SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Jumapili, 29 Mei 2016

T media news

STAA WEMA SEPETU AMUOMBEA KURA DIAMOND PLATNUMZ KWENYE TUZO ZA BET


Mbali na tofauti zao na Team zao mtandano, staa wa bongo miovie, Wema Sepetu amewaomba mashabiki wake wampigie kura mpenzi wake wa zamani, Diamond Platnumz ambaye anawania tuzo za BET kwenye kipengere cha Best International Act: Africa.

Wema aliandika haya kwenye ukurasa wakewa Instagram;

“Uzalendo ndo unaotakiwa… Tanzania Kwanza Vingine Baadae… Ama nene…? Vote Vote Vote….,”ameandika Wema kwenye picha ya BET Awards

Mashabiki wengi  amempongeza wema kwa uzalendo aliouonesha.



Katika kipengele hicho Diamond atachuana na wakali wengine kutoka Afrika kama Wizkid, Yemi Alade wa Nigeria, AKA, Cassper Nyovest na Black Koffie wa Afrika Kusini na wengine wawili.