Machapisho

Wabunge, Madiwani CHADEMA waandamana kwenda Ubalozi wa Ulaya wahofia maisha yao

Picha
Wabunge na madiwani wa chama cha demokrasia na maendeleo chadema wameandamana kuja ubalozi wa Ulaya kuja kuomba uangalizi wa usalama wakihofia usalama wa maisha yao lakini pia kuomba haki ya dhamana kwenye kesi inayowakabili viongozi wakuu wa chama hicho.

KATA 33 ZA WILAYA YA BUNDA ZAHITIMISHA ZIARA YA MWENYEKITI WA UVCCM WILAYA KWA KISHINDO JIMBO LA BUNDA MJINI

Picha
March 28,2018 Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Bunda *Ndg Gasper Charles* akiambatana na Katiba wa UVCCM Wilaya *Ndg Steven E. Shija* wamehitimisha ziara yao kwa Kata 33 za Wilaya ya Bunda Katika Kata ya Guta na Bunda Mjini Katika Kata ya Guta Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya alipokutana na Baraza Maalumu la UVCCM Kata, alipokea Vijana wapya 20 kuwa Wanachama wapya wa UVCCM baada ya kuona UVCCM ikishughurika na Changamoto za Vijana Pia Katika Kata ya Bunda Mjini Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya, akiambatana na Viongozi Mbalimbali walitembelea shughuri ya Ujenzi wa Mitaro kuboresha Barabara za Mjini, ambapo Mwenyekiti na Viongozi wote walishiriki Katika Ujenzi huo kuonesha kuunga Mkono jitihada za Serikali kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM Vilevile Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya alipokea Wanachama wapya kutoka CHADEMA, walioamua kuungana na Vijana wa CCM kulinda Amani ya Taifa lao na kushirikiana na Serikali katika kuwaletea Wananchi wa Bunda maendeleo _"Tumeona Juhudi za UVCCM k...

TANESCO yakanusha taarifa inayodai kuwa huduma ya mauzo ya LUKU itapatikana katika Ofisi za TANESCO pekee

Picha

Norah Ashindwa Kuficha Hisia Zake Afunguka Anavyomzimia Gabo

Picha
MKONGWE wa sinema za Kibongo, Nuru Nasoro ‘Norah’ amesema kati ya waigizaji wa kiume anaowakubali kutoka Bongo Movies ni muigizaji Gabo Zigamba. Norah alifunguka hilo hivi karibuni alipokuwa akipiga stori mbili tatu na mwanahabari wetu ambapo alipoulizwa kuhusu listi ya wasanii wa kiume anaowakubali Bongo, moja kwa moja alianza kwa kumtaja Gabo. “Wapo wengi ninaowakubali na listi yangu inaongozwa na Gabo namzimia kweli. Wengine ninaowakubali ni JB, Frank Mwikongi, Chiki Mchoma na Dude,” alisema Norah. Alipoulizwa nini kinamvutia zaidi kwa waigizaji hao, alisema ni namna wanavyojua kubadilika kulingana na matakwa ya filamu husika.

Wema Sepetu Ahusishwa Kutumbuliwa kwa Jokate UVCCM Huu Hapa Ukweli Wote

Picha
BAADA ya wikiendi iliyopita aliyekuwa Kaimu Katibu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UV-CCM), Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ kutumbuliwa katika nafasi hiyo, staa wa filamu za Kibongo, Wema Isaac Sepetu ametajwa, Risasi Mchanganyiko linakupa habari kamili. Mara tu baada ya sakata hilo kuchukua nafasi kwenye vyombo vya habari na mitandao mbalimbali ya kijamii, habari za ndani zinaeleza kwamba, Wema alianza kutajwa katika kumrithi mwanadada Jokate kwenye kiti hicho. Chanzo cha ndani ya umoja huo wa vijana kililieleza Risasi Mchanganyiko kuwa, nafasi aliyoondolewa Jokate kuna uwezekano mkubwa wa kushikiliwa na Wema na ndiyo maana siku za hivi karibuni ameonekana kuwa mwenye furaha tofauti na alivyokuwa siku za nyuma. “Nafasi ya Jokate itachukuliwa na Wema na Jokate atapewa nafasi ya juu zaidi ila kwa sasa ni siri kubwa hata ukiwauliza viongozi hawataweza kukueleza kuhusu hilo,” kilidai chanzo. MSIKIE KIONGOZI UVCCM Akizun...

Miguna Atimuliwa Tena Kutoka Kenya na Kupelekwa Dubai

Picha
Mwanasiasa wa upinzani Kenya aliyeidhinisha kiapo cha kiongozi wa upinzani Raila Odinga kuwa 'Rais wa Wananchi' Januari Miguna Miguna ametimuliwa tena kutoka nchini humo. Mwanasiasa huyo ametimuliwa huku mzozo kuhusu uraia wake ukiendelea. Bw Miguna ameandika kwenye Facebook kwamba ameamka na kujipata yuko Dubai na kwamba anahitaji matibabu. Amesema anafahamu kwamba kuna mpango wa kumpeleka London lakini anataka kupanda ndege ya kurejea Nairobi pekee. Mwanasiasa huyo amesema amesindikizwa na afisa wa idara ya ujasusi. Serikali imechukua hatua hiyo licha ya kuwepo kwa maagizo ya mahakama ya kuzuia kutimuliwa kwake na ya kuitaka serikali kufanikisha kurejea kwake nchini humo. Mawakili wa Bw Miguna wamethibitisha kwamba aliondolewa nchini humo kwa kutumia ndege ya shirika la Emirates iliyokuwa inaelekea Dubai. Bw Miguna alikuwa amezuiliwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) tangu alipowasili Jumatatu adhuhuri. Mwanasiasa huyo alikuwa anajaribu kurejea kut...

Licha ya Times FM Kuomba Radhi TCRA Yawakalia Kooni Yasema Kibano Kipo Palepale

Picha
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imesema licha ya kituo cha Redio Times kuomba radhi katika kipindi cha mahojiano kati yake na msanii Diamond, hatua ya kufika mbele ya kamati ya maudhui kwa ajili ya kuhojiwa ipo pale pale. Hayo yamesemwa leo Machi 29 na Ofisa Mkuu Idara ya Utangazaji wa mamlaka hiyo, Andrew Kisaka, alipohojiwa na MCL Digital, na kutakiwa kueleza kama uombaji wa radhi  wa kituo hicho ndio salama yao ya kutoitwa mbele ya kamati hiyo kujieleza kwa nini wasichukuliwe hatua. Katika maelezo yake, Kisaka amefafanua kwamba suala la kituo cha Redio au Televisheni kinapokosea ni lazima uongozi wake ufike mbele ya kamati hiyo na kuongeza kuwa hiyo ni sheria hivyo huwezi kuikwepa. Amesema sheria hiyo inabaki palepale hata kama itatokea uongozi huo, ukaomba radhi kwa kupitia njia nyingine kama hiyo waliyoifanya times. Sakata la Diamond, Times FM waomba radhi Akielezea kuhusu adhabu inayotolewa kwa kituo ambacho kimekosea, amesema ni pamoja na kupigwa faini au kufun...