SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Jumanne, 13 Septemba 2016

T media news

Kauli ya Serikali Kuhusu Polisi Wanaobambikiza Kesi na Adhabu zao

Vikao vya bunge la 11 limeendelea tena leo bungeni Dodoma September 13 2016 ambapo katika kipindi cha maswali na majibu Waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mwigulu Nchemba ametoa ufafanuzi wa swali la mbunge wa viti maalum CHADEMA Susan Maselle aliyehoji hatua za serikali kuhusu baadhi ya wanajeshi kuwabambikia kesi wananchi.

Waziri Nchemba amesema…

’Jeshi la Polisi linafanya kazi kwa mujibu wa sheria, kanuni, miongozo na taratibu. Wale wanaobainika kukiuka maadili ya jeshi huchukuliwa hatua kwa kuwapa adhabu mbalimbali ikiwemo kuwafukuza kazi‘

‘Mtu yeyote anayeona kuwa anaonewa anapaswa kuwasilisha malalamiko yake katika vyombo vya kisheria pindi anapoona hatendewi haki kutoka kwa Polisi kwa mujibu wa sheria za nchi‘ –Waziri Nchemba

Kuhusu tuhuma za Polisi kuwakamata wanasiasa na viongozi wa dini kisha kuwaweka rumande kwa muda mrefu? Waziri Nchemba kasema…

’Jeshi la Polisi halikamati watu kwa itikadi ya dini zao bali huwakamata kulingana na makosa yao na kuwafikisha mahakamani‘