BUNDA. Mahakama ya wilaya ya Bunda, jana desemba 27 2017 imemuhukumu kifungo cha miaka 30
BUNDA.
Mahakama ya wilaya ya Bunda, jana desemba 27 2017 imemuhukumu kifungo cha miaka 30 jela Baraka saimon 24 mkazi wa kijiji cha Muranda kata ya Namuhura kwa kosa la kubaka na kumpa mimba mwanafunzi mwenye umri wa miaka 16 .
Akisoma shtaka mbele ya hakimu mkaazi wa mahakama ya wilaya ya bunda Jacklin J. Rugemalira , mwendesha mashtaka upande wa jamhuri inspecta Masoud ameeleza mahakama kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo mnamo tarehe 19.oktoba.2017 saa za jioni.
Aidha amesema kuwa majira hayo mtuhumiwa alimbaka msachana huyo mwenye miaka 16 anaesoma katika shule moja ya sekondari.
Hata hivyo alipoulizwa kuhusu makosa hayo mshtakiwa amekiri kutenda kosa hilo na ndipo mheshimiwa hakimu amemhukumu kifungo hicho cha miaka 30 jela.
Maoni
Chapisha Maoni