Machapisho

Maandamano ya Ukuta ni ndoto ya mchana’

Picha
MSOMI maarufu nchini, Profesa Benson Bana na mwanasiasa aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa chama cha NCCR-Mageuzi, Leticia Mosore wamesema maandamano yaliyopewa jina la Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania (Ukuta), hayawezekani kwani ni ndoto ya mchana na hayana msingi wowote wala tija kwa wahusika hata kwa Taifa. Aidha, maandamano hayo ya nchi nzima imeelezwa kuwa ndio kifo cha Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kwani kila chama kimekuwa kikihangaika kivyake. “Wanaotaka kuandamana wanajidanganya na kuwalaghai wenzao kwani kufanya operesheni ni suala la dola na si la mtu au kikundi cha watu, hivyo maandamano hayo hayawezekani kabisa,” alisema Profesa Bana katika mahojiano maalumu na Idara ya Habari (MAELEZO). Mhadhiri huyo Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, aliongeza kuwa wanaojiita Ukuta ni kwamba Rais John Magufuli amewanyima ajenda, kwani utendaji wake umezidi fahamu zao na kuwafanya waanze kutapatapa wasijue nini cha kufanya. Alisema kama viongozi wa Ukuta ni w...

FASHION YA BEYONCE KWENYE TUZO ZA MTV VMA 2016 HAIJAWAHI TOKEA

Picha
Queen B, naweza nikasema kwamba tangu kipindi cha Destiny Childs miaka ya 90’s, Beyonce ni moja ya wasanii ambao wanajua kwenda na Fashion na kukamata macho ya watu kila wanapokuwa kwenye Red Carpet. Beyonce ni Moja ya wasanii ambao walikuwa wanapita kwenye Red Carpet ya MTV VMA 2016 na kukamata macho ya watu wengi na kufanya midomo ya watu kuwa wazi kwa muda, 100% hili gauni alilovalia ambalo linamuonekano kama wa Malaika hivi, huku kwenye mabega kukiwa kumezungukwa na kama Manyoya flani hivi ambayo yanavutia, hili gauni limetisha kinoma noma. Ukiachana na Bey kwenye mitupio hiyo, Blue Ivy naye alikuwa sambamba na Mama yake akiwa anafuata fashion za Bimdash wake. Hebu Tazama hapa Mama na Mwana walivyopendeza, Kama Nanii vile… Hiyo ilikuwa ni kwa upande wa Red Carpet, Sasa Beyonce aliamua kuonyesha ni jinsi gani alivyokuwa hana ziki kwenye upande wa Fashion, Kila Tuzo ambayo alikuwa akipokea alikuwa anakuja na Fashion nyingine ambayo bado ikawa inazidi kuteka bongo za...

Makusanyo Kodi za Simu Yapanda Maradufu

Picha
Sheria ya Fedha ya Mwaka 2016 iliyopitishwa kuhusu utozaji ushuru kwenye ada ya kutuma na kupokea fedha kwenye miamala ya benki na simu, imeanza kuzaa matunda kutokana na ongezeko la mapato lililoanza kushuhudiwa kutoka kampuni za simu. Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu iliyokutana jana na Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA), iliambiwa kutokana na sheria hiyo iliyopitishwa Bunge baada ya kupitisha bajeti ya mwaka huu, mwezi uliopita serikali imeshuhudia ongezeko kubwa la mapato, yaliyotolewa na kampuni za simu. Taarifa hiyo ilitolewa jana kwenye Kamati ya Kudumu ya Miundombinu, imeonesha Kampuni ya Vodacom ilikuwa ikitoa kodi ya ushuru wa bidhaa kwa fedha zinazotumwa kwa wastani wa Sh milioni 360 kwa mwezi, lakini baada ya mabadiliko ya sheria, Julai pekee mwaka huu imelipa Sh  bilioni 1.9. Mwakilishi wa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato (TRA), Godwin Barongo aliiambia kamati hiyo kuwa kwa upande wa Kampuni ya Tigo, walikuwa wanatoa wastani wa Sh milioni 250 kwa mwezi, lakin...

JOE HART KILA KITU TAYARI TORINO, BADO KUTANGAZWA TU

Picha
Klabu ya Torino inayoshiriki Ligi Kuu nchini Italy ‘Serie A’ muda wowote kuanzia sasa inaweza kutangaza kumsajili kwa mkopo kipa namba moja wa England Joe Hart kutoka klabu ya Manchester City. Jana mlinda lango huyo alipewa kibali cha kuodoka kambini na Chama cha Soka nchini England (FA) kwenda Torino kufanya vipimo vya afya. Hart alianza kupata wakati mgumu punde tu baada ya kuwasaili Pep Guardiola na kuambiwa kwamba yuko huru kuondoka endapo itatokea klabu yoyote inayomhitaji. Hart (29) alionekana kwenye picha jana akiwa jijini Turin na anatarajiwa kukamilisha uhamisho wake kabla ya dirisha la usajili kufungwa leo usiku. Hart atarejea kujiunga na wenzake kambini kuelekea mchezo wa kufuzu fainali za Kombe la Dunia mwaka 2018 dhidi ya Slovakia punde tu baada ya usajili wake kukamilika. Tangu msimu mpya wa EPL uanze, Hart hajacheza hata mchezo mmoja chini ya utawala mpya wa Guardiola ambaye tayari ameshamsajili kipa mpya kutoka Barcelona Claudio Bravo mwenye umri wa mia...

KASHFA:MENEJA WA DIAMOND ASEMA,MAVOKO ZILIPENDWA,HARMONIZE NA RAYMOND NDIO BRAND

Picha
Kumekuwa na maneno mengi ya watu wakidai kwamba timu ya WCB inawekeza sana kwa wasanii wake wawili Harmonize na Raymond kuliko kwa Rich Mavoko. Alipoulizwa kuhusu suala hilo,mmoja wa mameneja wa Diamond,Sallam alisema kwamba wanatumoia nguvu kubwa kwa Harmonize na Raymond kwa sababu ni wasanii wapya kwenye game ukilinganisha na Rich Mavoko. “Rich mavoko ni wa siku nyingi watu washamuona tayari,na sisi tunajua thamani ya Rich Mavoko ndio maana yuko WCB,lakini Raymond na Harmonize ni wasanii wapya,ndio wamekuja.Lakini kama unavyoona project ya kwanza ya Rich Mavoko imetoka,nyingine inakuja hivi karibuni” alifunguka meneja huyo.

MASANJA MKANDAMIZAJI , MPOKI WAINGIA KATIKA BIFU ZITO

Picha
  Siku chache tangu m c h e k e s h a j i mwenye jina kubwa Bongo, Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’ auage ukapera kufuatia ndoa yake iliyozua gumzo, nyepesi nyepesi za mjini zinasema kuwa kutoonekana katika shughuli hiyo kwa msanii mwingine, Silvery Mujuni ‘Mpoki’ kunatokana na bifu zito lililopo kati yao, Risasi Mchanganyiko limedokezwa. Mpoki na Vengu walikuwa ndiyo wasanii pekee wa kundi mahiri la vichekesho la Orijino Komedi ambao hawakutokea katika shughuli hiyo ambayo awali ilianzia katika Kanisa la Miito ya Baraka Kariakoo na baadaye katika Ukumbi wa Prime Rose, Mbezi Beach jijini Dar. Inafahamika kuwa Vengu ana matatizo ya kiafya na hajaonekana hadharani kitambo sasa.  KISIKIE CHANZO Chanzo chetu ambacho kiliomba hifadhi ya jina lake, kilisema ilikuwa ni jambo la lazima kwa Mpoki kuwepo katika shughuli hiyo, kwani alikuwa jijini, lakini kuwepo kwa tofauti kati yao, kulisababisha mtangazaji huyo wa redio kwa sasa, kutoonekana kwenye harus...

ASAMOAH GYAN AKWAMA KUJIUNGA NA KLABU YA ENGLAND

Picha
Uhamisho wa mkopo wa muda mrefu (msimu mmoja) wa hodha wa Ghana Asamoah Gyan kuhamia klabu ya Reading inayoshiriki ligi daraja la kwanza (Championship) umekwama. Mshambuliaji huyo wa zamani wa klabu ya Sunderland alitarajiwa kujiunga na The Royals akitokea klabu ya Shanghai SIPG ya nchini China. Kwa mujibu wa BBC, Gyan, 30, hatajiunga tena na klabu hiyo baada ya ripoti kutoka kwamba amefeli vipimo vya afya Gyan alifunga magoli 10 kwenye Premier League wakati akiitumikia klabu ya Sunderland kabla ya kwenda kucheza soka kwenye falme za Kiarabu.