SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Jumatano, 28 Februari 2018

T media news

Shilole na Mumewe Wasaka Mtoto


STAA wa Bongo Fleva, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ ameeleza kuwa baada ya kuingia kwenye ndoa miezi kadhaa iliyopita kwa sasa yeye na mumewe, Ashraf Uchebe wako kwenye harakati za kusaka mtoto.

Akibonga na Risasi Vibes, Shilole alisema kama kawaida ya watu wengi huwa wanatarajia tu baada ya ndoa waone matunda ambayo ni mtoto, yeye na mumewe wako kwenye kutafuta mtoto na Mungu akimjalia atapata.

“Kuhusu suala la mtoto kwa kweli ndiyo tunatafuta na Mungu akipenda tutapata tu maana kila kitu hupangwa na yeye,” alisema Shilole.