MKE WAZAMANI WA MBUNGE WA UKAWA FAIZA ALLY AAMUA KUMRUDIA MUNGU

NA RICHARD BUKOS

UNAMKUMBUKA yule mwanadada ambaye umaarufu wake kwa kiwango kikubwa umetokana na kupiga picha za nusu utupu? Huyu ni Faiza Ally na habari njema ni kwamba, sasa ameamua kumrudia Mungu wake kwani amehisi alikuwa anapotea.

Faiza aliliambia Ijumaa kuwa, watu wamekuwa wakimjua kwa staili yake ya kuvaa kihasara lakini sasa hivi ameamua kuswali swala tano.

Akizungumza na paparazi wetu maeneo ya Magomeni Mikumi jijini Dar kulikokuwa na dua ya kumuombea Msanii wa Filamu, Salim Ahmed ‘Gabo’, Faiza alisema: “Unajua Mungu ndiyo kila kitu, huwa tunajisahau tu lakini ukizinduka ni vyema ukamrudia, kwa hiyo kwa sasa nitakuwa navaa hivi.”

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

CHOMBEZO: UTAMU WA MADAM JESCA

Simulizi; MTOTO WA BOSS WANGU

SIMULIZI FUPI: UCHI WANGU UMENIPONZA