SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Jumatano, 28 Februari 2018

T media news

Harmonize Awajibu Wanaombeza Kuwa Jaji Kusaka Watangazaji Wasafi TV



Msanii wa muziki Bongo, Harmonize amefunguka nafasi yake ya kuwa miongoni mwa majaji katika kusaka watangazaji wa Wasafi Radio na TV.

 Muimbaji huyo akizungumza visiwani Zanzibar amesema yeye kuwa jaji ni nafasi ambayo anaimudu vizuri bila tatizo. 
“Mimi nakutana na watangazaji kila siku nafanya interview ndani ya Tanzania na nje, so ukiwa na kipaji mimi nitajua tu na kama huna kipaji sitosita kukuambia,” amesema.
Kumekuwa na baadhi ya watu wanahoji iwapo msanii huyo alistahili kuwa jaji kutokana hana uzoefu wowote wa kieledi na utendaji kazi mzima wa vyombo vya habari.