Idara ya uhamiaji yatakiwa kuimarisha misako na doria.
w 7/05/2024 07:23:00 PM Serikali imeitaka Idara ya Uhamiaji kuendelea kuimarisha Misako na Doria za kuwabaini Wahamiaji wanaoshindwa kufuata sheria za nchi pamoja na uhalifu unaovuka mipaka. Hayo yamesemwa leo Julai 5, 2024 na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Daniel Sillo wakati akizungumza katika Ufunguzi wa Kikao Kazi cha Kamishna Jenerali wa Uhamiaji na Maafisa Waandamizi kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Baraza la Maaskofu Jijini Dar es Salaam. Mhe. Sillo amewasihi kuzidisha nguvu katika udhibiti kwa kuongeza Misako, Doria na ikiwezekana kuwepo na doria maalum ambazo zitashirikisha wadau mbalimbali na Vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama ili kuwaongezea nguvu kwani nchi ikiwa salama dhidi ya uhalifu itaendelea kuvutia uwekezaji na kuendelea kuwa kivutio kwa wageni. "Kama tunavyofahamu nchi yetu inaelekea katika kipindi cha uchaguzi wa Serikali za mitaa pamoja na uchaguzi mkuu ni vema kuimarisha usalama katika vituo vyetu vyote vya kuingia na kutoka hapa nchini na tuhak...