TRUMP AKUMBANA NA UPINZANI WA KIMATAIFA KUHUSU MLANGO WA HORMUZ
Rais wa Marekani, Donald Trump, amejikuta akikabiliwa na upinzani kutoka kwa mataifa mbalimbali duniani kufuatia wito wake wa kuundwa kwa muungano wa kimataifa wa kulinda usafirishaji wa meli katika Mlango wa Hormuz. Njia hiyo muhimu ya bahari ni kiungo kikubwa cha usafirishaji wa mafuta duniani, hivyo mvutano wowote katika eneo hilo huathiri uchumi wa dunia kwa kiasi kikubwa. Katika majibu yaliyotolewa, nchi kadhaa zilionesha tahadhari na kusisitiza kuwa haziko tayari kujiingiza moja kwa moja katika mgogoro huo. Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer, alisema kuwa nchi yake inashirikiana na washirika wake kutafuta suluhisho la kidiplomasia la kuhakikisha usalama wa Mlango wa Hormuz, lakini akaweka wazi kuwa haitakuwa operesheni ya NATO. Kwa upande wa Ujerumani, Waziri wa Ulinzi Boris Pistorius alikataa wazi kushiriki katika mpango huo, akisema kuwa mgogoro huo hauhusiani na nchi yao. Kauli hiyo inaonesha msimamo wa baadhi ya mataifa ya Ulaya ya kuepuka kuingia katika mivut...