Machapisho

DC ARUMERU AZUNGUMZA NA MADIWANI ARUSHA DC

Picha
Mkuu Wa wilaya ya Arumeru *Mh.Jerry Muro* amewataka madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Arusha Dc kubuni vyanzo vipya vya mapato ili kuongeza kiwango cha ukusanyaji katika halmashauri hiyo. *Dc Muro* ameyasema hayo hii leo katika baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Arusha ambapo amesema kuwa vipo vyanzo vingi vya mapato ambayo halmashauri hiyo inaweza kukusanya na kufika kiasi cha shilingi *billion kumi.* Licha ya kutoa agizo hilo akalazimik kutoa tahadhari ya kutolipwa posho pamoja na kuvunjwa kwa baraza la madiwani kutokana na wao kushindwa kukusanya mapato Mara baada ya kutoa agizo kwa baraza hilo La madiwani mwenyekiti wa halmashauri hiyo ndugu *Noah Lembris* amemsisitizia Mkuu wa Wilaya kuwa watazidi kufuata sheria zaidi ili kufikia maendeleo ya wananchi pamoja. Katika kikao hicho cha baraza la madiwani kimejadili pia changamoto mbalimbali ikiwemo miradi ya maji iliyokwama kwa muda mrefu ambapo mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo *Dr Wilson Charles Mahe...

SHIRIKISHO LA VYAMA VYA WAFANYAKAZI AFRIKA(OATUU) LAMPONGEZA RAIS MAGUFULI KWA VITA DHIDI YA UFISADI NCHINI

Picha
Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Afrika**(OATUU**) lililokutana mjini Dar es Salaam,Tanzania kwa mkutano wa siku limempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.John Pombe Magufuli kwa mapambano ya dhati juu ya vitendo vya Rushwa na Ufisadi. Akisoma maazimio ya kikao hicho Katibu Mkuu wa *OATUU* *Cde Arzeki Mezhoud* amesema kwamba Tanzania ni kati ya nchi chache za mfano wa kuigwa katika mapambano dhidi ya Rushwa Afrika na Rais Magufuli ni kielelezo wa Kiongozi anayechukia Rushwa kwa Vitendo na kwamba *OAATU* inamuunga mkono katika jitihada hizi na asijione yupo peke yake katika vita hii kubwa. Akimkaribisha Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu(Kazi,Vijana na Ajira) *Mh Anthony Mavunde* kupokea maazimio hayo ya *OATUU* kwa niaba ya Serikali,Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania *(TUCTA)* Cde Tumaini Nyamuhokya amesema TUCTA inaunga mkono jitihada za serikali kupambana na Rushwa na muda wote itashirikiana na serikali katika mapambano hayo. Ai...

Makampuni yanayoajiri Vikongwe, kutoa mishahara midogo Kikaangoni

Picha
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, ametoa mwezi mmoja kwa Makapuni binafsi ya Ulinzi kuhakikisha yanarekebisha mfumo wao wa kuajiri pamoja na utoaji wa mishahara kabla ya Wizara yake haijaanza kuyahakiki makampuni hayo. Lugola amesema baadhi ya Makampuni hayo yameajiri wazee wasiojiweza ambao muda wote wanalala na wanasabaisha uhalifu kuendelea kwa kasi, wakati vijana wapo wengi wenye nguvu zao wanaweza wakazifanya kazi hizo kwa umakini zaidi, na pia tatizo lingine wanalipwa mishahara midogo hali hiyo inawafanya pia wajiingize katika uhalifu. Akizungumza na mamia ya wananchi mjini Bunda, mkoani Mara katika mkutano wa hadhara uliofanyika Stendi ya zamani mjini hapo, Waziri Lugola alisema, Serikali ya awamu ya tano kamwe haitataka uzembe, hivyo makampuni hayo yanayovunja utaratibu huo siku zao zinahesabika. Lugola aliongeza kua, licha makampuni hayo yamekua yakiwekeza nchini na pia yanasaidia kufanya doria katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo ya miji, lakini yapo maen...

MKUU MPYA WA WILAYA YA HAI LENGAI OLE SABAYA AAPISHWA KILIMANJARO LEO

Picha
Na Dixon Busagaga wa Globu  ya Jamii, Kanda ya Kaskazini MKUU wa mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Anna Mghwira leo amemuapisha Mkuu mpya wa wilaya ya Hai Mhe. Lengai Ole Sabaya katika hafla fupi ya kuapishwa kwa mteule huyo wa Rais Magufuli katika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wakuu wa wilaya za mkoa wa Kilimanjaro,Wakurugenzi,Makatibu tawala wa wilaya, kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa pamoja na ndugu na marafiki wa mkuu huyo mpya wa wilaya ya Hai. Mkuu mpya wa wilaya ya Hai, Mhe. Lengai Ole Sabaya akila kiapo mbele ya mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Anna Mghwira (hayupo pichani) ,Hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro. Mkuu Mpya wa wilaya ya Hai Mhe. Lengai Ole Sabaya akitia saini katika karatasi ya Kiapo mara baada ya kuapa kushika nafasi ya Ukuu wa wilaya ya Hai. Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Anna Mghwira (kushoto) akitia saini katika karatasi ya kiapo,mbele yake ni...

Umri sahihi wa kufunga ndoa ni huu hapa

Picha
Kwa mujibu wa utafiti wa Chuo Kikuu cha Utah kilichopo nchini Marekani imebainisha kwamba watu ambao wamefunga ndoa kati ya umri wa miaka 28 mpaka 32 wamekuwa na ndoa yenye mafanikio zaidi. Utafiti huo umebainisha kwamba ndoa ambazo zipo katika hatari ya kuvunjika ni zile ambazo mmoja wa wanandoa ana umri wa chini ya miaka 20 na wale waliofunga ndoa wakiwa na umri wa miaka zaidi ya 45 na kuongeza kuwa ndoa hizo hazijadumu zaidi ya miaka mitano. Taarifa za utafiti huo umeongeza kuwa kwa watu ambao wanasubiri kufika umri wa miaka 30 ili kufunga ndoa wanahatari ya kupata shida sana katika miaka mitano ya mwanzo ya ndoa yao Awali ilijulikana kwamba watu wanaofunga ndoa katika umri mkubwa ndiyo wananafasi ndogo ya kuachana, lakini utafiti huu umeonesha kwamba watu wanaofunga ndoa katika umri wa miaka 45 uwezekano wa kupeana taraka unaongezeka kwa asilimia 5 kila baada ya mwaka mmoja. Sababu kubwa inayosababisha watu walio katika umri mkubwa kupeana taraka ni historia za nyuma za kila m...

Dalili za awali za ugonjwa wa figo na jinsi ya kuweka figo zako katika afya bora

Picha
Figo zina majukumu muhimu sana katika mwili wa binadamu- kwanza inaondoa sumu kutoka mwili wa binadamu na kusafisha damu na kutoa sumu zote. Kama figo haifanyi kazi vizuri, basi hii inaweza kusababisha mkusanyiko wa sumu katika mwili na inaweza kusababisha baadhi ya matatizo makubwa ya afya. Dalili za mwanzo za ugonjwa wa figo na jinsi ya kuweka figo zako katika afya nzuri Figo inafanya kazi nyingi muhimu katika mwili wa binadamu 1. Kuweka katika uwiano mzuri kiwango cha maji Figo ina uwezo wa kusawazisha kiwango cha maji katika mwili wa binadamu,na pia inashiriki katika kutoa kemikali kwa njia ya mkojo 2. Kutoa taka mwilini Sisi sote tunajua moja ya kazi kuu za figo ni kusafisha mwili, kutoa sumu,chumvi na urea 3. Kusimamia kanuni za damu Kama kiwango cha oksijeni kitakuwa chini katika figo, itasababisha kuundwa kwa erythroprotein, homoni ambayo inachochea marrow katika mifupa(bone marrow) 4. Kusimamia Kanuni za asidi Hii ni muhimu sana katika kazi za figo, figo zinawajib...

Sugu Atinga Rasmi Bungeni....Wapinzani Walipuka kwa Furaha

Picha
Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi maarufu Sugu, ameingia bungeni kwa mara ya kwanza leo Mei 21, 2018 tangu aachiwe kwa msamaha wa Rais John Magufuli, Mei 10 mwaka huu. Baada ya kuingia bungeni, wabunge wa upinzani walilipuka kwa furaha wakimshangilia huku wakigonga meza zao kwa takriban dakika mbili, hali iliyosimamisha shughuli za Bunge kwa muda. Sugu ameingia ukumbini saa 3:20 asubuhi akiwa ameambatana na mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Kunti Yusuph ambaye alisikika akisema: "Leo bungeni ni Sugu tu." Wakati anaingia, naibu waziri wa Tamisemi, Josephat Kandege alikuwa anajibu maswali ya wabunge, lakini akalazimika kunyamaza kwanza. Sugu alikwenda moja kwa moja kwa mbunge wa Mtama, Nape Nnauye na kumpa mkono kisha  kwa  waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira, Kazi na Watu wenye Ulemavu,  Jenister Mhagama na kumpa mkono. Alielekea kwa mwanasheria mkuu wa Serikali, Dk Adelardus Kilangi na waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Ut...