MO Kukabidhiwa Simba SC Hali Bado Tete
Rais wa Simba SC, Evans Aveva akizungumza na wanachama wa timu hiyo leo wakati wa mkutano mkuu. Eneo la mkutano mkuu wa Simba Ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi, Oyesterbay jijini Dar. SIKU chache baada ya mfanyabiashara Mohamed Dewji ‘MO’ kutangaza kuwa yupo tayari kutoa kitita cha Sh bilioni 20 kuwekeza katika Klabu ya Simba ili ipate mafanikio, mpango wake huo unaonekana kutaka kugonga mwamba. Baada ya mkutano mkuu wa klabu hiyo uliofanyika leo katika Ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi, Oyesterbay, ambao ulikuwa na ajenda 10, moja kati ya ajenda hizo ilikuwa ikizungumzia taarifa ya kamati ya maboresho ya mfumo wa uendeshaji wa klabu hiyo. Katika ajenda hiyo ndipo lilipojitokeza suala zima la MO ambapo wanachana hao wa Simba zaidi ya 700 waliojitokeza kwenye mkutano huo walitaka bilionea huyo apewe timu hiyo kutokana na hali mbaya ya kiuchumi iliyopo klabu hapo ambapo imekuwa ikijiendesha kwa hasara kila mwaka. Katika msimu wa 2014/15 klabu hiyo ilifanikiwa kujik...