Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari, 2017

Maambukizi katika viungo vya uzazi vya mwanamke (PID)

Picha
Wiki hii mpenzi msomaji wangu namalizia aina za magonjwa yanayohusiana na mwanamke kupata muwasho na kutokwa na majimaji ukeni, Pelvic Inflammatory Diseases ‘PID.’ Ugonjwa huu hushambulia viungo vya ndani vyote vya uzazi vya mwanamke na kusababisha mwanamke apate maumivu chini ya kitovu na maumivu wakati wa kujamiiana kwa muda mrefu. Maambukizi katika tabaka la ndani la kizazi huitwa ‘Endometritis’, maambukizi ya mirija ya uzazi huitwa ‘Salpngitis’ na pia mwanamke anaweza kupata uvimbe ndani ya kizazi ambao unakuwa umejaa usaha uitwao ‘Tubo-ovarian abscess’ na maumivu makali ya muda mrefu ya tumbo kuanzia usawa wa kitovu kushuka chini ‘Pelvic Peritonitis’. Ugonjwa huu zaidi huenezwa kwa njia ya kujamiiana na husababishwa na bakteria ‘Neisseria Gonorrhoea’ na ‘Chlamydia Trachomatis’. Wengine wanaoweza kusababisha ni ‘Gardnella Vaginalis’, Haemophilus Influenza’, ‘Enteric gram n...

CHANGO KWA WATOTO WACHANGA(COLIC)

Picha
Watoto wachanga wanasumbuliwa na chango(colic) wanapokuwa na umri wa wiki 2 baada ya kuzaliwa ndipo wanapata achango. Chango ni maamivu makali ya tumbo anayopata mtoto na kulia mara kwa mara ikiwa usiku , mchana au jioni ,anaweza kulia zaidi ya msaaa 3 kwa siku usiku . Chango inachukua mda wa miezi 3-4 ndio mtoto apone,ingawa sio watoto wote wanapata na tatizo la chango. Sababu za kuleta chango kwa mtoto? Maziwa ya ngo’mbe yana protein nyingi , lactose inayopatikana kwenye baby formulas .(hayo yote yanaweza mletea allergy na maumivu ya tumbo) Mtoto atakapo nyonyeshwa sana mpaka kuvimbilwa (overfeeding)huchochea chango. Hormones-zinachochea mletea maumivu ya tumbo (mtoto akiwa na stress ya mazingira au mama anaposhindwa  kumweka position nzuri wakati wa kunyonya) Gesi – mtoto ,akiwa analia au kunyonya kwa haraka  anameza hewa inayokuja kuleta gesi na  kumuumiza  tumbo. Kiungulia(heartburn) Dalili ya chango kwa mtoto (colic) Mtoto atalia sana...

Gwajima asema atamshitaki Makonda kwa Mungu

Picha
Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima ameendelea kuonyesha msimamo wake wa kumshtaki Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwa Rais Magufuli huku akidai endapo ataona hakuna hatua inayochukuliwa atamshtaki kwa Mungu na majibu yatapatikana. Askofu Gwajima aliyasema hayo Jumapili hii wakati akiongoza ibada ya Jumapili kanisani kwake Ubungo Maji. “Watu wananiuliza, nitamfungulia kesi. “Mimi nawaambia nitamwambia Rais Magufuli kama nilivyosema, kama hakuna kitu kitakachofanyika basi nitamwambia Mungu aliye juu na majibu yatapatikana,” alisema Askofu Gwajima. Aidha Askofu huyo alisema yeye alipochokozwa haikuwa bahati mbaya ila alidai wanaomchokoza ni sawa na kufungulia koki ya maji yenye mgandamizo mkubwa au wamebusu transfoma ya umeme ambayo ni hatari kwa maisha ya binadamu kuisogelea kama huna utaalamu nayo kwa sababu husababisha kifo. Hata hivyo Askofu huyo alitoa mstari uliopo kwenye biblia ambao ni Yeremia 22: 11 ambapo alisema kila jambo lin...

Zitto Kabwe aililia serikali ugumu wa maisha

Picha
Mbunge wa Kigoma Mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo Mhe. Zitto Kabwe amefunguka na kuililia serikali juu ya ukali wa maisha nchini kufuatia gharama za maisha kupanda. Mhe. Zitto Kabwe ameitaka serikali ifanye juhudi na jitihada kupunguza au kumaliza kabisa ukali wa maisha kwa wananchi kwani "Mtwara unga wa ugali ( sembe) Sasa tshs 2000 - 2200 kwa kilo moja. Gharama za maisha ya mwananchi zimeongezeka sana kutokana na uhaba wa chakula maeneo mengi ya nchi yetu. Juhudi zifanyike kupooza ukali huu wa maisha unaokabili wananchi" alisisitiza Zitto Kabwe. Baadhi ya wananchi waliungana na Mhe. Zitto Kabwe juu ya kupanda kwa bei ya unga na katika maeneo yao kama ifuatavyo.

Wema Sepetu amchinjia baharini Batuli

Picha
Sasa Wema Sepetu na Batuli ni mbuzi na chui, urafiki ndio umefika mwisho. Tukio hilo limetokea baada ya Wema kukasirishwa na kitendo cha Batuli kusema kuwa yeye alishalipwa fedha zake za kampeni na CCM. Kupitia mtandao wa Instagram, Wema Sepetu ameweka picha ya rafiki yake huyo wa zamani na kuandika ujumbe ambao umeashiria kuwa urafiki wao ndio basi tena. “Neno Moja Kwake…! Temporary Post… Mimi naanza… Alikuwa Rafiki yangu na Tulipendana sana….,” ameandika Wema kwenye picha ya Batuli hiyo hapo juu aliyoiweka kwenye mtandao huo. Baada ya ujumbe huo wa Wema, Nay wa Mitego amemchochea muigizaji huyo ambaye wote kwa sasa wanakisupport Chadema kwa kuandika, “ @wemasepetu #MudaWetu Wana Maneno Mengi Tatizo Hawa Action… Usi mwamini ndugu Ata Rafiki, wachukulie Wote wanafiki, ishi tu kivyako Binadamu awa aminiki..!  Bongo5

TANGAZO:TAWFIQ MONEY SERVICE WAKALA WA KIBANK BUNDA

Picha
ANAPATIKANA BARABARA YA BOMANI MKABALA NA STENDI YA ZAMANI TUNATOA HUDUMA ZIFATAZO KWAJIA YA BANK: -KUFUNGUA AKAUNTI ZA CRDB,EQUITY ,POST  BANK. -KUWEKA PESA -KUTOA     PESA -KUTUMA  PESA -KULIPIA ADA ZA SHULE -KULIPIA MALIPO MBALIBALI YA SEREKALI. KUWEKA PESA NA KUTUMA NI BURE KABISA.  PIA TUNATOA HUDUMA ZA :- - BIMA ZA MAGARI - MOTOR VAHICLE PIA TUMEFUNGUA OFISI  NYINGINE NYASURA STENDI UPANDE WA GARI ZINAZO KWENDA MWANZA KARIBUNI KUPATA HUDUMA LUKU VING'AMUZI VYA TV SIMU NAMBA 0784699901,0756141420      

Waziri Nape: Sikupinga vita dhidi ya biashara ya dawa za kulevya bali nilishauri busara itumike

Picha
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye ametoa ufafanuzi juu ya kauli iliyonukuliwa ikionyesha kuwa alipinga vita dhidi ya dawa za kulevya iliyoanzishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda. Amedai kuwa hakupinga vita hiyo bali alitaka busara itumike kwa washukiwa. Waziri Nape alitoa ufafanuzi huo katika kipindi cha dakika 45 cha ITV, alipoulizwa swali na mtangazaji wa kipindi hicho kutaka kujua kuhusu kauli yake iliyoonesha kupinga utaratibu uliotumika wa kuwakamata au kuwapata watuhumiwa wa dawa za kulevya. “Niseme kwanza ilitokea nilikuwa na mkutano na waandishi wa habari, ukienda leo ukanitaja Nape ukaniambia baada ya siku mbili njoo kituoni, hata kama nilikuwa na madawa ya kulevya nyumbani kwangu hivi unayakutaje?  'Kwasababu kwa vyovyote vile nitayachukua, ntayaficha, ntakuja kituoni ntaripoti utanibana ntakwambia twende nyumbani kwangu ukakague mnaenda mnakagua mnakuta hamna, si basi!  "Kwahiyo nikawa na wasiwasi kwamba inawezekan...

Hii Ndiyo Namna Mourinho alivyofanikiwa kuibadili klabu ya Manchester United.

Picha
Wakati  Jose Mourinho  anaanza kazi ya ukocha na klabu ya  Manchester United kuliibuka maswali mengi kuhusiana na namna alivyokuwa anaendesha klabu. Ilikuwa wakati mgumu hasa wengi wakirejesha kumbukumbu za matokeo yake akiwa na klabu ya Chelsea na namna alivyoondolewa klabuni hapo. Sir Alex Ferguson aliwahi kuwaeleza wafanyakazi wenzie kuwa alifikiri siku zote kuwa Mourinho alikuwa kocha ambaye klabu yenye chapa kama ya Manchester United walikuwa wanahitaji kuwa naye. Aliwahi kunukuliwa akisema “tulimhitaji kipindi kirefu miaka kadhaa iliyopita.” Kinachovutia kwa sasa kwa Mourinho ni mbinu alizochukua katika kuimarisha klabu hiyo. Ferguson anakiri kufurahishwa na  namna ambayo Mourinho kajitahidi kubadili viwango vya wachezaji mmoja mmoja kuanzia kwenye viwanja vya mazoezi na uchaguzi wa timu. Lakini pia Mourinho kabadili mengi pale Carrington ambayo hayakufanyika mwanzo. ‘Kuanzia kwa mapokezi mpaka kwa wapishi, wengi ni walewale,’ lakin...

Kama sio wanangu na Mourinho nisingekua Manchester United.-Ibrahimovich

Manchester United wameweka kombe la kwanza kabatini kwao baada ya kuchukua kombe la EFL.Shukrani zimuendee mshambuliaji wao Zlatan Ibrahimovich aliyefunga magoli mawili kati ya matatu yaliyoipa ubingwa huo Manchester United.Ushindi huo wa Manchester United dhidi ya Southampton umewafanya United kuwa na jumla ya makombe 42 na kuipita Liverpool kwa idadi moja la kombe. Ushindi huo umeifanya Man United kuwa timu yenye mafanikio zaidi kwa sasa.Baada ya mchezo huu mshambuliaji huyo wa zamani wa PSG alieleza mambo mengi ikiwemo suala la usajili wake na vile vile mafanikio aliyowapa United hadi sasa.Toka amekuja Man United Zlatan amekuwa kinara wa ufungaji akiwa amewapa United ngao ya hisani na kombe hilo la EFL. Zlatan amesema mwanzoni hakuwa na uhakika kama atatua Man United.Zlatan amesema watoto wake walikuwa wanaizungumzia sana timu hiyo lakini pia simu ya kocha Jose Mourinho ilimshawishi kujiunga Man United.”Akili yangu haikuwa hapa lakink wanangu walianza kusukuma kuhusu hili,uhu...

Wasanii Bongo Movies Wampinga Wema Sepetu, Wakanusha Kuidai CCM

Picha
MOVIE BADO INAENDELEA: Hivyo ndivyo tunaweza kusema baada ya wasanii wa Bongo Movie Wasanii wa Bongo Movies waliokuwa wakishiriki kwenye kampeni ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 ya Mama Ongea na Mwanao ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kukanusha taarifa iliyotolewa na Wema Sepetu kuwa CCM haijawalipwa pesa za kampeni walizofanya kwenye uchaguzi huo. Mara baada ya Thea na Yobnesh kuzungumza maneno machache, mkutano huo na waandishi wa habari ulimalizika, ukiwa umechukua dakika chache tu na kuacha kila mtu akaizungumza lake. “Ni kweli inasemekana kwenye mitandao kuwa tulifanya kampeni na hatukulipwa, mimi kama Mwenyekiti Msaidizi wa Muda, nakanusha taarifa hizo kuwa si za kweli… wapo wanaoshawishiwa kulichafua kundi letu, kumchafua Makamu wa Rais Bi. Samia Suluhu na kuichafua CCM, mimi nakataa, sote tumelipwa na mikataba ipo. “Zipo simu za kushwishiwa kuhama lakini hatutohama chama na Kundi la Mama Ongea na Mwanao litaendelea kuwepo chini ya Usimamizi wa Bi. Samia Suluhu....

Rais amfuta kazi Mkuu wa majeshi Gambia

Picha
Rais wa Gambia Adama Barrow amemfuta kazi mkuu wa majeshi Jenerali Ousman Badjie. Jenerali Badjie alitangaza utiifu wake kwa rais aliyeondoka madarakani Yahya Jammeh baada ya uchaguzi wa Disemba ulioleta vuta nikuvute. Hata hivyo, chini ya amri yake, jeshi halikutoa msaada wowote pindi vikosi kutoka nchi za Afrika Magharibi vilipoingia nchini Gambia mwezi jana. Vikosi hivyo vilifanikiwa katika kumshawishi bwana Jammeh kukubali kushindwa na kuondoka nchini.

Messi na Neymar kuikosa UEFA

Picha
Nyota wa Barcelona Lionel Messi na Neymar wanaweza kunyimwa nafasi ya kuingia Uingereza iwapo watafuzu kuingia kwenye hatua inayofuata na kufuzu fainali kutokana na kesi zinazoendelea za makosa ya ukwepaji kodi. Rais wa UEFA, Aleksander Ceferin amesema kuwa anahofia wachezaji hao wanaweza wasiweze kuingia Cardiff ambapo mchezo wa fainali wa UEFA mwaka huu utafanyika kwenye uwanja wa  Principality Stadium mwezi Juni iwapo tu watafanikiwa kufuzu. Hata hivyo itakuwa kama maajabu Barcelona kuingia kwenye fainali ya mwaka huu ya mwezi Juni kwani tayari wameshafungwa mabao  4-0 kwenye mchezo wa kwanza wa raundi ya 16 dhidi ya Paris Saint-Germain. Mapema msimu huu, beki wa PSG, Serge Aurier alinyimwa ruhusa ya kuingia Uingereza kwenye mchezo dhidi ya Arsenal kwenye uwanja wa Emirates mwezi Novemba kutokana na kuwepo kwenye rufani ya kesi ya kudhuru. Lakini pia hali ya kisiasa inayohusu mpango wa Brexit ikiendelea kuwepo, Ceferin anaamini kuwa England itakumbana na tatizo kubwa k...

Uwanja wa Namfua wakataliwa rasmi na TFF

Picha
SHIRIKISHO la Soka nchini (TFF) limesema Uwanja wa kumbukumbu ya Namfua ulioko mkoani hapa hauna vigezo vya kutumika katika mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara. Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF, Salum Madadi, alitoa kauli hiyo juzi alipokuwa akiukagua uwanja huo kwa lengo la kutoa maelekezo ya marekebisho yanayotakiwa kufanyika ili timu ya Singida United iliyopanda daraja iweze kuutumia. Madadi alisema ili uwanja huo uweze kutumika katika ligi hiyo ya juu nchini, itawalazimu wamiliki kuchukua vipimo upya na ushauri wa kiufundi wa matengenezo yanayohitajika ili wafanye ukarabati na kufikia viwango. “Lakini kubwa zaidi sehemu yenyewe ya kuchezea inahitaji kuboreshwa haraka na kuwekwa uzio kwa ndani, pia kuna haja ya kuwa na vyumba vya kubadilishia,” alisema Madadi. Katibu Msaidizi wa CCM Singida, Adamu Makulilo, alisema kuwa anaamini kwa kuunganisha nguvu za wadau wa soka mkoani hapa watakamilisha matengenezo yaliyoelezwa na hatimaye Singida United ikautumia katika mechi zake za n...

Uamuzi wa pingamizi la Mwenyekiti UVCCM Machi 3

Picha
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Arusha, Machi 3 itatoa uamuzi mdogo wa pingamizi la kuendelea kwa kesi inayomkabili Mwenyekiti wa UVCCM, Mkoa wa Arusha, aliyesimamishwa uongozi, Lengai ole Sabaya. Kesi hiyo ni ya kujipatia huduma ya chakula na malazi kwa njia ya udanganyifu kwenye Hoteli ya Sky Way jijini Arusha, kisha kujifanya ni ofisa usalama wa taifa. Uamuzi huo utatolewa na Hakimu Gwantwa Mwankunga, Machi 3 mwaka huu kuhusu pingamizi lililowekwa na wakili wa utetezi, Edna Haraka. Awali shahidi wa kwanza, askari polisi namba F 1093, Sajenti Elia aliiambia mahakama kuwa Agosti 28, mwaka 2016 aliandika maelezo ya mshitakiwa kwa maelekezo ya mkuu wa upelelezi mkoa na kisha kumsomea maelezo hayo mshitakiwa ambaye aliyakubali na wote walisaini. Shahidi huyo alipewa kuyasoma upya maelezo hayo mbele ya mahakama ambayo yanamuelezea mshitakiwa kujifanya ofisa usalama wa taifa, kujipatia huduma ya chakula na malazi kwa njia ya udanganyifu katika hoteli ya Sky Way ya jijini Arusha, bila ya kulip...

Mwanamuziki Timbulo Aiponda Label ya QS Mhonda...Adai Haijui Muziki ndio Imempotezea Muda Q Chief

Picha
Timbulo amedai kuwa licha ya wimbo wake hivi karibuni kuvuja ikiwa na ID ya label ya QS Mhonda, haimaanishi kuwa amesainishwa na label hiyo. Akiongea na Pride FM, Timbulo amedai kuwa wimbo huo ulirekodiwa kipindi ambacho walikuwa na makubaliano ya kufanya kazi pamoja na sio kusainishwa. “Siwezi kusaini na QS, sio label ya muziki ambayo mimi naiona inaweza kukuza muziki wangu,” Timbulo alimuambia mtangazaji wa redio hiyo, Eddy Msafi. “Sio label ya muziki Tanzania ambayo inafanya hata muziki ambao unatakiwa Tanzania. Hawajui chochote kuhusu muziki, hiyo ni label ambayo labda wangekuwa wanafanya vitu vingine kama masuala ya ujenzi na vitu vingine kibao ambavyo mkurugenzi amesomea,” amesisitiza. Hivi karibuni label hiyo ya QS Mhonda imeingia kwenye headlines kutokana na kuwa na ugomvi na Q-Chief aliyekuwa amesainishwa mkataba wa maisha. Chief amepigana hadi amefanikiwa kujitoa kwenye label hiyo kwa madai kuwa haikuwa ikimsaidia kwa lolote. Yenyewe ilidai kuwa im...

Yasome hapa magazeti ya leo Februari 28, 2017

Picha

Mwanaume Aliyefanya Mapenzi na Maiti ya Mtoto wake Auawa

Picha
Mwanaume mwenye umri wa miaka 45 kutoka Kenya amepigwa na Wananchi baada ya kufumaniwa akifanya mapenzi na maiti ya Mtoto wake aliyekuwa na umri wa miaka 15 ambapo ripoti ya K24 TV imeripoti tukio hilo kutokea kwenye kijiji cha Kiwanja Ndege  kaunti ndogo ya Kuresoi Kaskazini. Mashaidi wanasema baada ya mtoto kufariki kutokana na uvimbe wa Ubongo kichwani walihifadhi mwili kwenye chumba cha pekee lakini mida ya SAA nane usiku baba wa mtoto huyo aliamka na kwenda katika chumba hicho na ndipo alipokutwa akiwa anafanya mapenzi na maiti hiyo kitendo ambacho kiliwakasirisha wananchi na kuanza kumpiga hadi kupelekea kifo chako

Mwenyekiti wa Chadema Mbowe Aifagilia Mahakama Arusha

Picha
Chama cha Demokrasia na Maendeleo kimeeleza kusikitishwa kwake na kitendo cha Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema kunyimwa dhamana na kukaa gerezani kwa zaidi ya miezi mine sasa. Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe akiwa nje ya mahakama mjini Arusha baada ya mahakama ya rufaa kufuta rufaa za upande wa Jamhuri, amesema kitendo hicho kiliwafanya waichukie mahakama kuona inapewa maelekezo na serikali, kumbe siyo kweli bali ni mchezo mchafu wa ofisi ya DPP. “Leo mahakama imetufariji sana na kuturudishia imani yetu kwao kuwa ni chombo kilichosimama kwa miguu yake kama Mhimili wake na haipokei maagizo ya serikali” Amesema Mbowe.  Amesema sakata hilo linawasababisha kupeleka hoja katika bunge lijalo kuwa waangalie wafungwa na mahabusu walio mo ndani, kwani siyo wote waliokaa kwa sababu za kuhusika na makosa, bali wanaonewa. Aidha amewapongeza majaji kwa kuitaka ofisi ya DPP kushikilia watu kwa misingi ya sheria na badala ya kuitia najisi mhimili huo kwa sababu ya mic...

Mwanariadha wa Kenya Afariki Dunia Akimalizia Mbio za Kilimanjaro Marathon

Picha
Mwanariadha Mkenya, Charles Maroa(36) amefariki dunia baada ya kuanguka ghafla baada ya kumaliza mbio katika Mashindano ya riadha ya Kilimanjaro Marathon yaliyofanyika Jumapili tarehe 26 Februari.  Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Wilbroad Mutafungwa amesema mwanariadha huyo alipewa msaada wa kufikishwa Hospitali ya KCMC. Mkenya huyo aliyekuwa akishiriki mbio za Kilomita 21 aliwahishwa Hospitali ya KCMC lakini alipofikishwa madaktari walibaini kuwa alishafariki.

Manara ame-post Instagram kuhusu Kessy kukaa benchi Yanga

Picha
Afisa habari wa habari wa klabu ya Simba Haji Manara ame-post kwenye ukurasa wake wa Instagram kuhusu mchezaji wao wa zamani Hassan Ramadhani Kessy na hali anayopitia kwenye klabu yake mpya ya Yanga. Manara ameandika ujumbe unaosomeka: “Unakumbuka yale maneno ya aliotudhalilisha huyo dogo? Mwambieni this is Simba na benchi ndio makazi yako ya kudumu.” Kessy aliondoka Simba mwishoni mwa msimu uliopita huku usajili wake ukizua utata mkubwa kati ya vilabu hivyo viwili vyenye nguvu kwenye soka la Bongo. Simba wanalalamika kwamba, Yanga ilimsajili Kessy akiwa bado anamkataba na Simba hali iliyopelekea kufungua kesi TFF ambao baadae Yanga ilitakiwa kuilipa Simba zaidi ya milioni 50 baada ya kubainika kuvunja kanuni za usajili wakati wa kumsajili mlinzi huyo wa kulia. Tangu Kessy ajiunge na Yanga ameshindwa kupata nafasi ya kudumu kwenye kikosi cha kwanza cha Yanga kwa kumtoa Juma Abdul kwenye nafasi yake.

Wafanyakazi wengine Wawili wa Quality Group ya Yusuf Manji Wafikishwa kizimbani

Picha
Wafanyakazi wengine wawili wa Kampuni ya Quality Group inayomilikiwa na Yusuf Manji ambao ni raia wa India wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam wakikabiliwa na mashitaka ya kuzuia maofisa wa Uhamiaji kutimiza majukumu yao. Washitakiwa hao ni Jose Kiran (40) ambaye ni Meneja Miradi wa kampuni na Prakash Bhatt (35) ambaye ni Katibu Muhtasi wa kampuni hiyo ambao wameongezwa katika kesi inayowakabili wafanyakazi 14 wa kampuni hiyo, raia wa India wanaokabiliwa na mashitaka matatu likiwamo la kughushi viza ya biashara. Wakili wa Serikali, Method Kagoma alidai mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha kuwa washitakiwa hao walitenda kosa hilo kinyume cha Kifungu Namba 30 (1) (f) na Kifungu Namba 2 cha Sheria ya Uhamiaji ya Mwaka 2002 iliyofanyiwa marekebisho na Sheria Namba 8 ya Mwaka 2015. Kagoma alidai washitakiwa hao wawili, Februari 20 mwaka huu katika Kampuni ya Quality Group waliwazuia maofisa Uhamiaji kutimiza majukumu yao baada ya kukata...