano wa kidiplomasia na ule wa kibiashara na Korea Kaskazini baada ya taifa hilo kufanyia jaribio la kombora lake la masafa marefu. Akizungumza katika baraza la usalama la umoja wa kimataifa ,mjumbe wa Marekani katika baraza hilo Nikki Haley amesema kuwa rais Trump amemtaka mwenzake wa China kukata usambazaji wa mafuta kwa Pyongyang. Amesema kuwa Marekani haitaki mzozo lakini Korea Kaskazini itaangamizwa iwapo vita vitazuka. Onyo hilo linajiri baada ya Pyonyang kufanyia majaribio kombora lake la kwanza katika kipindi cha miezi miwili. Marekani: Korea Kaskazini ilikusudia uchokozi Marekani yailalamikia Korea Kaskazini Marekani yatishia kuiadhibu Korea Kaskazini Korea Kaskazini imesema kuwa kombora hilo lililorushwa siku ya Jumatano ambalo inasema liliruka kimo cha kilomita 4,475, ikiwa ni mara kumi zaidi ya kimo cha kituo cha angani. Madai hayo hayakuthibitishwa na wataalam wametiliashaka uwezo wa taifa hilo kuwa na teknolojia kama h...

Ferooz Afunguka Prof Jay , Chege Kumtenga

Picha
Msanii wa muziki wa bongo fleva, Ferooz ambaye anafanya vyema na wimbo wake 'Nakaza roho' ameweka wazi kuwa alichoimba kwenye wimbo huo ni ukweli mtupu na kusema kuna watu wake wa karibu kama Prof Jay, Chege wamempa kisogo. Ferooz akipiga stori na mwandishi wa tovuti ya EATV amesema kuwa watu wake wa karibu wengi wao walimtenga na kumuweka pembeni na kudai hata alipojitahidi kuwatafuta lakini mawasiliano hayakuwa mazuri, jambo ambalo anasema hakutegemea kutokana na namna alivyokuwa akiishi na watu hao. Mbali na hilo Ferooz anasema katika kipindi ambacho aliyumba kimaisha alizidi kukatisha tamaa na watu wengi mbalimbali lakini alijipa matumaini na kupigana jambo ambalo anaona limeanza kuleta matumaini kutokana na watu kumpokea vyema na wimbo wake huo mpya 'Nakaza roho'  "Kiukweli namshukuru Mungu kwani wimbo huu umepokelewa vizuri na mashabiki wangu kila kona na sasa naanza kuona mtaani umeanza kufanya vizuri, kiukweli wimbo huu umenipa matumaini mapya kuwa nawe...

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya Novemba 30

Picha