Machapisho

Wakimbiaji wa Kike Wenye Homoni za Kiume Kama Caster Semenya Wabanwa na Kanuni Mpya za Riadha Duniani

Picha
Baadhi ya wakimbiaji wa kike wenye homoni nyingi za kiume watatakiwa kukimbia dhidi ya wanaume au kubadili mashindano mpaka pale watakapopata matibabu, hizi ni sheria mpya zilizotolewa na chombo cha riadha duniani. Sheria, ambazo zitaanza kutumika tarehe 1 mwezi Novemba,zitawahusu wanawake wanaokimbia kuanzia mita 400 mpaka maili moja Mshindi wa mbiao za mita 800 kwenye michuano ya Olimpiki, Caster Semenya ni miongoni mwa watakaoathirika Mkimbiaji wa Afrika Kusini awali alitakiwa kufanyiwa kipimo cha kubaini jinsia na wakuu wa shirika hilo laini majibu hayakuwekwa hadharani. ''Sheria hizo si kuhusu udanganyifu, ni kuhakikisha kunakuwa na michuano ynayofanyika kwa haki na umaana''Rais wa IAAF Lord Coe alieleza akizungumza baada ya kushinda mbio za mita 800 na mita 1500 kwenye michuano ya jumuia ya madola mwezi Aprili,Semenya alisema atakimbia umbali mrefu zaidi Wanariadha wanawake wanaotaka kushindana wanalazimika kupata dawa kwa kipindi cha miezi sita kabla ya ku...

Tambua Vitu Mwanaume Anavyokupima ili Akujue Unafaa Kuolewa Au Ni Hit And Run !

Picha
1. Ukienda kwake ukutane na vyombo vichafu na nguo chafu zimejazana usidhani ni mvivu, ni kamtihani anakupa. 2. Ukiingia kwake ukaona anampigia simu yule dada wa usafi anayekujaga mara moja kwa wiki aje afanye usafi alipwe usidhani eti anajali kihivyo. Anakutest aone kama utasema "Acha baby, ntakufulia mpenzi wangu". 3. Ukikuta kwake amefanya shopping ya vyakula vya kupika kama unga, mchele, na vingine halafu akakwambia mwende ule mgahawa fulani mkapate dinner usidhani eti ana hela kibao ya kutumia! Anakutest aone kama utamwambia mbaki kwake mpike mle. Uko chumba cha mtihani! 4. Siku kakuahidi kukutoa out halafu unafika kwake unakuta kajikunyata kama mgonjwa anakwambia mama ake kapiga simu anaumwa anaomba atumiwe hela. Halafu anakwambia hela aliyo nayo na ukipiga mahesabu unaona ni kama ile ya kutumia mkiwa out. Anakuomba ushauri afanyaje. Wewe unamwambia "Baby twende out, suala la mama nina uhakika kaka zako na dada zako watalishughulikia, atawapigia". Woiyeeee...

Mambosasa afunguka sakata la Katibu wa BAWACHA Aliyekamatwa na mtoto mchanga

Picha
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Jijini Dar es salaam, Lazaro Mambosasa, ametolea ufafanuzi suala ambalo limeanza kushika hatamu mitandaoni la kukamatwa kwa Katibu wa Baraza la Wanawake CHADEMA kata ya Kisutu Elizabeth Mambosho na kupelekwa rumande akiwa na mtoto mchanga. Kamanda Mambosasa amesema mwanamke huyo alishaachiwa kwa dhamana, na kwamba kesi yake inachunguzwa na makao makuu, licha ya kutoweka wazi sababu ya kukamatwa kwake. “Alikamatwa wakati mimi nipo safarini na alishadhaminiwa, na kesi yake inapelelezwa makao makuu, lakini sijui sababu ya kukamatwa kwake labda muwaulize makao makuu”, amesema Kamanda Mambosasa. Taarifa za kukamatwa kwa Elizabeth zimezagaa mitandaoni huku watu wakilalamikia kitendo cha kukamatwa akiwa na mtoto wake mchanga aliyejifungua wiki tatu zilizopita, huku akiwa na mshono kwani imeelezwa alijifungua kwa njia ya upasuaji.

Mbeya City Yamponza Kocha wa Simba, Yanga

Picha
WAKATI homa ya mchezo wa Ligi Kuu Bara kati ya Simba na Yanga ikizidi kupamba moto, uongozi wa Bodi ya Ligi Tanzania (TPLB) kwa kushirikiana na Kamati ya Waamuzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) umekumbana na changamoto kubwa kuhusiana na mwamuzi atakayechezesha mechi ya watani hao wa jadi itakayofanyika Aprili 29, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Changamoto hiyo inatokana na mwamuzi aliyekuwa amepangwa kuchezesha mchezo huo hapo awali kukumbana na kashfa ya kuboronga katika mechi ya Ligi Kuu Bara kati ya Mbeya City na Yanga iliyofanyika hivi karibuni kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya. Mwamuzi wa mechi hiyo alikuwa ni Shomary Lawi kutoka Kigoma ambaye anadaiwa kushindwa kuumudu mchezo huo kutokana na kukosa umakini baada ya kuruhusu mchezaji aliyekuwa amefanyiwa mabadiliko kuingia tena uwanjani na kuendelea na mchezo. Habari za kuaminika ambazo Championi Jumatano limezipata kutoka ndani ya TFF zimedai kutokana na Lawi kuboronga kwake katika mchezo wa M...

Hapa Ndipo Atakapozikwa Obama?

Picha
Marais saba wa Marekani na wake zao wamezikwa katika maeneo ya maktaba na makumbusho zilizobeba kazi zao za tangu ujanani hadi katika uongozi wa Taifa hilo. Pia marais wote wa Taifa hilo wana utamaduni wa kutaja eneo watakalozikwa, kwa kuwa utangazaji hufanyika mara tu waingiapo Ikulu au wawapo katika mbio za kuwania kuingia Ikulu. Hatua hiyo hufanyika ili kutoliweka Taifa katika sintofahamu pindi wanapoondoka duniani ghafla. Kwa sasa Marekani haina sheria ya eneo maalumu la mazishi ya viongozi kama zilivyo baadhi ya nchi zilizoendelea kutokana na kila mmoja kuwa na wosia wake tangu anapoanza maisha ya kujitegemea. Hata hivyo, wakati huo ukiwa utamaduni wa kawaida wa marais hao kuwa na mahala wanapochagua kuzikwa washindapo uchaguzi kwa mara ya kwanza, Rais wa 44 wa Taifa hilo, Barack Obama hakufanya na hajafanya hivyo hadi sasa. Maeneo walikozikwa marais wa Marekani yapo katika majimbo 23 ikiwemo District of Columbia. Marais 45 wameitawala nchi hiyo tangu mwaka 1789. Kati yao, 38...

Serengeti Boys Yatinga Fainali Michuano ya CECAFA

Picha
Vijana wa Serengeti Boys imefanikiwa kutinga hatua ya fainali ya michuano ya CECAFA chini ya umri wa miaka 17 inayoendelea huko nchini Burundi. Serengeti Boys wamefanikiwa kutinga kwenye hatua hiyo baada ya kuifunga Kenya kwa mabao 2-1 kwenye mchezo huo ambao umechezwa kwenye uwanja wa Muyinga. Mabao ya Serengeti yamefungwa na Jafar Juma (21) na Kelvin Paul (62).

Professor Jay Alivyoingia na Style ya Kurap Bungeni

Picha
Hapa nakukutanisha na Mbunge wa Mikumi Joseph Haule maarufu Professor Jay baada ya kupewa nafasi ya kuchangia mapendekezo yake katika makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ambapo akaamua kuingiza style za kurap baada ya kupewa dakika chache za kuchangiua. VIDEO