Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari, 2018

Rais Magufuli Atoa Maagizo Mazito kwa Kamishina wq Uhamiaji

Picha
 Rais John Magufuli ameitaka Idara ya Uhamiaji kuhakikisha inapambana na wahamiaji haramu pasipo kumwogopa mtu. Amemwagiza Kamishna wa Uhamiaji, Dk Anna Makakala kuwachukulia hatua kali watumishi wake watakaoshindwa kutekeleza wajibu wao ipasavyo. Dk Magufuli akizungumza leo Jumatano Januari 31,2018 akizindua hati ya kusafiria ya kielektroniki jijini Dar es Salaam, amesema utambuzi wa wananchi wanaoishi bila vibali na wenye vibali vilivyoisha ni muhimu. Amesema uhamiaji ina jukumu kubwa katika kutekeleza hayo. "Haiwezekani wahamiaji haramu wanakamatwa Mbeya halafu wamepita Kilimanjaro, Manyara. Kamishna (Dk Makakala) ifike mahali unapoona hili washushe vyeo, mwondoe nyota moja ili wajue wajibu wao," ameagiza Rais Magufuli. Amesema awali Uhamiaji iligubikwa na matatizo yakiwamo ya utoaji hovyo wa vibali vya uraia, hata kwa watu ambao walikuwa hawana sifa. "Kuna raia wengi walipata uraia bila sifa na wapo waliopata uraia na vyeo vya juu kabisa serikalini wakati  si ...

Serikali ya Kenya Yapiga Marufuku Kundi la NRM la Raila Odinga..Lawekwa Kundi Moja na Al Qaeda

Picha
KENYA: Serikali kupitia Waziri wa Usalama, Dkt Fred Matiang’i amepiga marufuku kundi la na National Resistance Movement (NRM) lililopo chini ya Muungano wa Upinzani (NASA) - Kundi hilo liliundwa baada ya Raila Odinga kususia uchaguzi wa marudio na limekuwa katika harakati za kuipinga Serikali na kuhimiza watu kususia bidhaa za makampuni ambayo yanadaiwa kuwa upande wa Serikali - Waziri huyo wa Usalama ameliweka kundi la NRM kwenye orodha moja na makundi ya kigaidi kama Al Shabaab na Al Qaeda

Wanasheria Wamuunga Mkono Makonda Kuwasaidia Waliodhulumiwa Mali Zao

Picha
Dhamira njema ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda kuamua kuwasaidia wanyonge walioteseka na kunyanyasika muda mrefu baada ya kudhulumiwa Mali zao walizochuma kwa Jasho imewafanya Wanasheria kuguswa na kuamua kujitokeza kusaidia jitiada hizo ili kuhakikisha haki ya mnyonge inapatikana pasipo kuvunja Sheria. Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akizungumza na wananchi hao. RC Makonda amesema idadi ya Wanasheria imeongezeka kutoka 160 hadi kufikia 246 siku ya leo ambapo ameshukuru Uongozi wa Shule ya Wanasheria kwa Vitendo (Law school), Mawakili wa kujitegemea pamoja na Chama cha Mawakili (TLS) kwa kumuunga mkono na kuwaomba wanasheria wengine kujitokeza kuwasaidia wananchi. Aidha RC Makonda ameshukuru jopo la wanasheria wanaohudumu kwenye Zoezi hilo kwa umakini na huduma nzuri wanayotoa kwa wananchi waliojitokeza kitendo kinachowapa faraja wananchi ambao wametaabika kwa miaka mingi kutafuta haki yao. RC Makonda amesema lengo lake ni kuhakikisha kila mwananchi a...

Mess Ampa Ahadi David Beckham

Picha
Baada ya nyota wa zamani wa Manchester United na Real Madrid David Beckham kutangaza kuwa yupo mbioni kuanzisha klabu ya soka, nyota wa Barcelona Lionel Messi amempongeza. Messi ametoa pongezi hizo kupitia video fupi ambapo pia amemwambia Beckham kuwa huenda miaka michche ijayo akaungana naye kuchezea klabu hiyo. ''Kwanza nikupongeze sana kwa hatua hiyo mpya unayoianzisha, naamini kila kitu kitakwenda sawa, na huwezi jua miaka michache ijayo naweza kupokea simu kwaajili ya kuchezea klabu hiyo'', ameeleza Messi katika video hiyo. Hivi karibuni nyota huyo aliyekipiga na vilabu kadhaa ikiwemo AC Milan na PSG ameweka wazi kuwa tayari wazo lake la kuanzisha timu itakayoshiriki ligi kuu ya Marekani (MLS) ameshaanza kulifanyia kazi na makao makuu ya timu hiyo yatakuwa jijini Miami. David Beckham ambaye ni raia wa Uingereza alicheza kwa mafanikio katika soka ngazi ya klabu kabla ya mwaka 2007 kutimkia nchini Marekani kwenye klabu ya LA Galaxy.

Familia ya Lissu Imelitaka Bunge Kutoa Fedha za Matibabu ya Lissu

Picha
FAMILIA ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema), imelitaka Bunge kutoa fedha za matibabu yake kama halitaki mtunga sheria wake huyo akafukuzwe hospitalini alikolazwa. Lissu amelazwa katika Hospitali ya Chuo Kikuu cha Luvein nchini Ubelgiji tangu mapema mwezi huu baada ya kutibiwa Hospitali ya Nairobi nchini Kenya kwa miezi minne. Msemaji wa familia ya Lissu, wakili Alute Mughwai, aliwaeleza waandishi wa habari ofisini kwake jana kuwa miezi ni mitano sasa Lissu hajapata stahiki zake kimatibabu kama Mbunge. “Tumemaliza miezi mitano tangu kutokea kwa tukio la kushambuliwa kwa Lissu na Bunge kama taasisi limeshindwa kutoa fedha za matibabu kwa mwenzao," alisema Mughwai. “Sasa Lissu atalaumiwaje? Akilia Mungu wangu mbona umeniacha, Bunge langu mbona limeniacha... au wanataka afukuzwe hapo hospitalini kwa kukosa fedha za matibabu? “Mpaka sasa hatujui kinachoendelea. Tunaweza kusema ni siasa au kwa namna nyingine tunaweza kutafsiri kuwa sababu Lissu ni mko...

Ifahamu orodha ya viongozi waliowahi kujiapisha kuwa marais kama alivyofanya Raila Odinga

Picha
Kiongozi wa Muungano wa Upinzani nchini Kenya (NASA), Raila Odinga, jana Jumanne, Januari 30, aliapishwa kuwa ‘rais wa wananchi’ nchini humo, baada ya kusema hatambui ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta katika uchaguzi wa marudio uliofanyika Oktoba mwaka jana. Mgombea mwenza wake Kalonzo Musyoka wa chama cha Wiper hakujitokeza katika sherehe hiyo ya kuapishwa, ingawa alikuwa miongoni mwa watu waliotarajiwa kuapishwa. Raila Odinga alitangaza kuwa Kalonzo Musyoka ataapishwa baadaye. Hili siyo tukio la kwanza la baadhi ya watu kutangaza kujiapisha kama marais w nchi zao barani Afrika na ulimwenguni kwa ujumla. Wapo viongozi wengi, hasa wa vyama vya upinzania ambao wamekuwa wakitangaza kujiapisha, kutokana na kutokubaliana na ushindi wa kiongozi aliyeo madarakani. Mfano viongozi wa nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo – Etienne Tshisekedi, Nigeria – Moshod Abiola, Uganda – Kiza Besigye na Jean Ping wa Gabon ni miongoni mwa viongozi wa upinzani wa Afrika amba...

Raila Odinga hatarini kushtakiwa kwa uhaini

Picha
MAMLAKA za Kenya, jana zilizima vituo vya televisheni kuzuia matangazo 'live' ya sherehe za kuapishwa kwa kiongozi wa upinzani, Raila Odinga, ambaye alisusia uchaguzi wa marudio wa mwaka jana uliobishaniwa. Alijitangaza kuwa "rais wa watu" mbele ya maelfu ya wafuasi wake katika mji mkuu wa Nairobi. Matokeo ya uchaguzi mkuu wa Agosti, mwaka jana, yalibatilishwa kutokana na  madai ya ukiukwaji wa kanuni. Uhuru Kenyatta alishinda uchaguzi wa marudio Oktoba, lakini Odinga hakushiriki, hivyo Kenyatta aliapishwa kuongoza muhula wa pili Novemba, mwaka jana. Alivionya vyombo vya habari kutotangaza shughuli ya jana na mwanasheria wa serikali alisema kufanya hafla hiyo ni kosa la uhaini. Hata hivyo, vituo vikuu vya TV vilionyesha tukio hilo kupitia mitandao yake ya kompyuta, kwenye YouTube na Facebook. Akiwa ameshika Biblia mkono wake wa kulia katika bustani ya jijini Nairobi, Odinga alitangaza kuwa anajibu "wito wa ngazi ya juu kuchukua ofisi ya rais wa watu wa Jam...

Malisa GJ: Raila Odinga ni 'JASIRI', Uhuru Kenyatta ni 'MSHINDI'

Picha
Kuna mambo mawili ya kujifunza Kenya. #Mosi; ni kuhusu Raila Odinga. Amekuwa jasiri, na mwenye msimamo thabiti wa kusimamia kile anachoamini hadi dakika ya mwisho. Ameongoza maelfu ya watu wake katika kuhitimisha safari ya "Kaanani". Kwenye kampeni aliwaambia wananchi wake atashinda, matokeo yalipotangazwa hakukubaliana nayo. Akawaaongoza watu wake kuyakataa. Na leo ameungana nao kujiapisha. Bila kujali vitisho kutoka vyombo vya dola, bila kujali kuwa anaweza kushtakiwa kwa "uhaini" lakini amejivika ujasiri. Hili ni funzo kwa viongozi wengi wa vyama vya siasa barani Afrika. Sio unawaambia watu "pigeni kura matokeo niachieni mimi" lakini siku ya matokeo unajifungia ndani, halafu baada ya miaka miwili unaenda kupongeza juhudi. If people grant their trust on u, please learn to fight your battle to the last. #Pili; ni kuhusu Rais Uhuru Kenyatta. Huyu ni kielelezo cha kiongozi wa mfano bora kabisa wa demokrasia duniani. Ameonesha "political maturity...

Umri wa Kustaafu Kwa Madaktari Bingwa, Wahadhiri Waandamizi na Maprofesa Sasa miaka 65

Picha
Frank Mvungi- Maelezo, Dodoma. Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepitisha muswaada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali ikiwemo sheria ya Utumishi wa Umma, Sura ya 298  (The Public Service Act) itakayowezesha muda wa kustaafu kwa  Wahadhiri waandamizi, Maprofesa na Madaktari Bingwa kuwa miaka 60 kwa hiari na lazima miaka 65. Akizungumza wakati akiwasilisha muswaada huo  Mwanasheria  Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju amesema kuwa marekebisho katika jedwali yanapendekeza kuongezwa kwa kifungu kipya cha 25A ambacho kinaainisha kuhusu umri wa kustaafu ambapo kwa sasa sheria ilivyo  haina masharti hayo isipokuwa umri wa kustaafu umetajwa katika sheria zinazoanzisha mifuko ya hifadhi za jamii. Aliongeza kuwa, uzoefu umeonyesha kuwamba Maprofesa na Wahadhiri waandamizi wa vyuo  Vikuu  vya Umma pamoja na madaktari Bingwa wa Binadamu wa Hospitali za Umma wamekuwa wakihitajika kuendelea kutoa huduma, utaalamu na uzoefu wao licha yakufiki...

Shamsa Ford Apigwa Marufuku Kutumia Mitandao na Mumewe Baada ya Kuambulia Matusi

Picha
STAA wa filamu za Kibongo, Shamsa Ford anadaiwa kupigwa stop kutumia mitandao ya kijamii na mumewe, Chid Mapenzi na kwa muda sasa haonekani hasa kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram ambako aliwaaga kabisa mashabiki zake.  Chanzo kilieleza kwamba Chid Mapenzi alimpiga marufuku mkewe Shamsa kutumia mitandao ya kijamii kwa kuwa muda mwingi alikuwa akiutumia kwenye mitandao hiyo huku wakati mwingine akiambulia matusi kutoka kwa mashabiki zake jambo ambalo lilimchefua mumewe huyo na kuamua kumkataza. Alipoulizwa Shamsa kuhusiana na suala hilo alikiri kwamba ni kweli mumewe alimtaka atoke kwenye mitandao ya kijamii kwa muda mpaka atakapomruhusu tena na hajui sababu za kukatazwa.  “Kwa sasa naishi kwa amani sana maana nimepumzika na matusi ya mitandaoni siyaoni tena, sijui mume wangu aliona nini ila aliniambia nitoke mpaka atakaponiruhusu tena ndiyo nitarudi,” alisema Shamsa.

Rais Magufuli Kuzindua Pasipoti ya Kielektroniki

Picha
Jonas Kamaleki- MAELEZO Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. John Pombe Magufuli leo  atazindua Pasipoti Mpya ya Tanzania ya kielektroniki jijini Dar es Salaam. Uzinduzi huo utafanyika Jumatano, Januari 31, 2018 kuanzia saa moja na nusu asubuhi, Makao Makuu ya Idara ya Uhamiaji, Kurasini Dar es salaam. Hayo yalisemwa na Mrakibu wa Uhamiaji ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji, Ali Mtanda katika mahojiano maalum na Idara ya Habari (MAELEZO). Mtanda alisema kuwa Pasipoti Mpya ya Tanzania ya kielektroniki ni sehemu ya Mfumo wa Uhamiaji Mtandao ambao utakuwa na visa, vibali mbali mbali na manejimenti mipakani. Kwa kuwa teknolojia inazidi kukua, Tanzania haiwezi kubaki nyuma ndiyo maana imeamua kuingia katika masuala ya digiti. Uzinduzi huu utahudhuriwa pia na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohamed Shein. Marais wastaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, waheshimiwa, Ali Hassan Mwinyi, Benjamin William Mkapa na Jakaya Mrisho ...

Wanne wafariki kwa kufukiwa na kifusi Arusha

Picha
 Wachimbaji wanne wamefariki na  mmoja yupo mahututi baada ya kuangukiwa na Ngema  walipokuwa wakipakiza  changarawe kwenye gari katika machimbo ya changarawe yaliyopo katika mlima Murieti katika jiji la Arusha. Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo amethibitisha jana Januari 30 kuhusu  kutokea tukio hilo  mchana, katika eneo ambalo ni machimbo ya muda mrefu ya changarawe. Miili ya watu watatu tayari imetambulika ambao ni Yusuph Mohamed Kamwende(35) Athuman Hussein  umri wake haujatambulika na Richard Kishimbo(57). "Bado  mwili wa marehemu mmoja haijafahamika na tunaomba watu kufika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya mkoa Mount Meru kutambua ndugu zao" alisema  Kamanda. Hata hivyo, alitoa  wito kwa maafisa madini kwenda mara kwa mara kwenye maeneo ya machimbo ili kutazama usalama wa maeneo hayo ili kuondoa majanga. "Pale inaonekana ngema moja ilikuwa imelegea sasa wao wakiwa wanachimba changarawe ndipo iliwad...

Serikali Yasisitiza Uwazi Shughuli Za Madini

Picha
Kampuni za Madini nchini zimetakiwa kufanya shughuli zake kwa uwazi sambamba na kufuata Sheria za nchi ili kuepuka migongano. Wito huo umetolewa jijini Dar es Salaam Januari 29, 2018 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Profesa Simon Msanjila kwenye mkutano na Balozi wa Canada nchini, Ian Myles aliyeambatana na Mshauri masuala ya Uwajibikaji kwa Jamii kwenye Tasnia ya Uziduaji kutoka Serikali ya Canada, Jeffrey Davidson. Ujumbe huo ulimtembelea Katibu Mkuu Msanjila kwa lengo la kujadiliana masuala mbalimbali kwenye Sekta ya Madini ikiwemo suala la Sheria ya Madini, masuala ya uwajibikaji kwa jamii (CSR) yanayofanywa na kampuni mbalimbali zikiwemo za kutoka nchini Canada na matarajio ya Serikali kwa kampuni (wawekezaji). Profesa Msanjila alisisitiza kuwa kampuni zinazofanya shughuli zake nchini zinalazimika kufuata taratibu na sheria za nchi ili kujijengea mazingira rafiki ya utekelezaji wa shughuli husika. Alisema lengo la Serikali ni kuhakikisha Sekta ya Madini inanufaisha Taifa k...

Watuhumiwa Waliovua Nguo Mahakamani Wafungwa Miezi Sita

Picha
Watuhumiwa 24 kati ya 61 wanaokabiliwa na kesi za ugaidi jijini hapa wamehukumiwa kifungo cha miezi sita jela  kwa kosa la kuvua nguo na kisha kugoma kuingia ndani ya chumba cha mahakama kusikiliza kesi zinazowakabili. Hukumu hiyo imetolewa leo Januari 30   katika mahakama ya hakimu mkazi Arusha na hakimu mkazi wa mahakama hiyo, Nestory Baro ambapo amesema kwamba watu hao wamehukumiwa kwa mujibu wa kifungu nambari 114 (a) cha mwongozo wa mashtaka ya jinai. Hata hivyo, baada ya hukumu hiyo baadhi ya watuhumiwa  wamevua  nguo zao na kubakisha  nguo zao za ndani wakati wakipandishwa kwenye karandinga  wakati wakirejeshwa katika gereza kuu la mkoa wa Arusha. Awali kabla ya kusoma hukumu hiyo mwendesha mashtaka wa Serikali ,Augustino Kombe ameiomba mahakama hiyo iwachukulie hatua kali na kutoa adhabu kwa watuhumiwa wa kesi hizo wanaogoma mahakamani. Mara baada ya kauli hiyo ndipo Hakimu Baro akasema kwamba anatoa kifungo cha miezi sita kwa watuhumiwa h...

Serikali: Hatuna Mpango Kurejesha Fedha za Sarafu

Picha
Serikali ya Tanzania imesema haina mpango wa kurejesha fedha za sarafu ndogo kuanzia senti tano hadi shilingi 20 katika mzunguko wa fedha kutokana na ubebaji wake kuwa mgumu. Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashantu Kijaji kwa niaba ya Waziri wa Wizara hiyo, leo Bungeni mjini Dodoma (Jumanne) katika mkutano wa 10 wa Bunge kwenye kikao chake cha kwanza wakati akijibu swali la mbunge wa viti maalum, Mhe. Salma Kikwete ambaye alitaka kujua ni kwa nini serikali haioni kuwa ni wakati muafaka kurudisha sarafu hizo katika mzunguko wa matumizi kutokana na kuwapo na bei za shilingi zinazohitajika kuwapo na senti. "Benki kuu ya Tanzania imepewa kisheria jukumu la kuzalisha fedha za noti sarafu kulingana na mahitaji pamoja na mazingira ya kiuchumi yaliyopo. Mambo muhimu ambayo yanazingatiwa wakati wa kuondoa na kuingiza katika soko noti na sarafu ya thamani ndogo na kubwa ni mfumuko wa bei wa bidhaa za huduma, kulinda thamani na wepesi wa sarafu kubebeka", al...

Raila Odinga Ajiapisha Kuwa ‘Rais wa Wananchi wa Kenya

Picha
Kiongozi  wa upinzani Raila Odinga (NASA) ameapishwa kuwa ‘Rais wa Wananchi’ wa Kenya licha ya kugomea uchaguzi mkuu wa marudio nchini humo. Raila Odinga amefika  leo katika Uwanja wa Uhuru Park pamoja na viongozi wengine wakuu wa NASA akiwemo Moses Wetangula na Musalia Mudavadi na kujiapisha akishika Biblia. Aidha, mgombea mwenza wake Kalonzo Musyoka wa Chama Cha Wiper hakuwepo wakati wa kuapishwa kutokana na kuhofia kukamatwa, ambapo Odinga amesema ataapishwa baadaye. “Odinga amesema leo ni siku ya kihistoria kwa Kenya, hatua ya leo ni kuelekea kutoa udikteta na kuleta demokrasia Kenya, maelekezo mengine mtayapata baadae,”  alisema Odinga baada ya kuapishwa. Awali Raila Odinga aliiambia kituo cha habari cha KTN kwamba shughuli hio ‘ si mapinduzi ya serikali’ Raila aligomea uchaguzi huo kwa sababu za kusema kuwa tume ya Uchaguzi nchini humo si ya Uhuru na haki. Uchaguzi huo wa marudio ulikuja baada ya Mahakama ikiongozwa na Jaji M...

Odinga: Tunachokifanya si Mapinduzi ya Serikali

Picha
Bw Raila Odinga amezungumza na kituo cha habari cha KTN kwa njia ya simu ambapo amesisitiza kwamba Rais Uhuru Kenyatta hakuchaguliwa kwa njia halali. Alipoulizwa anni atamwapisha, amesema: "Ngoja uone” na akasisitiza kwamba wanachokifanya leo kina msingi wake katika sheria na si mapinduzi. “Hatutambui uchaguzi wa Oktoba 26 (uchaguzi wa marudio ambao Odinga alisusia), zaidi ya asilimia 86 ya Wakenya hawakushiriki. Tuna serikali ambayo si halali ambao inajidai kuwa mamlakani,” amesema. Kuhusu taarifa kwamba amepokonywa walinzi, amesema: "Walinzi wangu waliondolewa muda mrefu sana uliopita. Najihisi kuwa hatarini ndio lakini watu raia ndio usalama wangu.” Bw Odinga ameitaka serikali kutotumia nguvu kuusambaratisha mkutano wa leo. "Wafuasi wangu wamo safarini kuelekea Canaan. Safari yetu ni halisi na haiwezi kuzuiwa. Article share tools Sambaza habari hii FacebookSambaza habari hii Twitter

Raila Odinga Ajiapisha kwa Kushika Biblia Kuwa Rais wa Wananchi Kenya

Picha
Raila Odinga amefika katika pamoja na viongozi kadha wakuu wa NASA na kujiapisha akishika Biblia. Amewaambia kuwa mgombea mwenza wake Kalonzo Musyoka wa chama cha Wiper ataapishwa baadaye. Viongozi wengine wenza wa Nasa Moses Wetangula na Musalia Mudavadi pia hawakufika katika wuanja huo. Bw Odinga amesema leo ni siku ya kihistoria kwa Kenya.

Ifahamu gharama inayotumika kubomoa majengo ya TANESCO Ubungo

Zoezi la ubomoaji wa majengo yalipokuwa Makao Makuu ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) bado linaendelea, ili kupisha ujenzi wa barabara za juu (Flyover) katika eneo la makutano ya barabara ya Sam Nujoma na Morogoro, Ubungo. Ubomoaji wa majengo hayo unatarajia kugharimu kiasi cha shilingi milioni 700, kiasi ambacho kimekuwa kikubwa kutokana na uhitaji wa kutumia mashine na vifaa vingine vya kisasa katika ubomoaji, ili kutoathiri majengo mengine yatakayobakia. Eneo linalobomolewa linahusisha jengo la ofisi za Makao Makuu, ofisi za mapokezi, karakana pamoja na uzio wa jengo hilo. Kwa mujibu wa Mtendaji Mkuu wa Uwekezaji wa TANESCO, Khalid James amesema kuwa, zoezi la ubomoaji limechelewa na kuwa la muda mrefu, kwa kuwa unahitajika umakini wa hali ya juu, kutokana na kuwa baadhi ya majengo hayakuathiriwa na agizo la ubomoaji lililotolewa. “Tunabomoa tu baadhi ya majengo, na tunatakiwa kulinda majengo yanayobaki ambayo hayakuathiriwa na agizo la ubomoaji,”  alisema J...

Hofu Yatanda Kenya Mamia ya Watu Wafurika Kushuhudia Kuapishwa kwa Odinga

Picha
Hofu ya kuzuka kwa vurugu nchini Kenya imezidi kutawala wakati mamia ya watu wakifurika katika viwanja vya Uhuru Park kushuhudia tukio la kuapishwa kwa kiongozi mkuu wa upinzani nchini humo, Raila Odinga. NASA wamepanga kumuapisha Raila Odinga kama Rais wa Kenya huku wakidai kuwa ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta mwezi Oktoba 2017 haukuwa wa halali na wa haki hivyo kukataa matokeo hayo. Hata hivyo, Serikali nchini humo imesema haitambui sherehe hizo za kuapishwa kwa Raila Odinga ingawaje imeuruhusu umoja huo kutumia viwanja vya Uhuru

Baada ya Kifungo Kumalizika Mdee, Bulaya Watinga Bungeni

Picha
Kifungo walichokuwa wakitumikia wabunge wa Chadema, Ester Bulaya (Bunda Mjini) na Halima Mdee (Kawe) cha kutohudhuria shughuli za Bunge  kimemelizika na leo Januari 30, mwaka 2018 wamehudhuria kikao cha kwanza kwa Bunge mjini Dodoma. Wabunge hao waliingia katika ukumbi wa Bunge saa 3:28 asubuhi na kushangiliwa kwa makofi, mengi kutoka kwa wabunge wa upinzani huku wabunge wachache wa chama tawala wakitoa kauli za kuwatania. Wabunge hao waliadhibiwa kwa azimio la Bunge Juni 5 mwaka jana kutohudhuria mikutano mitatu ya Bunge ambayo ni jumla ya siku 47, waliyokosa ukiondoa shughuli zote za mikutano ya kamati za Bunge. Adhabu hiyo ilikwenda sanjari na kulipwa nusu mshahara na posho kwa kipindi chote walichotumikia adhabu hiyo wakituhumiwa kudharau kiti cha spika. Mikutano mitatu waliyoikosa ni wa bajeti uliokuwa ukiendelea, wa saba uliofanyika kati ya Septemba 5 hadi 15 na mkutano wa tisa wa Novemba 7 hadi 17.

Maelfu Waliodhulumiwa Wazidi Kumiminika Ofisini kwa RC Makonda

Picha
Zaidi ya wananchi 3000 Jumanne hii wamejitokeza kwa wingi ikiwa ni siku ya pili ya utatuzi wa malalamiko ya kisheria kwa wananchi waliodhulumiwa chini ya wanasheria magwiji 160 ikiwa ni Mkakati wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda kusaidia wanyonge waliodhulumiwa mali zao kupata haki pasipo kuvunja sheria. Wananchi hao wametaabika kwa muda mrefu baada ya kudhulumiwa Mali zao Walizochuma kwa Tabu na sasa kupitia huduma ya Masada wa kisheria uliotangazwa na RC Makonda wanaamni watarejeshewa haki yao. RC Makonda amesema idadi kubwa ya wananchi waliojitokeza leo inatoa picha kamili Kuwa wapo viongozi wasiotekeleza vyema majukumu yao ya kiofisi kwenye idara zao ambapo ameahidi kuwawajibisha. Aidha RC Makonda amesema kilichomgusa kuandaa Wiki ya msaada wa kisheria ni baada kubaini uwepo wa wananchi wanaonyanyasiki na hata kufikia hatua ya kufa kwa presha au kupooza miili baada ya kudhulumiwa na watu wenye pesa au wanaotumia uelewa wa sheria kukandamiza wanyonge. Kutokana n...

Wabunge wa Upinzani Wasusa Kutoa Maoni Yao Bungeni

Picha
Msemaji wa upinzani wa Wizara ya Katiba na Sheria, Ally Salehe amesusa kusoma maoni ya upinzani ya Muswada wa Marekebisho ya Sheria Mbalimbali baada ya Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge kukataa kusomwa kwa baadhi ya maneno yaliyomo katika maoni hayo. Salehe alikuwa akisoma maoni hayo leo Januari 30 mwaka 2018 kwa niaba ya msemaji wa Wizara ya Katiba na Sheria, Tundu Lissu aliyeko nchini Ubelgiji kwa matibabu baada ya kushambuliwa kwa risasi Novemba 7 mwaka jana. Maneno yaliyozuiwa na Chenge kusomwa na upinzani ni kuhusu matukio ya uhalifu nchini, likiwemo la kushambuliwa kwa Lissu. Salehe alianza kusoma maneno hayo lakini alipofika aya ya nne alikatizwa na Chenge akimtaka asubiri, baadaye kumueleza kuwa lugha iliyotumika katika ukurasa kwa kwanza na pili wa hotuba hiyo si ya kibunge. Baada ya kauli hiyo, Salehe amesema upinzani unaiamini na unaisimamia hotuba hiyo kwa kuwa wabunge wote wanayo nakala yake, akaomba kuiwasilisha na kurejea kuketi.

Kampuni za kigeni zina nafasi gani katika kufanya biashara Tanzania?

Picha
Kiwanda cha matairi cha General Tyre Arusha ambacho kilikuwa kinaendeshwa kwa ubia wa serikali na sekta binafsi Katika siku za hizi karibuni naonekana ni vigumu sana kwa wiki moja kupita bila kuwapo taasisi yoyote itakayochapisha ripoti kuhusuTanzania. Wiki iliyopita ilikuwa zamu ya Benki ya Maendeleoya Afrika (AfDB). Katika chapisho lao kuhusu muonekano wa uchumi waTanzania kwa mwaka mmoja, walituambia jambo ambalo tayari limekuwa linasemwa mara nyingi nchini; kwamba uchumi wetu unakua. Aidha, AfDB wametabiri kuwa, kwa mwaka 2018, uchumi wa Tanzania utakua kwa 6.7%. Hii ni habari nzuri. Lakini ndugu zetu wa AfDB wametoa tahadhari moja kwetu; ni tahadhari ambayo nadhani inatupasa kuichukua kwa umakini mkubwa. AfDB walisema, kutokutabirika kwa mazingira ya biashara, kunaweza kuwaondoa wawekezaji katika sekta binafsi. Wanamaanisha nini? Wanaamini kwamba, wawekezaji hasa kutoka ughaibuni wanaokuja kuwekeza Tanzania wana wasiwasi kuhusu masuala ya sera, sheria na rushwa nchini. Natuku...

Wabunge wapya wala kiapo bungeni

Picha
Mkutano wa 10 wa Bunge umeanza leo Januari 30 mwaka 2018 mjini Dodoma kwa wabunge wapya watatu wa CCM kula kiapo cha uaminifu mbele ya Naibu Spika, Dk Tulia Ackson. Wakati wabunge hao wakila kiapo, takribani wabunge 50 wa upinzani walikuwa nje ya ukumbi wa chombo hicho cha kutunga sheria. Walioapishwa ni Dk Damas Ndumbaro (Songea Mjini), Justin Monko (Singida Kaskazini)  na Dk Stephen Kisurwa wa Longido. Pia, Dk Tulia aliomba wabunge kusimama kwa dakika moja kumkumbuka aliyekuwa mbunge wa Songea Mjini, Leonidas Gama ambaye alifariki dunia Novemba mwaka jana.

LIVE UPDTES: Hali Ilivyo Kenya, 'Raila Odinga Akijiapisha Kuwa Rais'....Matangazo ya TV Yamezimwa

Picha
Hali ya wasiwasi imetanda nchini Kenya baada ya kiongozi mkuu wa upinzani nchini humo Bwana Raila Odinga, kushikilia kuwa ataapishwa leo kama rais wa nchi hiyo. Muungano wa upinzani National Super Alliance (Nasa) umesema hafla hiyo itafanyika katika uwanja wa Uhuru Park, Nairobi. Baada ya sherehe hizo kuahirishwa mwezi uliopita, muungano mkuu wa upinzani nchini humo-NASA, bado unaendelea na msimamo wake wa kuwaapisha viongozi wake Raila Odinga na Stephen Kalonzo Musyoka, kama Rais na Makamu wa rais wa Jamhuri ya Kenya. Maafisa wa polisi walifika asubuhi na mapema katika uwanja wa Uhuru Park, Nairobi unaopanga kutumiwa na muungano wa Nasa kwa shughuli ya kumuapisha Bw Odinga. Kituo cha habari cha kibinafsi cha Citizen kimeripoti kuwa maafisa wa polisi wameamrishwa kuondoka katika uwanja wa Uhuru Park. ==>Mabasi ya wafuasi wa upinzani yazuiwa Voi Mabasi matatu yaliyokuwa yanawasafirisha wafuasi wa upinzani waliokuwa wanaelekea Nairobi kuhudhuria sherehe ya kuapishwa kwa kiongoz...

Waziri Mkuu asema Afrika imeazimia kujiimarisha kuzalisha umeme

Picha
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema nchi za bara la  Afrika zimeazimia kujiimarisha katika uzalishaji wa umeme hadi vijijini ili uweze kuleta maendeleo. Taarifa iliyotolewa leo Januari 30, mwaka 2018 na ofisi ya Waziri Mkuu imesema Majaliwa ametoa kauli hiyo jana Januari 29, 2018 baada ya mkutano wa viongozi wakuu wa nchi za Afrika uliofanyika mjini Addis Ababa, Ethiopia. Amesema nchi hizo zimeazimia kuzalisha umeme mwingi kwa lengo la kuinua kiwango cha maisha ya wananchi wake na kuharakisha maendeleo ya kiuchumi Katika mkutano huo ambao Majaliwa alimuwakilisha Rais John Magufuli, amesema nchi za Afrika zimejipanga kuzalisha umeme wa kutosha mijini na vijijini. Amebainisha kuwa nchi hizo zinatakiwa zijitegemee kiuchumi, ambapo nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) na jumuiya nyingine za Afrika zimefikia mapendekezo ya kuimarisha uzalishaji wa umeme. “Tanzania iko vizuri kwa sababu ina vyanzo vingi vya kuzalisha umeme na sasa ina mikakati ya kuzalisha umeme wa kutos...

NECTA Watangaza Matokeo ya Kidato Cha Nne 2017....Bofya Hapa Kuyatazama

Picha
Matokeo ya kidato cha nne yametangazwa rasmi na Katibu Mkuu wa Necta,  Dk Charles Msonde ==>Yatazame hapo chini Link 1: MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2017 Link 1: MATOKEO YA MTIHANI WA MAARIFA (QT) 2017 Link 2: MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2017 Link 2: MATOKEO YA MTIHANI WA MAARIFA (QT) 2017

Lowassa, Njoolay Wazipangua Tuhuma za Kigwangalla.....Sumaye Kaahidi Kumshitaki Mahakamani

Picha
Familia ya Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, Sumaye na  na Njoolay imetupilia mbali madai yaliyoelekezwa kwake na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamis Kingwangalla, jana. Katika madai yake aliyoyatoa wakati wa kuzindua Bodi ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), Njiro mjini hapa, Dk. Kigwangalla alidai Lowassa ni sehemu ya watu waliojipatia eneo katika eneo la mamlaka hiyo. Msemaji wa familia ya Lowassa, Fredrick Lowassa, alitupilia mbali madai yaliyotolewa na Dk. Kigwangalla huku akisema familia yao inatambua kumiliki eneo hilo kihalali. Akizungumzia tuhuma hizo Sumaye huku akicheka alisema,  “...Nitampeleka mahakamani. Nyinyi cha kufanya andikeni hicho alichokisema vizuri ili nimpeleke mahakamani. Sina nyumba yoyote Arusha sasa kama anadhani yeye kazi yake ni kuwachafua watu acha aendelee, nampeleka mahakamani.” Fredrick katika ujumbe wake alioutoa mara baada ya baba yake(Lowassa) kutajwa alisema, “Nimesikia taarifa za Kigwangalla akitaja...

Breaking News: Necta Yatangaza Matokeo ya Kidato cha Nne

Picha
Matokeo ya kidato cha nne yametangazwa rasmi na Katibu Mkuu wa Necta,  Dk Charles Msonde na aliyengoza kitaifa ni Ferson Mdee kutoka Marian Boys.

Wanaokopa Matrilioni Nje Ya Nchi Kwa Dhamana ya Ardhi ya Tanzania Kubanwa Zaidi

Picha
Bunge  limesema limebaini ardhi ya Tanzania imewekwa dhamana ya mkopo katika benki za ughaibuni na baadhi ya Watanzania na raia wa kigeni waliokopa matrilioni ya shilingi. Hayo yalielezwa mwishoni mwa wiki na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, Mohamed Mchengerwa Mchengerwa alisema kamati yake, mbali na mambo mengine, imetaarifiwa na serikali kuwa kuna Watanzania na Wakenya wachache wamekopa matrilioni ya shilingi katika benki za ughaibuni wakiweka dhamana mashamba yaliyopo nchini. Alisema changamoto hiyo ndiyo iliyoilazimu serikali kuwasilishaMuswada wa Marekebisho ya Sheria mbalimbali Na.5 wa Mwaka 2017 ambao umeigusa Sheria ya Ardhi, ili kutunga sheria ambayo itaondoa mwanya huo, akidokeza kuwa Sheria ya Ardhi iliyopo ina dosari ya kutokuwa na kipengele kinachodhibiti hali hiyo. Muswada huo unaotarajiwa kusomwa kujadiliwa katika mkutano wa 10 wa Bunge la 11 unaoanza leo, ulisomwa kwa mara ya kwanza bungeni Novemba, mwaka jana, wakati wa mkutano ulio...

Ngoma, Kamusoko Warejea Uwanjani Baada ya Kupona Majeraha

Picha
BAADA ya juzi Jumamosi, timu ya Yanga kufanikiwa kuifunga Azam FC mabao 2-1, habari njema kwa wapenzi na mashabiki wa timu hiyo ni kwamba, muda wowote kuanzia leo, mshambuliaji wa kutumainiwa wa timu hiyo, Mzimbabwe, Donald Ngoma atarejea uwanjani baada ya kupona majeraha yake yaliyokuwa yakimsumbua. Ngoma amekuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu na kushindwa kuitumikia timu yake hiyo ya Yanga kutokana na kusumbuliwa na nyonga aliyoumia Septemba 30, mwaka jana wakati  ilipokuwa akiitumikia timu hiyo dhidi ya Mtibwa Sugar katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. Kukosekana kwa Ngoma timu hiyo kupunguza makali yake katika safu ya ushambuliaji, jambo ambalo hiyo. Akizungumza na Jumatatu, Mwenyekiti wa ya Yanga, Hussein Nyika, alisema kuwa Ngoma hivi sasa yupo fi ti na alikuwa akiendelea na stamina katika moja ya gym zilizopo jijini Dar es Salaam na programu yake hiyo ilimalizika jana Jumapili. “Kwa hiyo muda wowote kuanzia leo, Ngoma ataanza kufanya mazoezi ya uwanjani pamoj...

Rita Kuwachulia Hatua Wafungishaji Ndoa

Picha
Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini nchini RITA, imesema, ndoa zote zilizofungwa bila kuzingatia sheria ya ndoa ikiwemo viongozi wa dini waliofungisha ndoa hizo kutokuwa na Leseni ya kufungisha ndoa huenda zikabatilishwa. Afisa Usajili Msaidizi wa RITA Jane Barongo, amefafanua kuwa ndoa hizo zitabatilishwa tu endapo itabainika viongozi waliofungisha ndoa hizo hawakuwa na Leseni ya kufungisha ndoa kutoka serikalini. Barongo ameongeza kuwa kiongozi wa dini atakayebainika kufungisha ndoa bila kuwa na Leseni ya serikali anaweza kuchukuliwa hatua za kisheria kwa mujibu wa sheria ya ndoa ambayo imeipa Rita mamlaka ya kisheria, kusajili ndoa zote zilizofungwa kihalali. Kwa upande mwingine amesema tayari serikali imewakumbusha viongozi wote wa dini kuhakikisha wanakamilisha taratibu za kukata Leseni ya kufungisha ndoa kabla ya kufungisha ndoa yoyote nchini.

Odinga Anatarajiwa Kuapishwa Leo na Upinzani Nchini Kenya

Picha
Viongozi wakuu wa Muungano wa upinzani nchini Kenya NASA, wametangaza kuwa maandalizi yamekamilika kuelekea kumuapisha kiongozi wake Raila Odinga kama rais wa watu leo January 30, 2018 katika bustani ya uhuru jijini Nairobi. Mkurugenzi Mkuu wa NASA Norman Magaya amewaambia wafuasi wa NASA kukusanyika katika uwanja wa Uhuru Park kwa maandalizi ya kumuapisha Odinga na Naibu wake Kalonzo Musyoka saa nne asubuhi. Wasiwasi umetokea kuhusu iwapo shughuli hiyo itafanyika katika bustani hiyo baada ya jeshi la Polisi kupiga marufuku mkusanyiko wa watu katika bustani hiyo. Kamanda wa jiji la Nairobi Japhet Koome, amesema hataruhusu yeyote kuonekana katika bustani hiyo.“Siwezi kuruhusu watu kwenda kuumizana katika bustani ya Uhuru Park,”.

Asha Baraka Amjia Juu Alichoki "Sitaki Ali Choki Afie Kwangu''

Picha
Baada ya msanii wa mziki wa Dance Ali Choki kupiga stori na eNEWZ wiki chache zilizopita na kusema mwaka 2018 atafanya kazi zake mwenyewe kama Mama Asha Baraka ataendelea kulala, kiongozi huyo wa Twanga Pepeta amemjibu Choki. Mama Asha Baraka baada ya kusikia kauli hiyo  amesema anamshangaa sana Ali Choki kusema maneno hayo kwani tangu mwaka jana alishamruhusu akafanye kitu anachotaka hata kama ikiwa ni pamoja na kazi zake binafsi. ''Namshangaa sana Ali Choki mimi nishampa ruhusa afanye kazi nyingine yoyote bila kujali mkataba wetu unasemaje hivyo yeye aendelee na mambo yake wala asinifikirie'' amesema. Asha Baraka pia amesema kuwa hataki Ali Choki afie Twanga Pepeta hivyo kama ana uwezo arudi akaifufue  Extra Band kwani alimpa uongozi ndani ya Twanga Pepeta akashindwa kuiongoza. Ali Choki tayari ameshaonekana akiingia  studio na msanii Beka Flavour kuandaa kazi zake binafsi hivyo huenda akawa tayari ameshajiandaa na maisha bila ya Twanga Pepeta. Zaidi tazama eNEWZ...

Bodi ya Filamu Wamaliza Beef na Kampuni ya Utaarishaji wa 'Filam Utu Wangu'

Picha
Bodi ya Filamu Tanzania (KBF) kupitia kwa Katibu Mtendaji wake Bibi. Joyce Fissoo, wamefanikiwa kumaliza tofauti zilizokuwepo kati ya Sikujua Mbwembe ambaye ni mtayarishaji wa filamu ya ‘Utu Wangu’ dhidi ya Kampuni ya Steps Entertainment. Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Steps Entertainment Dilesh Solanki akibadilishani mihutasari ya kikao cha usuluhi wa madai ya msanii wa filamu Sikujua Mbwembwe Sikujua alikuwa na tofauti na kampuni hiyo ya usambazaji wa filamu kutokana na kuidai fedha zake kutoka kwenye filamu hiyo ambapo kutokana na kikao hiko ameahidiwa kulipwa fedha zake hizo anazodai kuanzia February 5 ya mwaka huu. Soma barua hiyo hapo chini. Hatimaye Bodi ya Filamu nchini imerejesha furaha kwa msanii na mtayarishaji wa filamu ya Utu Wangu kufuatia kuongoza kikao cha usuluhishi kilichofikia muafaka kwa msanii huyo kulipwa stahiki zake. Hayo yamejitokeza leo wakati wa kikao cha usuluhishi wa madai ya Msanii Sikujua Mbwembe mtayarishaji wa Filamu ya Utu Wangu dhidi...

Kigwangalla Awataja Vigogo Watano Waliochukua Maeneo ya Hifadhi Akiwemo Lowassa na Sumaye

Picha
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla amesema vigogo watano ni miongoni mwa wanaotajwa kuwa ni kati ya watu 83 waliochukua maeneo na kujenga nyumba katika kiwanja cha Mamlaka ya Hifadhi Ngorongoro (NCAA), wakiwamo mawaziri wakuu wa zamani, Edward Lowassa na Frederick Sumaye. Akizungumza na wajumbe wa bodi mpya ya NCAA aliyoizindua jana, Dk Kigwangalla alisema mwingine ni Daniel Ole Njoolay ambaye aliwahi kuwa mkuu wa Mkoa wa Arusha, ambaye alisema ameshangazwa na madai hayo. Aidha, Lowassa kupitia kwa mwanae, Fredrick ambaye ndiye msemaji wa familia amepangua tuhuma hizo huku Sumaye ambaye alikuwa waziri mkuu tangu mwaka 1995 hadi 2005, akisema atamburuza mahakamani Dk Kigwangalla kwa maelezo kuwa hana nyumba katika eneo hilo wala jijini Arusha. “Nimewataja hawa baadhi, najua kuna wengine, sasa naipa jukumu bodi na menejimenti kuendelea kuwataja na hatua za kurejesha ardhi zianze,” alisema. Waziri huyo alisema tayari ameshamueleza Waziri wa Ardhi, Nyumba ...

Ebitoke " Pamoja na Kujilengesha Bure ila Ben Pol Kanipotezea'

Picha
MCHEKESHAJI, Anna Exavery ‘Ebitoke’ amefunguka kuwa hajawahi kuachana na msanii, Ben Pol isipokuwa aliona jamaa kama amempotezea hivyo akaamua kujiweka kando.  Akizungumza na Full Shangwe, Ebitoke alisema hajawahi kuachana na Ben Pol ila alipoona yuko kimya na yeye akaamua kukomaa na mishe zake.  “Hatujawahi kuachana na Ben Pol, niliona yuko kimya na mimi ikabidi nikomae na mishemishe zangu, ila sisi bado ni washkaji ,” alisema Ebitoke. Na Gabriel Ng’osha

Baada ya Video ya Wema na Diamond Kusambaa Mitandaoni Mama Diamond Afunguka Haya

Picha
Maneno yamekuwa mengi baada ya Wema Sepetu kupanda kwenye stage na kumuita Diamond Platnumz wakiwa Maisha Basement na wengi  kujiuliza kuhusu ukaribu wao tokea wakiwa Hyatt Regency katika utambulisho rasmi wa msanii Marombosso katika record label ya WCB. Mama Diamond akaamua kupost instagram sehemu ya video clip Wema akiwa kwenye stage na kuandika “KWA HERUFI KUBWA NYIE ONGEENI CHAMBANENI CC TUNAPIGA PESA”