SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Jumapili, 11 Machi 2018

T media news

TANGA RAHA- Sehemu ya Ishirini na Saba ( 27 )

AGE………………18+

WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA 

Rahma akazidi kuongeza kasi ya mashambulizi ila kutokana nimesha mzoe hakunitisha sana zaidi ya mimi kuzibana sehemu zake ambazo siku zote nikimbana huwa niamshinda kwenye mechi zake.Galfa mwili wa Rahma ukaanza kukakamaa huku macho yake yakibadilia na kiini cheusi kikapotea na kukabaikia kweupe tu huku mapuvu yakiaanza kumtoka mdononi kitendo kilicho anza kunichanganya kwani tangu nimjue Rahma sikuwahi kumuaona akiwa katika hali kama hii

ENDELEA

Hali ya Rahma ikazidi kuwa mbaya kitandani na kunifanya nizidi kupagawa hata sikujua nifanye kitu gani kitakachoweza kumrudisha Rahma katika hali yake ya kawaida.Nikasimaa na kuiokota suruali yangu chini na kuivaa kisha nikuitoa simu yangu mfukoni na kukuta haina chaji ikanilazimu kuitafuta simu ya Rahma na ndani ya chumba changu haikuwepo ikanilazimu kwenda sebleni na kuikuta juu ya meza ya chakula nikaichukua na kukuta meseji moja na kwabahati mbaya nikaifungua

‘WEWE RAHMA UPO WAPI TUNAKUSUBIRIA NYUMBANI KWENYE KIKAO HUYU MUME WAKO AMESHA KUJA’

Nikajikuta nikiirudia rudia meseji yake kuisoma kiasi kwamba nikajikuta nikikaa juu ya meza vizuri na kwa haraka namba iliyo tuma meseji ninaifamu ni ya mama yake ambayo alinipa siku moja shuleni.Nikabaki nikiwa nimetulia zaidi ya dakika tano huku nikijikuta rohoni mwangu nikijiwa na wivu mkali ulio andamana na hasira kali,Nikastuka simu yake iikita na kuona ni namba ya baba yake ikiingia na kubaki nikiwa nimeitazama kiasi kwamba nikajikuta nikianza kutetemeka kwa woga,Hadi simu inaka nikajikuta nikiwa kimya nisijue ninafanya nini

Wazo la kumpigia Halda likanijia kichwani na nikaanza kuifungua simu ya Rahma sehemu alipo hifadhi majina ya watu mbalimbali na kujikuta zaidi ya dakika kumi nikilitafuta jina la Hilda ila sikulipata kwani sikujua ameliandika  vipi ndani ya simu yake.Nikasikia honi ikipiga getini na kwaharaka nikajua atakuwa ni Hilda ambeye ameondoka nyumbani kwetu muda si mrefu na kwa haraka nikanyanyuka na kutoka nje na hatua ya kwanza nikachungulia dirishani kutazama ni nani anaye piga honi na kujikuta nikistuka na kajasho kembemba kakianza kunienda mbio,hii ni baada ya kuliona gari jeusi anina ya Land cruser likiwa limesimama nje kwangu huku likiwasha taa zote mbili

“Nani huyu?”

Nilijiuliza mwenyewe kana kwamba kuna mtu pembeni yangu ninaye zungumza naye kumbe nipo peke yangu.Nikamshuhudi Hilda akishuka ndani ya gari hilo na kuanza kupiga hatua za haraka kuja kwenye geti langu kidogo moyo ukanipata matumaini na kujikuta nikulifungua geti na Hilda kwa ishara akamruhusu dereva wa gari kuliingiza ndani na nikabaki nikiwa ni nimeduwaa hadi gari linasimama akashuka jamaa mmoja mweusi kiasi aliye valia vizuri na kujikuta nikirudi katika hali ya kawaida baada ya jamaa kunisalimi

“AHaaa salama tuu kaka karibuni”

Nilizungumza huk u nikiliegesha geti langu na endapo kutatoke ishu yoyote niweze kukimbia kuepukana na msala uliopo ndani

“Eddy huyu anaitwa Rashid ni dereva wao Rahma”

“Ahaa karibu ndugu”

“Asante vipi huyo bibie yupo ndani?”

Swali la dereva nikajifanya kama sijalisikia na kuongoza ndani huku wao wakinifwata kwa nyama na mimi moja kwa moja nikaingia ndani na kuukuta Rahma akiwa ametulia huku mapigo yake ya moyo yakienda taratibu kiasi kwamba nikabaki nikimtazama kwa muda.Nikasikia sauti ya Hilda ikimuita Rahma huku akionekana kuja kwenye chumba chetu ikanilazimu kunyanyuka kitandani kwa haraka na kwenye kuufungua mlango na kumkuta akiwa amesimama mlangoni kwetu

Muambie huyo Rahma kwao wanamsubiria sana na ninampigia simu hapokei”