Machapisho

Waziri Lukuvu Amnyang'anya Ardhi Makonda

Picha
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imesema itamchukulia hatua muwekezaji aliyetoa ardhi kwa serikali ya mkoa wa dar es Salaam kwa ajili ya ujenzi wa viwanda, kwa madai kuwa ardhi aliyoitoa siyo yake. Waziri wa wizara hiyo, William Lukuvi, alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaam na kufafanua kuwa muwekezaji huyo aliidanganya serikali pamoja na kumdanganya mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, ambaye ndiye aliyekabidhiwa eneo hilo kwa niaba ya serikali. Mbali na kosa la kuidanganya serikali, Lukuvi pia alisema atamchukulia hatua mfanyabiashara huyo kwa kumiliki ardhi kinyume cha sheria. Kuhusu Mkuu wa Mkoa , Paul Makonda, Lukuvi alisema tayari amekwishafanya naye mawasiliano na kumuelewesha kuwa alidanganywa kwa kuambiwa kuwa anapewa eneo kwa ajili ya viwanda, huku eneo lenyewe likiwa ni mali ya serikali. Siku ya Jumanne wiki iliyopita Makonda alikabidhiwa ekari 1500 za ardhi na Mkurugenzi wa Azimio Housing Estate Mohamed Iqbal kwa ajili ya ujenzi wa v...

Mbunge Awaomba Wananchi Wampige Mawe

Picha
Mbunge wa Korogwe Vijijini, Stephen Ngonyani maarufu Profesa Majimarefu, ametoa ruhusa kwa wakazi wa jimbo lake kumwadhibu kwa kumpiga mawe iwapo atashindwa kutekeleza ahadi alizoahidi wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa 2015. Majimarefu aliyasema hayo wakati akizungumza kwa nyakati tofauti kwenye mikutano ya hadhara na wananchi wa Vijiji vya Kwemshai, Ngulu na Mlungui, katika ziara yake jimboni mwake. Alisema licha ya kuwa nje ya nchi kwa matibabu, lakini baada ya afya yake kuimarika amerejea nchini akiwa tayari kutatua kero za umma. Aidha, amewaomba wapigakura wake kuendelea kushirikiana naye huku wakimpatia muda kumwezesha kuwatatulia kero hizo.   “Nawashukuru kwa kuniombea pale nilipokuwa nikiugua, nilikuwa nje ya nchi kwa matibabu sala zenu zimeniwezesha kuungana nanyi leo,"  alisema. Aliwaeleza wananchi wa Kijiji cha Mlungi kuwa tatizo la maji na umeme viko mbioni kutatuliwa ndani ya mwaka huu na kwamba wale wanaoeneza maneno kuwa hakutafanyika kitu wanaji...

Hii Ndio Kazi ya Shanga Kiunoni Kwa Mwanamke Pamoja na Maana ya Rangi zake

Picha
Najua wengi mtakuwa mnafahamu rangi na maana zake lakini kwa wale wasiojuwa  ama wanaopenda kuvaa lakini wanajinunulia rangi yeyote huu ndo wakati mwafaka. Wanaume wengi wanaopenda wanawake wao wavae shanga ili kusisimuana tu .Je mnafahamu zinamaanisha nini?....Karibu  tujifunze  pamoja.  Katika swala la mahaba shanga hutumika kusisimuana haswa pale utakapompata mwanaume anayejuwa kuzitumia vizuri na unaweza kuvaa hata kumi ukitaka .  Jana  niliguswa  sana na simulizi la rafiki yangu juu  ya  shanga, hivyo nikaona  boraniandike  na wengne wajue.Hii ni sehem ndgo ya simulizi  lake.   ".........Nilikutana na boyfiriend wangu maeneo ya  Shycom …tukaelekea kwenye disko. Tulikuwa tunacheza madensi, halafu blues, ya Boyz to Men ikaanza kupigwa. Wenye disko walipunguza taa. Mimi na boyfriend wangu tukakumbatiana na kuanza kucheza Blues.  Miili yetu iligusana na akaana kunipapasa taratibu kufuatana n...

Chadema yaweka ulinzi mkali nyumba ya mama Wema......Ni Baada ya Nyumba Hiyo Kupigwa Mawe Usiku

Picha
Nyumba ya mama Wema Sepetu, Mariam Sepetu, iliyopo Sinza Mori jijini Dar es salaam usiku wa kuamkia jana imepigwa mawe juu ya bati kwa muda wa saa moja na nusu. Kutokana na tukio hilo viongozi wa Chadema wamechukua hatua ya kuweka ulinzi mkali nyumbani hapo na kuzungumza kuwa wamegundua kitu ambacho hawatakiweka wazi kwa sasa. Baada ya tukio hilo kutokea mama Sepetu aliwasiliana na mwanae Wema Sepetu pamoja na viongozi wa Chadema, ambapo Meya wa Ubungo, Boniface Jacob alifika na kuangalia hali ya mama huyo na kuamua kuweka ulinzi. ”Tumeshaangalia mazingira yote tumegundua kitu ambacho hatuta kiweka wazi kwa sasa ila tutaweka ulinzi mkali na atakaye jaribu shauri yake hatuta kubali suala hili liendelee kumkuta kamanda wetu na mimi mara kwa mara nitafika kuangalia mazingira” amezungumza hayo Meya wa Ubungo, Boniface Jacob. Meya alifafanua kuwa ulinzi huo hautaishia nyumbani kwa mama Wema bali hata nyumbani kwa Wema Sepetu ulinzi utaimarishwa kwani amegundua wanachama hao wapya w...

Ridhiwani Aanika uhusiano wa Jakaya Kikwete na Lowassa.....Asimulia Jinsi Aliyopigiwa Simu na Baba Yake Baada ya Kupiga Picha na Lowassa

Picha
Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete ambaye pia ni mtoto wa rais mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete ameeleza uhusiano uliopo kati ya baba yake na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kuwa bado ni maswahiba. Ridhiwani ametoa ufafanuzi huo kutokana na imani iliyojengeka kuwa kuna uhasama kati ya Dkt. Kikwete na Lowassa ambao awali walikuwa maswahiba wakubwa kabla ya siasa kuingiza doa kwenye uhusiano huo.  Uhasama huo uliaminika kuwepo na kuongezeka hasa baada ya Dkt. Kikwete kuongoza kamati ya maadili ya CCM iliyoliondoa jina la Lowassa katika orodha ya waliokuwa wakiwania nafasi ya kugombea urais, hali iliyopelekea mwanasiasa huyo kuhamia Chadema na kugombea nafasi hiyo. Akizungumza wikendi hii na mtangazaji wa Clouds FM, Millard Ayo baada ya kuenea mitandaoni picha inayomuonesha akisalimiana na kuteta na Lowassa, Ridhiwani alieleza kuwa hakuna uhasama kati ya baba yake na mwanasiasa huyo mkongwe kama wengi wanavyoamini. Aliongeza kuwa amewahi kuwashuhudia wakizungumza na kuwasili...

Zitto Kabwe Atoa Kauli Nzito Kuhusu Sakata la Godbless Lema....Ataka ofisi ya DPP iwajibishwe

Picha
Kitendo cha Mbunge wa Arusha mjini kukaa rumande kwa zaidi ya miezi minne sasa pasipo kupatiwa dhamana kimemfanya Mbunge wa Kigoma Mjini Mh. Zitto Zuberi Kabwe kushindwa kuzuia hisia zake na kutaka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali iwajibishwe Katika mtandao wake wa kijamii Mh. Zitto amedai kuwa kitendo cha  Mbunge huyo ambaye ni muwakilishi wa wananchi kunyimwa dhamana  ni siasa za ukomoaji ambazo zinajenga chuki kwenye jamii na chuki huwa zinazaa visasi. "Haitoshi majaji kukemea Ofisi ya DPP, Mfumo wetu lazima uweke uwezo wa waendesha mashtaka wa aina ya kesi ya Mbunge wa Arusha Mjini kuwajibishwa. Wanasheria tazameni namna ya kuwajibisha ofisi ya DPP kwa uonevu wa makusudi dhidi ya wananchi"  Ameandika Zitto Kabwe Hata hivyo kauli hiyo ya Zitto imekuja mapema jana baada ya  majaji watatu  kutoka mahakama ya rufaa kuitaka ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa serikali na DPP kuwa makini na kuwataka kuwashikilia watu kwa misingi ya kisheria na kuongeza...

Wanne wasadikiwa kufariki dunia baada ya kuzama mgodini Buhemba

Picha
Siku chache baada ya serikali kuufunga mgodi wa magunga uliopo buhemba wilayani butiama mkoani mara baada ya kuua watu wawili na kujeruhi 13, wachimbaji wengine wanne waliovamia mgodi huo katika shimo namba moja maarufu kama Long Base usiku wa kuamkia leo wanasadikiwa kufariki dunia baada ya kuangukiwa na kifusi walipokua katika shughuli za uchimbaji wa madini kinyemela. Mpaka sasa tayari maiti mmoja imeopolewa huku zoezi la kuopoa miili mingine mitatu linaendelea pamoja na majeruhi saba wapo hospitali. Channel Ten ilifika katika eneo hilo na kazungumza na waokoaji pamoja na mashuhuda katika ajali hiyo na hapa wanasimulia. Masaa machache baadae kamati ya ulinzi na usalama mkoa ikafika eneo la tukio na kuzungumza na wananchi. Kisha agizo likatolewa na mkuu wa mkoa linataka kufungwa kabisa mgodi huo huku eneo hilo likiwekewa ulinzi na askari wa jeshi la kujenga taifa.